SCENE
52: -
KESHO
YAKE ASUBUHI: -
NYUMBANI
KWA WAZAZI WA MARY: -
(Vincent na Colton wanafika
nyumbani kwa wazazi wa Mary)
Vincent:
hodi humu ndani
Bibi:
karibu baba
Vincent:
shikamoo mama
Bibi:
marahaba…
Dada
yake Mary: karibu…
Vincent:
habari yako
Dada:
nzuri
Colton:
shikamoo
(wanaitikia)
Vincent:
Mary hajafika?
Bibi:
ameenda kumuona mwanae jela yaani Analia tu …amekonda mwanangu yaani ila asante
ni wewe ndo umesababisha tukamtafuta Mary
Vincent:
nilitaka kumuona mwanangu
Colton:
(amekaa kimya)
Bibi: na
huyu ni mwanao?
Vincent:
ndio…mtoto wangu wa kwanza kaka wa huyo bibie…ambae yupo jela au niende
nikakutane na Mary
Colton:
baba
Vincent:
oh, okay nimekumbuka…
Dada:
nini?
Vincent:
hamna kitu
Dada:
nimeona mnakonyezana
Vincent:
usijali
Dada:
niwaletee chai, maziwa au kahawa?
Vincent:
usijali shem
Dada:
hamnywi chochote?
Vincent:
tumetoka tumekula kabisa… (anaangalia simu
yake) Mary nae sijui yuko wapi
Dada:
atakuja tu
Vincent:
natakiwa kwenda kazini
Colton:
msubiri tu dad atakuja
Vincent:
(anakaa anatulia)
Mary: (anakuja) nimechelewa samahanini…za hapa
jamani… (kwa mama yake) shikamoo mama
Bibi:
marahaba mwanangu, mjukuu anaendeleaje?
Mary:
yupo tu mwanangu...analia tu
Dada:
hakuna jambo lililowahi kumshinda Mungu
Mary:
hakika…asanteni sana kwa kunitia moyo (anakaa
kwenye sofa nyuma ya kina Vincent) yule Vince?
Bibi: anakusubiri
kaja na mwanae
Mary: (anawaendea) embu ngoja nikawaone
Colton:
(anageuka kwa mshangao) aunt Mary
Vincent:
unamjua?
Colton:
namjua ndio...
Mary: (anawafikia na anamuona Colton) Colton???
Colton:
ma mdogo
Vincent:
mbona siwaelewi?
Mary: (anasikitika) kwanini umefanya hivi?
Vincent:
eeh basi sina haja ya kuwatambulisha naona mnajuana
Colton:
huyu ni mama yake Miriam binti niliyesababisha aende jela
Mary:
unafanya nini hapa?
Vincent:
jamani
Colton:
nipo na baba yangu huyu hapa nimekuja kumuona mdogo wangu
Mary:
Vincent ni baba yake Miriam
Colton: (anashangaa) kwa maana nyingine
nimemkosea mdogo wangu?
Mary:
yes... kama wewe ni mtoto wa Vincent
basi Miriam
Dada:
makubwa…kwahiyo kaka kamsababishia dada makubwa?
Mary:
ipo hivyo
Vincent:
aisee hii dunia ndogo sana jana alipokuwa ananisimulia nikajua sijui nani yaani
haya sikuwaza pamoja ya kwamba kulikuwa na uwiano kwenye hizi hadithi…mtoto wa Mary
kwenda jela kwa kosa ambalo hakulitenda na Colton kumsingizia mtu na sasa yuko
jela na kwamba zimepita wiki mbili pamoja na kufanana huko hata sikuwaza kama
atakuwa mtu mmoja
Bibi:
aisee…sasa wewe baba unamsaidiaje mdogo wako
Colton: (kwa Mary) naomba unisamehe mama
Mary:
panga tu mipango ya kumsaidia baada yah apo ndo tutaanza kuongea
Colton:
nitafanya ila nani atanisaidia?
Mary:
Jeremy
Colton:
mchumba wake Miriam?
Mary:
ndio
Colton:
ataniua akiniona
Mary: (anashusha pumzi)
Colton:
ma mdogo kaongee kwanza na shemeji
Mary:
hawezi kukufanya chochote…asante Mungu nimekuona Colton sasa mwanangu
hatonyongwa asante sana Mungu wangu kweli umeonyesha UKUU wako jina lako
litukuzwe
Vincent:
(anawaangalia Colton na Mary kwa zamu)
Mary:
nitamwambia Miriam
Vincent:
tulia kwanza…yeye hatutamwambia kwanza...huu mpango tunapanga sisi sasa ni
jeshi la kumsaidia binti yetu
Mary:
asante Yesu
Vincent:
tutapanga kwa ajili ya siku ya hukumu acha tuwaonyeshe kuwa tumeshindwa
Dada:
hapo umenena shem
Vincent:
(kwa Mary) mpigie mkwe tupange
tunakutana wapi…
Mary:
sawa
Colton:
mimi sitaki kuonekana kwa dunia mimi tayari ni marehemu
Mary:
tunakuhitaji lakini
Colton:
najua na nipo tayari kuwapa ushirikiano wa kutosha
Mary:
asante sana...
Vincent:
hilo limeisha
Bibi:
Mungu hajawahi kushindwa
(wanaonekana kuwa na tumaini
jipya)
0 Comments