MUNGU MKUU 5

 


SCENE 5

(Jumamosi nyingine tulivu, kila mtu anaonekana yupo nyumbani na anafanya shughuli zake, Ariana anatoka chumbani kwake akiwa amefura kwa hasira kutokana na uwepo wa Miriam)

Ariana: yaani hili litoto silipendi kweli tangu lije sina raha na maisha yangu na ninatamani hata kuliua

Miriam:(Analia sauti ya kichanga)

Ariana:(anaifata sauti hiyo na kugundua amelala chumbani kwa wazazi wake) cheki linalala utasema limezaliwa humu (anambeba na kuondoka nae) sasa leo ndo siku nitakayo liua hili litoto (anatoka nae nje na kumpeleka mbali sana, anapofika machakani anamtupa na kurudi nyumbani baada ya muda kidogo, anapofika nyumbani anagundua kuwa hakuna hata mmoja aliyehisi kuwa mtoto hayupo) safi sana hakuna aliyegundua kuwa mtoto hayupo

Keddy :( anamjia) mwanangu…ulikuwa wapi sijakuona nilikuja chumbani kwako sijakuona mama umekunywa chai?

Ariana: hapana…shikamoo mama

Keddy: marahaba mama hujambo?

Ariana :( anatabasamu) sijambo…

Keddy: wow…leo unaonekana una furaha kweli mwanangu niambie nini siri ya furaha yako?

Ariana: nimeamka tu vizuri mama

Keddy: safi au ndo umeamua kumkubali mdogo wako?

Ariana: ndio mama nimeona tu nimkubali mdogo wangu na ninaahidi kumpenda kama mdogo wangu wa tumbo moja

Keddy: hongera dada Ariana kwa kubadilika huko…ninafurahi sana mwanangu (anamuita Mary) Mary…Mary

Mary:(anaitikia sauti inatokea jikoni) abeee dada

Keddy: njoo usikie habari njema sana kwa leo jumamosi bwana ametuzawadia habari njema sana leo

Mary:(huku anakuja) nini tena dada?

Keddy: Ariana ameamua kuwa dada mzuri na ameahidi kumpenda sana mdogo wake kuanzia leo

Mary:(anaonyesha furaha) kweli?

Keddya: muulize mwenyewe...

Mary: eti mama ya kweli hayo?

Ariana: ndio ma mdogo ya kweli kabisa…kuwa nimeamua kumpenda na kumthamini Miriam kama mdogo wangu wa damu

Keddy: wow, hii ni habari njema sana kwetu…yaani kila nikikuangalia mwanangu Napata raha sana

Mary:(anafurahi sana tena)

Ken:(anakuja akitokea chumbani na kumkumbatia mwanae ishara ya upendo) malkia wangu hujambo mama

Ariana: sijambo baba shikamoo…

Ken: marahaba mama yangu mzuri… (kwa Keddy na Mary) nyie Miriam yuko wapi?

Keddy:(anacheka) masihala hayo mume wangu

Ken: masihala ya nini tena?

Keddy: wewe si umetoka chumbani baba na mtoto alikuwepo huko?

Ken: hayupo nimetoka chumbani hayupo

Ariana:(anacheka kisirisiri)

Keddy:(anaonekana kuchanganyikiwa sana na habari hiyo) what?

Mary:(anaonekana amehamaki sana) Mungu wangu mwanangu…

Keddy:(anaenda chumbani kuangalia kama ni kweli) Miriam… (anaangalia alipomlaza hayupo) Mungu wangu jamani mwanangu kweli hayupo (anaanza kulia)

Ken:(anamfuata mkewe na kumkumbatia) come down honey

Mary:(anaanza kulia)

Ariana:(anawaangalia tu na wala hana hata wasiwasi)

Ken: mara ya mwisho alikuwa wapi?

Keddy:(huku Analia) nilikuwa nimemlaza hapa mume wangu jamani

Ariana:(anajisemea moyoni) yaani mama bwana yaani mtoto sio mwanae lakini alivyomkomalia utasema ni mwanae wa kumzaa yaani anashindwa kunililia mimi anamlilia huyo mbwa na bora hata nilivyomtupa hana maana mshenzi huyo

Keddy:(kwa Ariana) Ariana mama mdogo wako amepotea sasa sijui yuko wapi…

Mary:(anaendelea kulia kwa uchungu)

Ken:(kwa Mary) Mary…embu msaidie dada yako kwenda kuuliza kwa walinzi huko labda waliona mtu kamchukua

Mary: sawa shemeji… (anatoka kuelekea nje)

Ariana:(anacheka moyoni) yaani hata walinzi hawajui kama nilitoka na huyo mtoto nilimtoroshea mlango wa nyuma (anacheka tena)

Mary:(anarudi ndani) hawajamuona hata wao

Keddy: maskini mwanangu sijui atakuwa wapi…

Ariana: ishi, yaani mama Analia kabisa kisa mtoto ambae hajamzaa?

