ON MY WEDDING DAY 4


 

SCENE 4: -

(Patrick yuko ofisini kwake anafanya kazi zake za kila siku, wakati huo mlango wa ofisini kwake unagongwa)

Patrick: ingia mlango uko wazi

Mtu:(anaingia kisha anasimama mbele yake)

Patrick: karibu… (ananyanyua kichwa anatabasamu mara baada ya kumuona mgeni wake) wow…Edwin…

Edwin: nambie…

Patrick: rafiki yangu muda mrefu sana ulipotelea wapi my brother…

Edwin:mi nipo bwana… (anavuta kiti kisha anakaa)

Patrick: dah!!!sio siri nimefurahi kukuona Edwin…rafiki yangu wa miaka mingi jamani  

Edwin: hata mimi nimefurahi kukuona my friend…how is London...

Patrick: pako poa tu my friend…how is South Africa?                                                                                                                         

Edwin: pako very fine my friend yaani pako poa kuliko kawaida…         

Patrick: eti eeh…that’s very good…

Edwin:by the way nambie…my friend una jipya gani maishani mwako maana ulinipigia simu una hamu kweli ya kuniona

Patrick: kama ulivyosema tu kuwa nilikuwa na hamu ya kukuona

Edwin: kwanini

Patrick: nilikukumbuka na pia nilitaka kukuambia kuwa iam in love

Edwin: wow…really

Patrick: yes…I love her so much kiasi kwamba nataka awe mke wangu…nitamuoa huyu dada…just nasubiri atulie

Edwin: what do you mean atulie?

Patrick: ana majukumu mengi sana na akili yake haijawa tayari kuwa mke wa mtu maana anaona kama akiolewa atamuacha mama yake katika hali ambayo si nzuri

Edwin: kwanini usimsaidie afikie hayo malengo haraka ili sisi tule ubwabwa

Patrick:(anacheka) nipo kwenye hatua za mwanzo kumsaidia, nampenda na ninamthamini sana

Edwin:(anacheka kidogo) sijawahi kukuona ukimuongelea mwanamke jinsi unavyomuongelea huyu mwanamke

Patrick: she is so perfect for me yaani ni bonge la demu…mpole, mpenda watu, anayafanya majukumu yake kwa moyo, yaani kwa kifupi anafaa kuwa mke…

Edwin: nataka nimuone huyu dada, anaitwa nani?

Patrick: Olivia…

Edwin: ana jina zuri sana nimelipenda…mlikutana wapi?

Patrick: instagram…alini follow, akawa ana comment sana picha zangu mwisho wa siku tukaanza kuchat…sikujua kuwa anaishi Mwanza so nilipotoka London nikamwambia kuwa tukutane Mwanza akasema huku ndiko anapoishi, nilifurahi kumuona kwa mara ya kwanza, she is so beautiful

Edwin: naomba nimuone kama una picha yake hapo

Patrick: nakosaje picha yake kwa mfano (anachukua simu yake kisha anamuonyesha rafiki yake) huyu ndo malkia wangu…kipenzi cha nafsi yangu

Edwin:(anaiangalia ile picha kisha anang’ata midomo na kulamba midomo yake kama mtu aliyetamani kitu anachokiona) oh…My God, she is so beautiful…naomba nimuone kwa macho kabisa

Patrick:(anacheka kidogo) kwani hapa humuoni kwa macho…

Edwin: No..No…yaani nataka nimuone live bila chenga

Patrick: usijali my friend…Jumamosi huwa napenda kwenda nae migahawani ili tukae pamoja sasa siku ya jumamosi ndo utamuona shemeji yako

Edwin: Jumamosi mbona mbali sana

Patrick :( anamtania) mbona una hamu ya kumuona mke wangu umemtamani nini?

Edwin: hapana…kwanini useme hivyo? Nataka tu kumuona kwanini ameuchukua moyo wako hivyo?

Patrick: nakutania…(anacheka)najua huwezi kunichukulia mwanamke nimpendae kwa dhati…wewe ni kama kaka yangu wa damu

Edwin: uko sawa kabisa Patrick…siwezi kumtamani na wala kumuangalia mwanamke uliyemchagua maana wewe ni kama mdogo wangu wa damu…na pia umeshanisaidia vitu vingi sana my dear

Patrick: that’s right my brother cha kufanya tu ni kuombeana ili mimi na Olivia wangu tufunge ndoa

Edwin:(anajichekesha sana) haina shida my brother

Patrick: by the way umefika tu nikaanza stori zangu za mwanamke wangu mpya…

Edwin: No, it is ok najua ulifurahi sana…maaana navyojua wewe mdogo wangu hujawahi kabisa kupenda mtu hivi…mara nyingi ulikuwa unachezea tu wadada wa watu

Patrick: tulikuwa tunachezea wote…hukumbuki hata wewe ulikuwa na hizo…au mpaka leo bado una katabia ka wanawake…niambie ukweli maana sijakaa na wewe siku nyingi mimi baada ya msiba wa wazazi wangu nikaenda London na wewe ukaenda South Africa basi hata hatukuonana tena…

