SCENE 4: -
(Mchana mtulivu, jua kwa mbali
linawaka na kila mtu katika nyumba ya bwana Kenneth anaonekana anafanya kazi Fulani,
wakati huo watoto yaani Ariana na Miriam wapo sebuleni, Ariana anaangalia
runinga huku kwakuwa ni mdogo Miriam amelala kwenye kitanda chake cha kitoto na
wakati huo anajigeuza geuzana kucheza mwenyewe huku dada yake anaonekana hana
hata wazo la kumuangalia na kucheza nae)
Ariana
:( anajisemea moyoni) yaani hili
litoto sijui limetoka wapi yaani linaniudhi maana mama kila saa anamuangalia na
kumpenda yeye…yaani amekuja kunichukulia mapenzi yote ya mama yangu
Miriam
:( anaanza kulialia)
Ariana:
atakoma… (Anaendelea kuangalia runinga)
Keddy
:( anaingia akitokea nje) Ariana
mtoto Analia humsikii?
Ariana
:( anampuuzia mama yake)
Keddy:
nakuongelesha, kwanini mdogo wako Analia humbebi?
Ariana:
huyo sio mdogo wangu mama, sio mdogo wangu kabisa, huyu si mlimkuta hapo nje,
simjui…sio damu yangu
Keddy
:( anajishusha) mwanangu, pamoja na hayo,
huyu mtoto tumemchukua na kumfanya mtoto wetu hauna budi kumkubali
Ariana:
kwani mama huwezi kunipa mdogo wangu wa kiukweli ukweli?
Keddy:
Mungu mkuu mwanangu amenipa mtoto kwa njia yake anayoijua mwenyewe, mwanangu…
Ariana:
hapana mama…nakwambia kabisa kuwa sitaweza kumkubali huyu mtoto Kama mdogo
wangu hata siku moja…kwangu Mimi atabaki kuwa mtoto wa nje na sio mdogo wangu…
Keddy:
nikuambieje mwanangu ili uelewe
Ariana:
siwezi kuelewa hata kidogo na nafsi yangu imekataa kumkubali Miriam kama mdogo
wangu
Keddy:
sawa sina usemi (anamnyanyua Miriamna
kuingia nae ndani)
Ariana:
Hilo litoto ndo sababu ya mimi kukosa mapenzi yako mama
Keddy
:( anarudi) mwanangu tulikaa miaka
kumi na mbili bila kupata mtoto mwingine…wewe mara zote mwanangu ulililia mdogo
wako na kila mara nilishindwa kukupa mdogo wako mwanangu kwasababu ya kwamba
daktari aliniambia sina uwezo wa kushika tena mimba
Ariana:
mama wewe sio mgumba ungesubiri tu Mungu angekupa tu mtoto mama na sio
kuniletea mtoto sijui ametoka wapi na mbaya Zaidi unampenda Zaidi yangu
Keddy:
huo sio ukweli mwanangu nawapenda wote Zaidi na Zaidi wote ni wanangu na
ninawapenda sana wanangu…na hata Mungu analijua hilo
Ariana:
mama unampenda sana huyo mtoto ambae hatujui ni mtoto wa nani kuliko mimi
mwanao wa kumzaa kila saa ni yeye tu, mimi hata hujui nina tatizo gani wewe
unawaza tu kuhusu huyu mtoto
Keddy:
hiyo sio kweli mwanangu mbona hata wewe nakupenda mama
Ariana
:( machozi yanamlenga) natoka shuleni
hata hujui Kama nimerudi au sijarudi wewe kutwa nzima kumuangalia huyo mtoto
Keddy:
lakini huyu bado mdogo na anahitaji kuwa na uangalizi mkubwa…
Ariana:
yupo ma mdogo Mary yupo na mpaka huwa anamnyonyesha inamaana anaweza
kumuangalia vizuri kwanini mama huna muda na mimi na ndo mwanao wa kumzaa...