Keddy: madaktari waliniambia kuwa sina uwezo wa kubeba mimba tena Mungu akaonyesha ukuu wake na kunipa mtoto kwa njia zake mwenyewe leo simuoni sijui yuko wapi…

Mary:(huku Analia) tutampata tu dada usijali dada yangu

Ariana: inamaana hicho kitoto kina nini mpaka kiwe kinapendwa hivyo? yaani na mfanyakazi anamlilia utasema ni mwanae?

Ken:(huku anaelekea nje) ngoja nikatoe taarifa polisi(anatoka)

Keddy: mwanangu…jamani (anamuita Ariana) mwanangu mdogo wako kapotea

Ariana:(anamuangalia tu na wala hana cha kumwambia)

Mary: dada ngoja nikamuangalie nje hapo…sidhani kama atakuwa ameenda mbali

Keddy: nenda mdogo wangu…mi sina hata nguvu za kutembea najisikia vibaya sana

Mary:usiwaze sana(anajisemea moyoni)yaani huyu mama anampenda mwanangu sana mpaka nafurahi(anaondoka na kuenda nje na kuanza kuangalia huku na huku)sijui atakuwa wapi na bora hata angekuwa ni mkubwa kwamba anatembea tungejiuliza kaenda wapi yaani hapa ni wazi tu kwamba kuna mtu kamchukua lakini ni nani na kwa nini yaani sioni hata adui nayemjua mimi anaweza kufanya hivyo au baba yake?lakini angejuaje yote haya kwamba mtoto anakaa hapa hapana sijui ni nani amefanya hivi(anaendelea kumtafuta)mwanangu jamani(kwa mbali anasikia sauti ya mtoto mchanga)mwanangu(anakimbilia ilipo sauti anakuta ni Miriam)jamani mwanangu(anamkumbatia na kumbusu sana)asante Mungu…mwanangu haya twende kwa mama yako anakusubiri(anatoka anakimbia kurudi nyumbani baada ya dakika kadhaa anafika nyumbani)dada,nimempata Miriam

Ariana:(anakasirika sana)

Keddy: umemtoa wapi…?

Mary: vichakani huko…

Keddy: (kwa mshangao) vichakani? Kaendaje?

Mary: hata sifahamu dada mimi nilikuwa natembea tembea nikasikia analia ndo nikamchukua na kumleta huku

Keddy: jamani sasa alienda kimiujiza au?

Mary: hapo ndo sijajua dada nachojua ni kwamba nimempata huko

(Wanabaki wanaangaliana)

Keddy: haya ndo yanaitwa maajabu ya Mungu na ukuu wake unashangaza jamani (anamchukua mtoto na kumbusu na kumkumbatia)

Ariana:(anajisemea moyoni huku anamuangalia Mary) yaani lina kiherehere kweli nani aliliambia litoke humu ndani na likamtafute huyu mtoto natamani nilibamize(anafyonza)

Keddy: Ariana huyu hapa mdogo wako uliyesema utampenda na kumtunza

Ariana:(anaachia tabasamu la uongo)

Keddy: ngoja nimpigie baba Ariana (anachukua simu na kumpigia mume wake) hello baba Ariana

Ken:(anaonekana ndo anatoka kituo cha polisi) naam mama…

Keddy: mtoto amepatikana

Ken: wow…. amepatikana wapi?

Keddy: Mary kamtoa vichakani

Ken: (anashangaa sana) vichakani? Nani kampeleka?

Keddy: sijui mume wangu

Ken: (anaguna)

Keddy: kikubwa tu mtoto amepatikana

Ken: sawa ila lazima tujue mtoto kafikaje vichakani ina maana kuna mtu kampeleka

Keddy: mimi naona tuachane na hilo mume wangu kikubwa tu tumempata

Ken: sawa lakini nataka tu kujua

Keddy: baba Ariana stop

Ken: anyways sawa

Keddy: (anacheka kidogo)

Ken: umefurahi ee

Keddy: sana baba

Ken:(anatabasamu) kama naliona tabasamu lako mke wangu…basi ni sawa kama ni hivyo ngoja nitoe taarifa polisi maana nilikuwa tayari nimeshawataarifu juu ya kupotea kwa mtoto wetu

Keddy: waambie tumeshamuona

Ken: sawa (anakata simu)

Keddy:(anatabasamu) baba Ariana amefurahi pia

Mary: (anatabasamu)

Keddy: alitaka kujua mtoto kafikaje vichakani ila nimeona tu haina maana kikubwa tumemuona

Mary: kwakweli

Keddy: (kwa Ariana) haya mbebe mdogo wako

Ariana: (anambeba kishingo upande)

Mary: (anamuangalia Ariana)

Ariana: (anajichekesha)

Keddy: kweli umefurahi kumuona mdogo wako

Ariana: sana mama si nimekuambia kuwa nitampenda

Keddy: nimekubali mwanangu

Mary: hiyo imekaa vizuri

Keddy: (anatabasamu)

(Wote wanajikuta wanacheka kwa furaha kasoro Ariana anayeonekana kuchukia kupita kiasi, na mara zote wakimuangalia anaonyesha tabasamu ambalo si la furaha bali la kinafki na la kujilazimisha)

Post a Comment

2 Comments