ON MY WEDDING DAY 1

 


SCENE 1: -

(Majira ya saa moja usiku,hali ikiwa imepoa na hali ya hewa kwa ujumla ni nzuri na kaupepeo Fulani mwanana kanavuma kwa mbali,uwanja wa ndege jijini mwanza msichana mrembo sana aitwae Olivia amesimama huku anaonekana kuna mtu anamsubiri na pia anaonekana kuwa ana shauku kubwa sana ya kumuona mtu huyo,baada ya muda hatimae mgeni wa msichana Olivia anawasili na anaonekana kuwa ametoka nchi ya nje,mara baada ya kufika Olivia anamuona na kwa furaha anakimbia kumlaki mtu huyu ambae kwa haraka anaonekana ni mwanaume wake yaani mpenzi wake maana anamkumbatia na kumbusu)

Olivia :( huku anamkimbilia) Patrick my love

Patrick: hello baby… (Anamkumbatia na kumbusu)

Olivia :( anambusu pia) hi darling karibu tena kwetu…

Patrick: asante…ila hata mimi hapa ni kwetu sema tu sababu ya masomo na biashara zangu najikuta nakaa sana nje…ila sijasahau kuwa mimi ni mtanzania huoni hata lugha naijua (Anacheka kidogo)

Olivia: haswa mpenzi…naona kabisa kuwa unaikumbuka kabisa lugha yetu

Patrick: Oh! I missed you so very much baby...Nikikuambia uje England huji unajivuta kweli sijui kwanini

Olivia: bado visa yangu haijatoka ila ikitoka nitakuwa naenda na wewe

Patrick :( anacheka) asante…ok yaani nimechoka kweli nahitaji kwenda kupumzika...Nilikuambia kuwa nikija tena nitakuonyesha nyumba yangu nahisi Leo ndo siku nzuri na muafaka wa mimi na wewe kwenda kuiona nyumba yangu

Olivia: si umesema kuwa umechoka? kwanini usiende kupumzika tu

Patrick: wewe umekuja kunipokea airport Ili unipeleke wapi

Olivia: ok sweetheart…umeshinda sina la kuzungumza…umeshinda

Patrick :( anacheka sana) ok dear twende…zetu

( Pamoja wanaondoka uwanjani hapo nje ya uwanja huo yupo dereva wa kijana Patrick aliyekuwa anamsubiri boss wake muda mrefu,taratibu wakiwa wameshikana mikono Patrick na Olivia wanaliendea gari lile,kisha wanapanda na bila kupoteza muda wanaondoka kuelekea nyumbani kwa Patrick…baada ya mwendo wa kama nusu saa wanafika katika jumba safi na la kifahari,nyumba inapendeza na inaonekana ni ya gharama kubwa sana,geti safi,kuna walinzi na wamama wawili ambao wanaonekana ndo wamepewa jukumu la kuiangalia nyumba hiyo,Patrick anashuka kwenye gari kisha anamfungulia mlango Olivia ambae pia anashuka kwenye gari hilo huku anashangaa sana mazingira hayo yanayovutia kuliko)

Patrick: karibu sana my love, hapa ni nyumbani kwangu, (anawaonyeshea wavulana waliokuwa wamesimama karibu na geti) wale ni walinzi wa nyumba yangu ni kama ndugu zangu pia

Olivia: oh!!!Nice to meet them (anatabasamu)

Patrick:na wale (anaonyeshea wanawake wawili wa makamo) hawa ni mama ambao nimewaweka waangalie nyumba yangu kipindi tu napokuwa sipo nyumbani nipo labda London au Dubai kwa ajili ya biashara zangu

Olivia: oh…jamani nashukuru kuwafahamu (anatabasamu)

Patrick :( anawaita wafanya kazi wake wote) tafadhali njooni…

Wafanyakazi :( wanamuendea)

Patrick :( Kwa heshima anamsalimia mmoja wa wamama) shikamoo dada Agnes…

Agnes: marahaba baba habari za London?

Patrick: nzuri sana (kwa mama mwingine) da. Halima...Shikamoo

Halima: marahaba mdogo wangu habari za London?

Patrick: nzuri tu…

Agnes: naona umekuja na mwali

Patrick :( anacheka) anaitwa Olivia ni mpenzi wangu tulikutana katika mitandao ya kijamii…Instagram (anacheka)

Halima: sawa…ni muda gani sasa?