Edwin: yes, my brother hatukuonana tena na nilikua na kukumbuka sana makeke yako na jinsi ulivyokuwa unatumia pesa kupata wanawake, najua na huyu umetumia pesa nyingi sana

Patrick: huyu yeye imekuwa tofauti…nilipokuwa London nilikuwa simtumiii pesa na wala hakujua kama naweza kuwa nina pesa nyingi kiasi hiki…kwahiyo alinikubali tu…hivyohivyo na hata mar azote nilipokwa nakuja na kumsalimia sikuwahi kumuonyesha kuwa nina pesa so alinikubali hivyo hivyo…kwahiyo nilipoona hivyo nikaamua kumweka maanani…so she is wife material

Edwin: hongera sana kwa mwanamke mpya mpya my brother, mwenzio sijapata hata mpenzi

Patrick: don’t give up my brother, Mungu ni mwema siku zote atakupa tu

Edwin:ni matumaini yangu pia

Patrick: ok…what would you like…soda, beer au wine?

Edwin: unajua napenda shampeni

Patrick: ok… (anachukua simu yake ya mezani kisha anampigia sekretari wake) nambie Mary…naomba utuletee waini ofisini

Sekretari: sawa boss

Patrick: enhe!!!nambie…mbona umepoa huna yake makeke yako my brother…

Edwin: maisha magumu sana my brother, sina mpenzi

Patrick: ah!!hiyo isikupe tabu mbona wanaake ni wengi sana

Sekretari:(anakuja na wine pamoja na glasi za wine mbili kisha anaziweka mezani kisha anawakaribisha halafu anaondoka)

Patrick: unaweza ukamchukua hata huyu yuko vizuri sana

Edwin: nataka kama wako

Patrick: yupo rafiki yake yaani wapo kama mapacha… (anamimina waini kwenye glasi kisha anampa Edwin)

Edwin:(anapokea) waambie jumamosi waje wote

Patrick: hiyo itakuwa sawa kabisa…ngoja nitamwambia…aje nae Jumamosi

Edwin:(ananyanyua glasi) cheers…

Patrick: cheers…

(wanagonga glasi zao huku wanaonekana wana furaha sana)

Patrick: oh… (anaangalia simu yake) simu inaita, na ni shemeji yako(anapokea)hello baby…

Olivia: nambie honey…I miss you so much…

Patrick: I miss you too…my queen

Olivia:(anacheka)

Patrick: nambie mbona huongei unacheka tu mama

Olivia: uko wapi?

Patrick: ofisini my dear…nafanya kazi

Olivia: ok…mi nipo nyumbani na mama

Patrick: mnafanya nini?

Olivia: tunaangalia runinga…flat screen…mpya na upya wake

Patrick: wow (anacheka kidogo) …na je tayari mafundi wameshajenga choo cha ndani?

Olivia: ndio mume wangu

Patrick: afadhali maana dah!!nilikuwa Napata tu wivu kila nikifikiria kuwa huwa unaenda kuoga nje na khanga moja dah

Olivia:(anacheka tena) yaani wewe una matatizo sana

Patrick: huwa nina wivu sana yaani hiyo ndo kasoro yangu

Olivia: nakuahidi sitakupa sababu ya kuwa na wivu my love

Patrick: asante sana…my love

Olivia: asante darling na pia mafundi wamekuja kuweka uzio ndo wanamalizia, walianza jana leo wanamalizia

Patrick: asante mama…you are the queen; I have always wanted to keep in my palace yaani wewe ni malkia niliyekuwa namtaka katika himaya yangu

Olivia: I promise to never let you down my King

Patrick: I love you

Olivia: I love you too king

Patrick :( anakata simu kisha anatabasamu)

Edwin: kweli hapo nimekubali kwamba kweli unampenda huyu dada…yaani mpaka nyumba yao umeona uanze kuikarabati…kweli ni kipenzi cha nafsi yako, umekamatika kijana (anacheka)

Patrick: (anacheka) haswaaaa—binti amenikamata lakini nimefanya hivyo maana nataka nimuoe

Edwin: cheers to that…

Patrick: cheers

(Wanaendelea kunywa vinywaji vyao huku wanaendelea na mazungumzo ya hapa na pale)

Edwin: Patrick unataka kuoa?

Patrick: exactly…nimempata the right person kwanini nivunge? Naoa mwenzenu yaani naoa kabisaaaa kama nimepata niliyemtaka kwanini nichelewe?

Edwin:si ndo hapo? ila lazima niseme kila shetani na mbuyu wake na wewe mbuyu wako ni huyu demu…Duh mpaka ume surrender kabisa? huyu dada kakupa nini?

Patrick: yaani, sijui kanipa nini jamani …sijui kaniroga(anacheka)

Edwin: itakuwa, Patrick huyuhuyu wa kuchezea watoto wa watu leo umependa baba…noma sana na ulikuwa unabadilisha mademu wewe (anacheka)

Patrick: watu hubadilika bro we huamini hilo?

Edwin: naamini na nakupongeza sana

Patrick: cheers to that

edwin: cheers

(wanagonga glasi huku wanaendelea na mazungumzo yao)


Post a Comment

0 Comments