ON MY WEDDING DAY 5


 

SCENE 5: -

(Olivia amekaa sebuleni kwao na rafiki yake kipenzi aitwae Monica, wanapata vinywaji baridi huku wakibadilishana mawazo mawili matatu.)

Monica :( anaguna) shoga danga ulilolipata shoga usiliache…

Olivia: sio danga huyo shoga yangu ni mwanaume ninaempenda kwa dhati na ninatamani sana anioe

Monica:(anakunywa kinywaji kidogo) aisee maana kapabadilisha kwenu ndani ya siku kadhaa tu kila kitu kipo sawa ona jamani hadi raha

Olivia: ndo hivyo shoga yangu mwanaume wa hivyo unaanzaje kumuita danga?

Monica: kwakweli

Olivia:(kimya kidogo huku anakunywa soda yake taratibu)

Monica:(anaonyeshea runinga kubwa iliyokuwepo sebuleni hapo) na hiyo TV kakununulia yeye

Olivia: ndio hata haya masofa yeye ndo aliniletea na bado mama anatakiwa kwenda kutibiwa Nairobi mwezi ujao

Monica: wewe huyo mwanamume mbona bonge la kitu shoga yangu mi mbona sipati wa hivyo?

Olivia:(anacheka) jamani…utapata tu wakati wako bado haujafika

Monica: huyo mumeo ni mtu mzima?

Olivia: sio sana ana miaka 35

Monica: ametoa wapi mali zote hizo? mbona bado mdogo sana?

Olivia:(anacheka)

Monica: asije akawa jinni…maana si uliniambia mlikutana instagram

Olivia: ndo hivyo shoga yangu

Monica: mwenzangu jinni hilo…

Olivia: hamna bwana (anacheka) yaani anasali sana

Monica: ana vituo vya mafuta…sijui vingapi

Olivia: vitatu…tu jamani

Monica: sasa vichache hivyo…sijui na mabasi mangapi

Olivia: matano…

Monica:(anaguna) embu nimuone si una picha zake…

Olivia: nyingi sana

Monica: nionyeshe…

Olivia:(anachukua simu yake aina ya iphone kisha anamuonyesha picha ya Patrick)

Monica: shoga…mbona mwanaume mtamu hivi…mzuri hivi…yaani umepata mwanamume ana kila kitu…halafu mrefu huyu yuko vizuri sana kwenye mambo yetu yaleeee

Olivia: umeanza(anacheka)yaani huwezagi kuacha kuongea ujinga rafiki yangu

Monica: halafu kakununulia simu nyingine mpya na upya wake… (anampa glasi) embu niongezee kinywaji nijinywee hapa

Olivia:(anaipokea glasi, anasimama kisha anaelekea jikoni)

Monica:(anajisemea moyoni) mwanaume ana kila kitu huyu, cheki alivyo mzuri

Olivia:(anarudi na kinywaji anampa kisha yeye anachukua cha kwake kisha anaendelea kunywa taratibu)

Monica: halafu si huwa anaenda London sana…?

Olivia: ndio…kuna biashara aliachiwa na wazazi wake ndo huwa anakuwa anaifanya

Monica: biashara gani

Olivia: siwezi kukuambia sasa hivi…

Monica: niambie bwana au madawa ya kulevya…?

Olivia: hamna…sio madawa ya kulevya…dhahabu…

Monica: dah…huyu mwanaume ni noma sana

(mama anakuja wakati huo wapo bado wapo kwenye maongezi)

Olivia: shikamoo mama

Mama: marahaba mama…

Monica: shikamoo mama

Mama: marahaba mwanangu… (kwa Olivia) mwenzio nanakutafuta sana mbona hupatikani

Olivia: Patrick ana vituko mimi mbona simu yangu ipo hewani

Monica: labda mtandao…

Mama: chukua simu yangu umpigie… (anampa kisha anaondoka) ukimaliza niletee ndani (anaingia ndani)

Monica: bonge la simu la mama

Olivia: kaletewa na mkwe wake (anapiga simu ya Patrick inaita mwisho inapokelewa) honey…

Patrick: mambo…

Olivia:(anatabasamu kidogo) poa…

Patrick: hupatikani

Olivia: nisamehe baby

Patrick:it is okay…sasa Jumamosi…naomba uje na rafiki yako maana na mimi nakuja na rafiki yangu…yaani anatafuta mchumba yaani pamoja na pesa zake hajapata mwanamke anasema kuwa Mungu amenijalia mwanamke mzuri hivyo nay eye anataka mwanmke mzuri kama wewe na mwenye akili ya maisha nikamwambia kuwa na wewe una rafiki yako mnafanana kama mapacha so akasema kuwa anataka kumuona hivyo njoo nae sawa ee