Keddy:
huelewi mwanangu…hata kama ningezaa mtoto ni lazima ningekuwa ninamuangalia
Zaidi yako
Ariana:
ingekuwa bora maana ningejua kuwa ni mdogo wangu wa tumbo moja wala
ninsingekuwa nina shida na hilo ila huyu mama sio mdogo wangu mama…
Keddy:
lakini ni zawadi na kwa kawaida ya zawadi ni kuipokea na kuitunza mwanangu
(Wakati huo Mary ambae pia ndo
mama wa mtoto Mirriam amesimama pembeni yao na anawasikiliza yote wanaozungumza)
Keddy:
nikuambiaje Ariana ili uelewe kuwa Miriam hayupo hapa kukuchukulia nafasi yako,
nafasi yako itabaki kuwa yako
Ariana:
hatuwezi kufika mwisho mama bora tu uniache mama…na sitawahi kumkubali huyu
mtoto kama mdogo wangu atabaki kuwa mtoto mliomuokota…
Keddy:
nitakupiga sasa, usisahau kuwa mimi ni mama yako na ni lazima uongee na mimi
kwa adabu usione kuwa nimenyamaza ukaona sina akili…nakuvumilia kwakuwa
nakupenda na kumbuka ni wewe ndo ulikuwa unataka mtoto sasa nimeshangaa Mungu
katupa zawadi unaleta ujinga kuwa makini Ariana
Ariana:
nakubali kuwa nilitaka mdogo wangu…nimepata ila siwezi kumkubali maana sio
ndugu yangu
Keddy:
undugu sio kufanana, ni kufaana mwanangu sasa mimi nitatoa wapi mtoto huku
nimekwambia sina uwezo tena wa kupata mtoto…mkubali tu huyu mtoto na utakuwa tu
na Amani mwanangu jitahidi kumchukulia tu kama mdogo wako na utaona kuwa maisha
sio magumu
Ariana:
No! Siwezi kumchukulia kama mdogo wangu
Keddy
:( anaondoka huku amembeba Miriam)
ngoja nimlaze mtoto maana ubishi wako mpaka mtoto amelala
Ariana
:( anaonyesha kukasirika)
Keddy
:( anamlaza mtoto)
Ariana:
kila kitu imekuwa yeye yaani mpaka mimi naonekana sio mtoto wa hapa bali yeye
Mary
:( anakuja alipo Ariana) Ariana
mwanangu
Ariana
:( anamkatisha) najua na wewe upo
hapa kumtetea huyo mtoto hakuna anayenipenda hapa…kila mtu ananichukia na
kuniona sifai
Mary:
hiyo sio kweli Ariana mwanangu…Mimi mbona nakupenda sana
Ariana
:( huku anaondoka) huo ni uongo mtupu
(anabamiza mlango wake kwa hasira)
Keddy
:( anatoka chumbani kwake kwa haraka)
nini hicho?
Mary:
Ariana amebamiza mlango…anaona kila mtu hampendi kisa Miriam…
Keddy:
muache tu…atageuza mawazo kikubwa tuendelee kumvumilia
Mary:
unampenda kweli Miriam, dada yangu utasema ni mwanao wa kumzaa
Keddy:
ni zawadi toka kwa Mungu nahisi Mungu alinisikia kilio changu cha muda mrefu
nahisi nilikuambia kuhusu stori yangu ya kutopata mtoto kwa muda mrefu mara
baada ya kumzaa mwanangu Ariana…kama nilivyokuambia mwanangu Miriam nilimkuta
hapo nje…mama yake alimuacha hapo nje
Mary:
mmeshawahi kumtafuta mama Mirriam?
Keddy:
hapana na wala sitaki kumjua maana atamchukua mwanangu
Mary:
na siku mama yake akitokeza je?
Keddy:
sitaki hata kujua na kufikiria kitakachotokea mara baada ya mama yake Miriam
kutokea ila nitamuomba tu asinichukulie zawadi niliyopewa na Mungu
Mary:(anajisemea moyoni) mama yake Miriam ni
mimi dada, na wala sitamchukua hata siku moja maana unamlea kama mwanao wa kumzaa
upo tayari kugombana na mwanao kisa mwanangu kweli unampenda mwanagu kama
mwanao wa kumzaa, kwanini nimchukue hii siri itabaki moyoni mwangu milele na
milele(anatabasamu)maskini anaona ni
zawadi kutoka kwa Mungu kweli huyu mwanamke ni mtu mzuri sana…sasa sijui mwanae
kamchukua nani maana hata hawaendani tabia
Keddy:
unaonekana kuna kitu unawaza, unawaza nini…mwenzangu?
Mary
:( anacheka kidogo) wala sina
chochote nachowaza…
Keddy:
tupike shoga yangu shemeji yako anakuja sasa hivi kula kwahiyo tumalize kupika
haraka
Mary:
nishapika mbona mie…
Keddy:
uko vizuri mwaya
Mary
:( anatabasamu) Asante mwaya
Keddy: je unadhani kuwa ipo siku
Ariana atamkubali
Mary:
atamkubali tu…endelea kumbembeleza atamkubali tu ipo siku…
Keddy:
tujipe moyo mwenzangu tutashinda
Mary:
kabisa…ipo siku watakaa na kufurahia maisha pamoja mpaka utakuja kufurahi na
kushangaa wewe wape muda tu
Keddy:
na unapenda kweli kunipa moyo mwenzangu
Mary:
ndo ukweli wenyewe
Keddy:
Asante mwaya
Mary:
haya usijali dada yangu
Keddy:
haya asante kwa kunipooza shoga yangu…. naomba tukatenge huyu akija akute
tayari tumeshapika na kutenga
(Kwa pamoja wanaenda kutenga chakula na
wanatenga huku wanaendelea kuongea mambo tofauti tofauti na wanaonekana
wanafurahia na maana wanacheka)
0 Comments