SCENE
2: -
(Asubuhi
nyingine, siku moja baada ya kijana Patrick kutoka London, Olivia amelala kwao,
wakati simu yake inaita sana na kwa kuwa yupo usingizini hasikii, mama yake
anaingia chumbani humu anaona simu yake inaita anamuamsha)
Mama:
Olivia… (Anampiga piga)
Olivia:(huku
anavuta shuka) mama niache bwana, we si unajua jana mimi nilichelewa kurudi
nyumbani (sauti ya kama mtu aliyelemewa na usingizi sana)
Mama:
mwenzio anakupigia simu
Olivia:(anakurupuka)
mama yangu (anachukua simu yake mara moja) duh...Missed calls 14
duh!!!huku kulala kulala gani mbona nimezidi(anampigia)
(Simu
inaita mwisho inapokelewa)
Mama :( anaondoka)
Patrick:
dah…wewe unalala utasema umekufa nimeamkia hapa kwenu Leo nimesimama hapa mpaka
nimekoma
Olivia:
pole dear…yaani usingizi huwa unanichukulia muda kweli
Patrick:
eeh jamani embu badilika huko kulala kama umekufa kumenichanganya mwenzio
nikajua umedanja (anacheka) nipo hapa nje
Olivia
:( anacheka) karibu ndani dear, sasa mbona umesimama nje?
Patrick:
nilijua nitakupata mapema nilitaka twende rock city mall tukafanye shopping au
umebanana leo
Olivia:
no, niko free
Patrick:
twende sasa
Olivia
:( anacheka tena) hata sijaoga…ngoja nioge kwanza
Patrick:
hapo sasa utanichelewesha unajua...
Olivia :(
anashuka kitandani) ngoja nije maana kuingia ndani umekataa
Patrick
:( anacheka) mi naona ndani nitachelewa Sana we Fanya twende
Olivia :(
anafika nje) njoo bwana
Patrick
:( bado simu ipo sikioni) nitachelewa
Olivia:
dakika mbili nyingi
Patrick
:( anaingia nae ndani)
Olivia:
hivi umegundua?
Patrick:
nini?
Olivia:
bado tunaongea na simu
Patrick
:( anacheka) sijagundua Hilo…we umetoka mtupu ndo nilikuwa nakushangaa
Olivia :(
anacheka Sana) nimetoka uchi??? Ila Patrick we chizi (anacheka sana)
Patrick:
ndo hivyo…mama yuko wapi?
Olivia:
atakuwa ndani
Patrick:
eti eeh
Olivia:
nimuite aje akupe kampani?
Patrick:
usimsumbue we kaoge bwana
Olivia:
je ungependa chai?
Patrick:
sasa hivi saa tatu yote hii
Olivia:
sasa je?
Patrick:
hapana nimeshakunywa
Olivia:
poa (anamuwashia runinga ndogo iliyokuwepo hapo sebuleni) enjoy feel at
home
Patrick:
thank you honey
Olivia:
poa (anaenda nje kwenda kuogea nje)
Patrick:
mbona unaenda kuogea nje ndani hakuna bafu?
Olivia:
hakuna bafu
Patrick:
hii Ni nyumba yenu au mmepanga?
Olivia:
yetu…
Patrick:
duh…sasa na khanga moja mke wangu hao majirani si huwa wanafaidi?
Olivia:
umeanza wivu
Patrick:
Mimi nina wivu mpaka huwa najiogopa
Olivia :(
anacheka) mi naenda kuoga bwana hatutamaliza na haya masihala yako
Patrick:
fanya haraka nikakufanyie shopping my wife
Olivia:
poa
Patrick:
pia ulizia Kama tunaweza kupata nafasi tukaweka choo cha ndani…maana sio kwa
kuwafaidisha midume huko nje
Olivia:
ipo sehemu ilitengwa kwa ajili ya choo cha ndani ila hatukukamilisha maana pesa
nayo ikawa haionekani
Patrick:
usijali…nipo hapa…sitaki mke wangu uwe unaenda kuoga nje na watu walivyo hawana
dogo watakuwa wanakuchungulia
Olivia :(anacheka
sana) yaani wewe (anaenda zake kuoga)
Patrick:
oga haraka bwana
Olivia:
poa (anaingia bafuni)
Patrick
:( anaendelea kuangalia runinga ila anaitazama sana nyumba ile kubwa na
yenye ramani nzuri tu sema tu imechakaa sana) lazima nimtengenezee Olivia
wangu mazingira mazuri nay a kuvutia hivi…hamna kwa kweli
Olivia
:( anatoka bafuni) si unaona?
Patrick:
mwenzangu umeoga vizuri kweli
Olivia:
kabisa halafu huwezi kuamini
Patrick:
haya kavae
Olivia
(: haraka anaingia kuvaa, Kama dakika kumi hivi anakuwa amemaliza kuvaa,
anaenda kwenye dressing table yake chakavu anaanza kujipodoa na kama dakika
tano anatoka alipo Patrick) si umeona... (Anamuita mama) mama
Mama :( anakuja)
eeh baba huyo
Patrick:
naam mama, shikamoo?
Mama:
marahaba (kwa Olivia) nini, nimesikia umeniita
Olivia:
natoka mama yangu, tutaonana baadae
Mama:
sawa mama
Patrick
:( anatoa pesa mfukoni mwake kisha anampa mama) mama chukua hizi
zitakusaidia siku mbili tatu mama yangu
Mama:
Asante baba…Mungu akuzidishie
Patrick:
asante mama
Olivia:
kwaheri
Patrick
:( anatangulia nje)
Olivia
:( anamnong’oneza) sh. Ngapi (anacheka) na mimi naomba
Mama:
wee nae mbea embu nenda mwenzio anakusubiri
Olivia
:( anacheka kisha anaenda nje alipo Patrick)
Patrick:
umemeliza kucheka
Olivia
:( anacheka tena)
Patrick:
inaonekana humalizi leo
Olivia
:( anacheka tena)
Patrick:
basi tukae hapa tucheke wote
Olivia:
twende bwana
Patrick
:( anamfungulia mlango anahakikisha kuwa amekaa kisha anapanda kwenye gari analiwasha
halafu wanaondoka)

0 Comments