ON MY WEDDING DAY 3


 

SCENE 3: -

(ni asubuhi nyingine nzuri na njema, ndege wa angani wanaruka ruka wakimsifu Mungu na uumbaji wake, Patrick yupo bustanini kwake amekaa ametulia, anakunywa chai huku anafuatilia habari mbalimbali kupitia simu yake ya mkononi, wakati anaendelea kupitia mawili matatu anapata wazo la kumpigia mpenzi wake simu)

Patrick: ngoja nimpigie baby simu kwanza nimemkumbuka tangu jana mchana tulipoachana nae sijamuona tena (anaweka simu yake sikioni inaita mwisho inapokelewa) my Queen

Olivia: yes, my king, bado umelala?

Patrick :( anacheka kidogo) huwezi amini nilitaka kukuuliza hivyo pia umefanya kuniwahi, sijalala nipo bustanini nakula upepo mwanana huku ninakunywa chai vipi wewe umelala?

Olivia: hapana nipo tu, nimetoka kuoga

Patrick: njoo nyumbani kuna vitu nataka tuzungumze…

Olivia: sawa…nakuja

Patrick: nikupe dakika ngapi? au nimwambie dereva wangu aje akuchukue?

Olivia:  hata hivyo ni sawa pia

Patrick: tukupe muda gani utakuwa umemaliza kujiandaa?

Olivia: dakika kumi na tano

Patrick: utakuwa umemaliza kujiremba kweli?

Olivia: kabisa

Patrick: basi sawa, ngoja nimwambie aje akuchukue

Olivia: poa (anakata simu)

Patrick :( anamuita dereva wake) Edrick...

Edrick :( anakuja mbio mbio) naam boss

Patrick: nakupa namba ya mtu hapa, umpigie akueleze yuko maeneo gani umchukue umlete nyumbani hapa, ni shemeji yako(anacheka)halafu nishakwambia usiwe unaniita boss jamani

Edrick: samahani boss

Patrick: umeniita tena boss…

Edrick: samahani Patrick

Patrick: hapo sawa, ngoja nikutajie namba ya shemeji yako utampigia... (Anamtajia)

Edrick :( anaichukua kisha anaihifadhi) sawa mdogo wangu ngoja nikamchukue shemeji yangu

Patrick :( anacheka Sana) poa kaka yangu

Edrick :( anaondoka nae huku anacheka)

BAADA YA DAKIKA ISHIRINI

(Edrick anarudi akiwa na Olivia, wanapofika wanaegesha gari kisha Olivia kwa madaha anashuka kwenye gari la kifahari la bwana Patrick Kalenzi ambae ni mpenzi wake)

Patrick :( anamuona) wow…Queen Kumbe ni Zaidi ya mzungu ee

Olivia :( huku anamuendea) kwanini?

Patrick: umeniambia dakika kumi na tano kweli zikawa hivyo

Olivia: hapana baby, zimezidi kama dakika tano (anafika alipo Patrick)

Patrick: sio mbaya (anambusu mdomoni kisha anamkumbatia) karibu nilikuwa nimekukumbuka kweli Jana tulipomaliza shopping nikakuacha nyumbani sikukuona tena Jana hata dinner ulikataa kula na mimi

Olivia: nilikuwa na mama si unajua mama anaumwa sana so inabidi mara nyingi nikae nae

Patrick: anyways sawa hiyo haina shida, karibu ukae mi nilikuwa nakunywa chai

Olivia :( anatabasamu kisha anakaa karibu kabisa na alipokaa Patrick) nambie

Patrick: karibu tunywe chai…nenda jikoni waambie wakupe unachotaka then tuje tukae hapa mi huwa napenda sana kukaa hapa patulivu sana

Olivia: napaona ni pazuri sana...ila mwenzio nishakunywa chai

Patrick: poa basi hata juisi au hata maziwa basi fanya hivyo, ili nafsi yangu itulie jamani sweetheart

Olivia: sawa usije ukalia…(anacheka)

Patrick :( anacheka)

Olivia :( anaenda jikoni na baada ya muda anarudi akiwa amebeba juisi ya embe) sasa naona utafurahi

Patrick; hapo sawa, kwanza sisi hapa mgeni akija natakiwa awe mwenyeji wakati huohuo, umewakuta kina dada Halima?

Olivia: wapo...

Patrick: yaani hapa ni kujichotea tu hakuna mtu wa kukuuliza

Olivia: wow…mnaishi vizuri sana,

Patrick:ni jambo zuri sana kuishi hivyo maana unaweza kusema kuwa unamtesa mwanadamu mwenzio na je siku akiamua kukupokonya kila kitu alichokupa? anapokonya wewe anampa huyo uliyekuwa unamuona hafai utafanyaje? ni muhimu sana baby kuwa na roho ya Wema ili hata siku huna watu watakukumbuka kwa ule wema ingawa si kwa asilimia kubwa ila tu watakukumbuka na hata Mungu atakuhurumia, jifunze kukaa na mtu na kumchukulia na ukipata nafasi ya kumsaidia msaidie…hiyo nayo ni zaidi ya sadaka.

