MUNGU MKUU 55


 

SCENE 55: -

BAADA YA MIEZI TISA: -

HOSPITALINI: -

 (Jeremy, Vincent, Ken, Mary, Keddy wamekusanyika hospitali wanaonekana kuwa wanasubiri kitu Fulani kama habari Fulani)

Jeremy: (anakaa chini baada ya kuzunguka zunguka kwa muda)

Keddy: hatimaye umekaa mwanaume loh

Vincent: (anacheka) bora…

Ken: (anacheka)

(wazazi wa Jeremy wanafika)

David: bado tu?

Ken: bado mwenzangu

Mama: mbona imemchukua muda hivyo? Tangu jana usiku?

Keddy: yaani nawaza kweli sijui yamemkuta yapi?

Mary: Mungu atamsaidia

Jeremy: nyamazeni kidogo mimi mnanichanganya mnajua?

Mary: tulia baba

David: kuwa na kifua unadhani kuwa baba wa familia ni lelemama

Mama: kwani kasemaje?

David: anachanganyikiwa yaani hii hali imchanganye?

Jeremy: najaribu kutafakari baba

David: eeh baba tafakari…

(wanacheka)

Vincent: (anachungulia) nesi bado

Mary: si usubiri mwanaume?

Vincent: kwakweli imechukua muda… wewe bibi mwenye miaka 37

David: bibi mdogo kuliko bibi wote duniani

Mary: jamani ndo raha ya kuzaa ukiwa na miaka 17…miriam ana miaka 20 sasa hivi na anajifungua Napata mjukuu

Keddy: hongera shoga ree sio mimi miaka 45

Jeremy: hata wewe ni bibi kijana

Keddy: unanipa moyo?

Jeremy: kwe… (anamuona nesi haraka anamuendea) nesi

Nesi: (anasimama)

Ken: nesi…

David: tuambie basi

Nesi: hongereni

Jeremy: enhe…

Nesi: amejifungua mtoto wa kike

(wanafurahi kupita kiasi)

Vanessa: (anakuja) nimechelewa?

Jeremy: (anamkumbatia Vanessa) amejifungua mtoto wa kike

Vanessa: (anaruka ruka)

Nesi: mnaweza kumuona

(wanaingia kwa kukimbizana)

Miriam: (bado dhaifu)

Jeremy: (anamkimbilia na kumkumbatia) asante sana (anamuangalia mtoto) oh so sweet anafanana na wewe Miriam

Miriam: (anatabasamu)

David: jamani mjukuu

(wanacheka)

Ken: mjukuu

Vincent: mjukuu

(wanacheka)

Miriam: oh, asanteni kwa maombi yenu nimejifungua salama

Mary: amen mama

Miriam: natamani kaka yangu angekuwepo hapa…

Sauti: (kutoka nyuma yao) mtoto anaitwa nani vile?

(wanageuka)

Vincent: mwanangu

Colton: (anakuja anawakumbatia)

Jeremy: oh shemeji(anamkumbatia)

Colton: (anamkumbatia)

Miriam: oh, Mungu amenipendelea leo nina furaha nimepata mtoto lakini pia kaka yangu ametoka ila nina huzuni maana dada yangu

Keddy: amechanganyikiwa

Miriam: mama

Ken: wamempeleka mirembe…akili yake sio nzuri alianza kama utani hatimaye akawa chizi kabisa

David: haya ni mapito na majaribu siku zote ni mtaji wa kuongeza Imani na Mungu atakapokupa jaribu ni lazima akupe na mlango wa kutokea

Keddy: hakika shemeji

Jeremy: jamani leo ni siku ya furaha naomba tufurahie tafadhali

Ken: yes, embu tufurahie

Vincent: nina habari njema

Colton: ipi tena?

Vincent: mpo tayari kusikia?

Miriam: tupo tayari...

Vincent: mimi n Mary tumeamua kufunga ndoa

(wanafurahia)

Colton: hongereni sana

Miriam: hongereni sana…mwananngu amekuja na Baraka zake

Jeremy: mtoto wetu

Ken: hii ni habari njema sana...tuna harusi mbili sasa za kuandaa harusi ya Mary na Vincent, Miriam na Jeremy

Colton: Colton na Vanessa

Keddy: leo tuna surprise nyingi jamani

Ken: mlianza wapi na lini?

Colton: wakati nipo jela ndo tulianza kupendana, alikuwa anakuja sana yeye na Miriam na alikuwa nanionyesha huruma ya kutosha…niliona moyo wake mzuri alisema atanisubiri hata ningekaa miaka 10 gerezani…

David: tuna harusi tatu

Colton: naomba nianze mimi na Vanessa

Miriam: jamani mambo haya…Vanessa alikuwa rafiki yangu na sasa ni wifi yangu (anatabasamu)

Jeremy: yes, baby...na Colton alikuwa adui yangu na sasa ni shemeji yangu

Keddy: maisha bwana yanakuwa yana mambo mengi sana ila tunayaweza mambo yote katika yeye atutiae nguvu

Miriam: na anayetutia nguvu ni MUNGU pekee… (kwa Ken) Dad dada Ariana atapona na kuwa mzima usisahau ukuu wa MUNGU

Ken: nitausahau vipi ukuu wake?

Miriam: (amebeba kichanga chake)

Mary: kwahiyo mtoto anaitwa nani?

Miriam: Mary Glory

Jeremy: (anatabasamu)

Ken: jina zuri sana

Colton: jina zuri sana

Keddy: nimependa jina

Mary: napenda jina

Vincent: (kwa Mary) huna lolote kisa linaanza na Mary

(wanacheka)

Ken: God bles you child

David: wow jina lina utukufu linapendeza

Miriam: ni Mary Glorify…namtukuza Mungu wangu kwa mambo makubwa aliyonitokea najua ni yeye ndo aliyapanga lakini ninajisikia vizuri sana kwamba linionyesha ukuu wake kwenye hilo hivyo namtukuza na ndo maana mwananngu anaitwa Glorify

Mama Jeremy: hongereni sana kwa kupata mtoto wanangu

Miriam na Jeremy: asante mama

Vincent: jina zuri halafu lina upako

Ken: tuongelee harusi inaanza ya nani?

Miriam: baba na mama

David: yeah sio mbaya halafu anafata Colton na Vanessa

 (Colton na Vanessa wanafurahi)

Keddy: mwisho kabisa Miriam na Jeremy

Jeremy: imekaa vizuri tuanze mipango sasa David: yes, mara moja…

Vincent na Mary: (wanatabasamu)

David: (anambeba kichanga) njoo mke wangu…(anambusu)

Kichanga: (kinajikunja na kucheza cheza)

Post a Comment

0 Comments