Patrick :( anacheka) ni muda kidogo mama yake anajua na mara nyingi huwa nikija naenda moja kwa moja kwao kwanza halafu ndo nakuja nyumbani…kwahiyo ni muda sasa tangu tuwe wapenzi nampenda na nina malengo nae

Agnes: siku hizi utandawazi sisi zamani tulikuwa tunakutana na wapenzi wetu kwenye chagulaga huko au unaletea mchumba nyumbani lakini siku hizi mambo yamekuwa tofauti watoto wengi wanakutana mitandaoni

Halima: nakwambia kazi kweli kweli jamani…

Agnes :( Kwa Olivia) karibu wifi

Olivia :( Kwa heshima huku anapiga magoti) shikamooni mawifi zangu

Kwa pamoja: marahaba hujambo

Olivia: sijambo

Patrick: ok... dear, hawa ni kama dada zangu sio kama ni dada zangu (anacheka kidogo) …wameniangalia muda wote wa maisha yangu yaani tangu baba na mama bado wapo hai wenyewe wamekuwa ndo dada zangu mimi kwetu nipo peke yangu...Kama wewe tu (kwa Agnes) yupo peke yake huyu (anatabasamu)

Agnes: jamani kweli?

Patrick: ndo hivyo sister… (Kwa Olivia) kwahiyo ndo hivyo mpenzi nadhani nilikuambia kuwa baba na mama yangu walikufa kwa ajali ya ndege walikuwa wanatoka Dubai, kwahiyo sina baba wala mama wala kaka ila nina dada zangu wawili hawa hapa

Olivia: oh, nashukuru na ninafurahi sana kuwafahamu…mimi naitwa Olivia kama baby alivyokwisha nitambulisha nina umri wa miaka 27, ninaishi nyegezi, ninaishi na mama yangu sina baba

Halima: pole Sana Kwa kupoteza mzazi mmoja ila yote ni kumshukuru sana Mungu maana wanasema kazi yake haina makosa yeye akipanga amepanga kikubwa tu ni kuwaombea wapumzike kwa Amani

Olivia: amina wifi…

Agnes: karibuni ndani naona Patrick amaeamua kufanya utambulisho nje

Patrick :( anacheka) kumbe nimefanya kosa eeh

Halima: Sana...Tena Kama mchumba ilibidi aingie ndani kwanza tumpe maji au juisi au wine ndo tuanze utambulisho

Patrick: basi nisameheni au nichapeni bakora (anacheka)

Agnes: umeshasamehewa

(wanacheka kisha wanaingia ndani ambako ndo ufahari wote ulipo, sofa safi meza kubwa ya kioo, runinga yenye kioo kikubwa ukutani, ukienda sehemu ya kulia sasa ndo utakubali, maana pana samani nzuri na za thamani, Olivia anapashangaa sana, dada Agnes na dada Halima wanatenga vinywaji, na wanapomaliza kutenga, wanaketi na wenyewe na taratibu wanakunywa vinywaji vyao)

Patrick :( Kwa Olivia) feel at home darling…

Olivia :( hata hasikii maana akili yake imeshageukia kwenye vitu vya kifahari anavyoviona sebuleni)

Patrick: baby…

Olivia :( anakuwa Kama ameshtuliwa usingizini) yes…baby

Patrick :( anacheka) feel at home…

Olivia: thank you baby…

(Kwa pamoja wanaangua kicheko, huku wanaendelea kunywa vinywaji vyao taratibu)

Halima :( huku ananyanyuka) ngoja nikaangalie dinner Kama iko tayari

Olivia :( anaangalia simu yake) ah…mi naona niwaache usiku umeingia na sijamuaga mama

Patrick :( anatoa simu yake matata aina ya iphone) ngoja nikuagie Kwa mama yako ingawa hautalala huku ila utachelewa kidogo (anapiga simu inaita mwisho inapokelewa) hello mama…shikamoo

Mama: marahaba baba hujambo?

Patrick: sijambo…Patrick anaongea hapa

Mama: najua baba upo hapa nchini?

Patrick: ndio mama, ndo nimekuja Leo, ndo nimefika mama yangu

Mama: sawa baba karibu

Patrick: Asante mama…samahani mama

Mama: bila samahani baba

Patrick: nipo na Olivia na tutapata nae chakula cha usiku kwahiyo atachelewa kidogo…mama yangu

Mama: ondoa shaka mwanangu kuwa huru baba ni mwenzio huyo mwanangu kuwa nae huru tu

Patrick: Asante mama…nitamleta baadae

Mama: sawa baba

Patrick :( anakata simu) kesi imeisha au sio...lets enjoy baby

Olivia: sawa (anacheka tena)


Post a Comment

0 Comments