Olivia:(kwa Monica) Mungu kakusikia…jumamosi tutaenda kukutana na rafiki yake Patrick na yeye anatafuta mchumba kama wewe

Patrick:(anacheka) kumbe yupo hapo eeh

Olivia: yeah…

Monica:(anacheka)

Patrick: basi poa tutawakutanisha jumamosi

Olivia: wazo zuri…sana

Patrick: enhe mambo mengine?

Olivia: nimekumisi bae…

Patrick: ofisini unapajua…nyumbani unapajua…pale kwenye kitimoto unapajua unashindwa kuja?

Olivia: njoo wewe…

Patrick: duh…mama yupo hapo mi naona aibu bwana

Monica :( anamuangalia Olivia)

Olivia:(anacheka) we njoo kwanza yeye siku hizi anashinda ndani anaangalia tamthilia zake za kihindi zilizotafsiriwa

Patrick: sawasawa ana Amani sasa hivi ee

Olivia: saaaana…asante baby

Patrick: usijali, you are my wife lazima nikuangalie wewe na uwapendao…

Olivia: I love you Patrick

Patrick: I love you my queen

Olivia: baadae...

Patrick: baadae (anakata simu)

Olivia:(anashusha simu na kuiweka mezani)

Monica: mnapendana kweli…hadi raha

Olivia:(anacheka)

Monica: mna muda gani now…

Olivia: mwaka tayari…maana tumeanza kuchati muda mrefu sana…baadae tukaja kuonana halafu akarudi London...amekaa kule muda mrefu juzijuzi ndo amerudi

Monica: anarudi lini London

Olivia: bado sana

Monica: haya…bwana una bahati mara nyingi watu wakikutana mitandaoni wanachezewa kisha wanaachwa solemba ila kwako jamaa anaonekana kapagawa kabisaaaa

Olivia:(anacheka) yote ni mipango ya Mungu...si unakumbuka nilivyohangaika na mahusiano

Monica: nakumbuka vizuri sana…

Olivia: kwahiyo Mungu yupo na anatenda

Monica:(anaguna) kwako tu…

Olivia: usikate tamaa rafiki yangu, twende hiyo jumamosi tuone Mungu kakuwekea nini…maana Patrick anasema hata huyo rafiki yake anatafuta mwanamke muda mrefu ila hajapata…twende shoga yangu

Monica: ndo uniazime nguo

Olivia(anacheka)usijali shoga yangu

Monica:(anacheka) twende mwaya nikamuone shem kwa macho

Olivia: poa…cheers…to our men

Monica :( ananyanyua glasi) cheers... (Anagonga glasi)

(Wanacheka huku wanaendelea kunywa vinywaji vyao)

Olivia: twende tukapike jikoni

Monica: poa

(Wananyanyuka wanaelekea jikoni ili wapike wanapofika huku wanaanza kupika huku wanaonekana kufurahiana, wanapika huku wanakunywa vinywaji na mazungumzo pamoja na vicheko vinaendelea)

Monica: naona shoga yangu hata mama yako anasikia raha si kwa kubadilika huku…loh

Olivia: acha tu shosti…nampenda na kumheshimu Patrick kanitoa mbali huyu kaka (anaguna)

Monica: tena mbali sio kitoto (anacheka kimbea) si na mimi litokee danga linibadilishe maisha?

Olivia: Mungu ni mwema sana rafiki yangu, atatokea tu wala hata usijali

Monica: eti ee

Olivia: nyumba ilikuwa imeparama nyiee—Mungu huyu achene aitwe Mungu

Monica: nakumbuka shoga yangu sasa hivi imekuwa tamu hiyo…(anaguna)

Olivia: ndo hivyo kila jambo na wakati wake…kuna wakati wa kuvuna na kupanda…

Monica: mwenzangu huu kwako ni wakati wa kuvuna, sijui shoga ulipanda lini ila unavuna ona nyumba ilivyo tamu

Olivia: acha tu

(wanacheka huku wanagonga mikoo)

Monica: shoga mwanaume umepata…tena mwenye roho yake(anaguna)

Olivia: namshukuru Mungu sana jamani


Post a Comment

0 Comments