MUNGU MKUU 53


 

SCENE 53: -

USIKU WA SIKU HIYO: -

NYUMBANI KWA JEREMY: -

(wazazi wa Miriam wakiambatana na Colton wanafika nyumbani kwa Jeremy)

Jeremy: (anafungua mlango) mama mkwe

Mary: abeee baba

Jeremy: mbona usiku sana kheri? (anaangalia pembeni ya Mary anamuona Colton) Oh God… Colton? (anashangaa sana)

Colton: za jioni shemeji

Jeremy: shemeji?

Mary: tunaomba uturuhusu kuingia ndani

Jeremy: nakuruhusu wewe lakini sio huyu mnyama ni kwasababu yake mchumba wangu yupo jela

Colton: ((kwa unyonge) iam so sorry

Jeremy: tell me umefaidikiaa nini… (kwa ukali) nakuuliza umefaidika nini?

Vincent: msamehe ndo maana tumekuja kujua tunafanyaje

Jeremy: mpenzi wangu anateseka kumbe wewe hukufa … (anachukia sana)

Mary: ndo maana tumekuja tujadili cha kufanya

Jeremy: (anatulia)

Mary: naomba utukaribishe baba

Jeremy: karibuni (kwa Vincent) shikamoo

Vincent: marahaba

(wanaketi)

Jeremy: mtatumia nini?

Vincent: mimi niko sawa

Colton: hata mimi nipo sawa

Mary: hata mimi nipo sawa tu

Jeremy: (anakaa pembeni ya Mary) ndio mama mkwe karibu

Mary: huyu ni baba yake Miriam

Jeremy: kumbe mlikuwa mnawasiliana?

Mary: hapana alimkumbuka tu mwanae akaenda kwa mama yang undo wakanitafuta mimi…

Jeremy: karibu baba mkwe…

Vincent: asante mkwe

Mary: cha kushangaza Colton ni mwanae

Jeremy: (anashangaa sana) kwa maana nyingine Colton ni kaka wa Miriam

Mary: ndio

Jeremy: (kwa Colton) yaani this is incredible and a perfect coincidence Miriam alihitaji muujiza na muujiza wenyewe ndo huu

Mary: nini kifanyike?

Jeremy: kwanza mimi nimshukuru Mungu kwa ukuu wake lakini pili iwe siri yetu tusiamini mtu Colton atakuwa kadi yetu ya thamani sana siku ya hukumu

Mary: kwanini siku ya hukumu

Jeremy: nadhani ni nzuri Zaidi… (kwa Colton) so nani alikuwa anakulipa?

Colton: Ariana

Jeremy: nilijua tu

Mary: ulijua? Ulijuaje?

Jeremy: Miriam amekuwa akisema mara kwa mara kuwa jioni ile ni Ariana ndo alimpigia simu…Miriam hawezi kudanganya…mdomo wake huongea ukweli tu

Vincent: unampenda sana mwanangu

Jeremy: nampenda sana Miriam baba mkwe yaani nampenda (anatabasamu kidogo) yeye ni malkia wangu…

Vincent: najisikia vizuri sana kusikia hivyo...

Jeremy: (kwa Colton) bado unawasiliana na Ariana?

Colton: huwa ananipigia ila mimi huwa sitaki kumpokelea...aliniumiza sana alitoa damu yangu alinikata niliumia sana

Jeremy: pole sana

Colton: kiukweli nahitaji mdogo wangu awe huru

Jeremy: sawa...utaishi hapa kuanzia sasa hivi nitakuficha hapa akuna atakayejua upo wapi

Colton: sawa shemeji

Jeremy: usijali…as long as unataka kumsaidia Miriam mimi nitakulinda

Colton: usisahau kuwa mimi ni kaka yake ingawa nimefanya kosa (anasikitika kidogo) Miriam has to forgive me

Jeremy: atakusamehe hana shida ila nataka kukuuliza Ariana alikupa sh. ngapi kufanya haya?

Vincent: (anainamisha kichwa)

Colton: sikupewa hata mia mbovu shemeji yaani hata sijui kwanini au nini kilinifanya nifanye haya…tena kibaya nimetenda kwa mdogo wangu

Jeremy: naona kabisa unajutia sana

Colton: kabisa shemeji nilianza kujutia baada ya kumsaidia Ariana lakini baada ya kujua kuwa Miriam ni mdogo wangu nimejuta mara mia shemeji

Vincent: nini hatima ya Colton kwenye hili

Jeremy: (anakaa kimya kidogo)

Mary: nini kitatokea kwa Colton baba

Jeremy: sijui maana sio mtaalamu wa sheria ila navyoona ataadhibiwa sawa kabisa na Ariana lakini yeye itakuwa kidogo na kama atakuwa na tabia nzuri itapunguzwa

Colton: kwa vyovyote shemeji mimi nipo tayari kwa adhabu yoyote nilifanya vile kwa sababu ya mapenzi mazito niliyokuwa nayo kwa Ariana (anasikitika) yalinipeleka pabaya

Jeremy: aisee

Vincent: mkwe tusaidie

 Jeremy: haina shida tutafanya juu chini hata kama ataenda jela hatakaa sana…tuna mwanasheria mzuri

Vincent: asante mkwe

Jeremy: tupo pamoja

Colton: Ariana ananipigia simu sana nimjibuje

Jeremy: akikupigia pokea akikuomba mkutane kutana nae

Colton: (anakaa kimya)

Jeremy: atajaribu kukuua nitakupa bullet proof hautadhulika

Colton: asante sana shemeji kwanza kwa kunisamehe

Jeremy: usijali tupo pamoja maadamu umekiri mimi nashukuru na kufurahi kwa ukiri wako

Colton: asante shem

Mary: (anatabasamu)

Vincent: tuungane kumsaidia mpendwa wetu

Mary: bila shaka

Jeremy: bila shaka baba mkwe

Vincent: (anatabasamu kidogo)

(wanaendelea na maongezi yao)

Post a Comment

0 Comments