Olivia: nakupenda Patrick, we ni mtu wa pekee sana.

Patrick: usije tu kunisaliti, nitajiua, nauogopa usaliti sana na Zaidi nauchukia usaliti, kama umeamua kunipenda wewe nipende na kama umeamua kunipotezea muda nambie na  nionyeshe mapema ili nijitoe mapema kabisa…

Olivia: usijali mpenzi wangu sitawahi kuja kukusaliti

Patrick: na ukifanya hivyo?

Olivia: siwezi hata kufikiria nakupenda sana na kama nikifanya hivyo basi niache

Patrick: haya ni vyema ulivyojichagulia adhabu ila hiyo kama utanisaliti ndo nakuacha lakini kama hujanisaliti…nitakupenda na kukutunza milele

Olivia: nakupenda

Patrick: nakupenda Zaidi

Olivia :( anamlalia begani)

Patrick: tupendane mpenzi wangu

Olivia: Mungu atusaidie

Patrick: atatusaidia unadhani anakawia kuwasaidia watu wake? (anabadilisha mada) baby…mimi kuna vitu nataka nikufanyie mimi kama mpenzi wako,

Olivia: vitu gani?

Patrick: kwanza kabisa kuifanyia matengenezo nyumba yenu lakini cha pili nikufungulie biashara au nikusomeshe chagua kimoja kati ya masomo au biashara

Olivia; baby, uko serious unataka kunifanyia hayo?

Patrick:na Zaidi mpenzi wangu, mimi nimekupenda sana maana kwanza unaonekana una akili sana, unapambana kwa ajili ya mama yako kweli wewe ni mwanamke unaefaa sana kuitwa mke

Olivia:(anacheka) asante my love ni lazima nipambane kwa ajili ya mama yangu, kwake yeye ni mimi t undo ndugu yake hana mume, kaka wala dada kwahiyo inabidi nipambane tu

Patrick: hicho ndio kilichonifurahisha kwako wewe ni jembe, sasa mimi nataka nikusukume uzikaribie ndoto zako

Olivia: nitashukuru Sana mume wangu

Patrick: I love you

Olivia :( anambusu mdomoni)

Patrick: kazi utakayo nifanyia ni kuandika kwenye karatasi wapi panahitaji matengenezo na gharama zake na pia utanipa jibu kuwa umechagua nini kati ya masomo au biashara na gharama ya kitu ulichochagua sawa ee

Olivia: sawa

Patrick: nivipate mapema ili nipange bajeti zangu

Olivia: ok baby Leo nitaenda kujadiliana na mama tuone tutahitaji kiasi gani

Patrick: sawa malkia wangu…

Olivia :( anatabasamu huku anamuangalia mpenzi wake usoni)

Patrick: mbona unaniangalia Sana unataka kunikariri au?

Olivia: hapana naangalia tu ukuu wa Mungu, nimeteseka sana na maisha ila ghafla tu ukatokea wewe,

Patrick: njia za Mungu hazichunguziki yeye akipanga amepanga na hakuna mtu hata mmoja ambae anaweza kupangua hata iweje

Olivia: namwamini sana Mungu wangu, Mungu aliyewavusha waisraeli kwenye bahari ya shamu, namtukuza kwa mambo yake makuu

Patrick: hata mimi namuamini sana Mungu, Mungu aliyemlinda Daniel kwenye shimo lililokuwa na simba wakali, namuamini Mungu wa Ibrahim, Isaka na Jacobo

Olivia: wow…unaijua biblia baby

Patrick: mimi mlokole

Olivia: kweli?

Patrick: sana

Olivia: nitakuwa nakupitia kila Jumapili ili twende kanisani

Patrick: sawa…nitakuwa nafurahi sana

Olivia: kweli

Patrick: Sana

Olivia: mama atafurahi sana

Patrick: anapenda walokole ee

Olivia: yeye mwenyewe mlokole

 (Mazungumzo Yao yanaendelea kwa muda huku kila mmoja wao anaufurahia uwepo wa mwenzie)

Patrick: kwahiyo Andika nilivyokuomba tuone naanzia wapi

Olivia: sawa la azizi

Patrick: na jibu kwamba unataka kufanya nini kati ya masomo au biashara au tunaweza kufanya vyote wewe unatakaje?

Olivia: yaani napagawa mwenzio ila nitakuambia

Patrick: usipagawe ndo kwanza tunaanza tulia mtoto upendwe vizuri

Olivia: Mungu huyu (anaguna)

Patrick: unatakiwa kujua mumeo nina roho ya kitajiri kwahiyo utaenjoi

Olivia: hata mimi nimeona

Patrick: basis awa (anacheka)

Olivia: nakupenda patrick

Patrick: nakupenda pia


Post a Comment

0 Comments