MUNGU MKUU 51


 SCENE 51: -

NYUMBANI KWA VINCENT:

 (Majira ya saa mbili usiku Vincent amekaa nyumbani kwake akiangalia taarifa ya habari huku anapata kinywaji chake cha baridi huku matamanio ya moyo wake yanaonekana machoni kwake kuwa anatamani kuwa na watu pembeni yake)

Vincent: nimewakumbuka wanangu sana mmoja nimeishi nae sema akanikimbia lakini mwingine sijawahi kumuona (anasikitika) sina mke namkumbuka sana Mary sijui nifanyeje nimezungumza nae ila anaonekana ana mawazo sana juu ya mwanae ambae ni mwanangu

(mlango unagongwa)

Vincent: nani usiku huu? (ananyanyuka na kufungua mlango) Colton

Colton: baba (anaingia huku Analia)

Vincent: mwanangu shida nini?

Colton: nimechoka baba…nimechoka kufanya dhambi

Vincent: sielewi unachoongea

Colton: dad

Vincent: embu kaa unywe kwanza maji kisha uniambie

Colton: (anakaa)

Vincent: (anamletea glasi ya maji) kunywa halafu kaa utulie

Colton: (anapokea kisha anakunywa) asante baba

Vincent: usijali…tulia…

Colton: mimi sio mtu mbaya baba ni ujinga wangu tu ndo ulisababisha haya

Vincent: umefanyaje?

Colton: nimejifanya nimekufa ili mdada wa watu aende jela

Vincent: hiyo ni mbaya mwanangu ila bora sasa limeisha au?

Colton: sijui baba ila tu nimeona nitoroke nije nikae na wewe

Vincent: umefanya vyema maana hata mimi nimempata yule mama aliyemzaa mdogo wako amesema nionane nae ili nikutane na mwanangu ingawa anasema mwanangu yupo jela sasa hii ni wiki ya pili

Colton: huwezi amini hata mimi tangu nimefanya huo ujinga hii ni wiki ya pili

Vincent: son, embu nisindikize kesho tukakutane na mama mtoto ili atupeleke kwa mdogo wako mwanangu utajisikia vizuri…ukimuona mdogo wako nimekuwa nikiongelea hilo kwa miaka sasa

Colton: ndio baba…

Vincent: ila sijaelewa kitu umesema kuwa umejifanya umekufa enhe ikawaje baada ya kujifanya umekufa?

Colton: baba nilikaa mochwari kwa usiku kucha palipokaribia kukucha nikaja kuchukuliwa na askari mmoja akanitoa

Vincent: mochwari wewe mtoto?

Vincent: ndio baba mochwari

Vincent: aisee watoto utasema huna kwenu…huku una kwenu na mimi baba yako nina nyumba za kutosha za wewe kulala sasa ukaenda kulala mochwari (anasikitika) enhe kwahiyo wakakuzika au?

Colton: hapana …askari waliolipwa na Ariana wakanitorosha ila walitengeneza kaburi

Vincent: (anashangaa)

Colton: baba nimefanya kosa najutia

Vincent: jutia mwanangu umefanya jambo baya sana kwanza ni dhambi…kumbuka una mdogo wako wa kike utajisikiaje mtu akimfanyia kama ulivyomfanyia huyo binti?

Colton: baba tufanyeje?

Vincent: aisee kwani kesi inaanza kusikilizwa lini?

Colton: baada ya wiki mbili

Vincent: tuna muda wa kujifikiria cha kufanya

Colton: maskini Miriam…

Vincent: ndo nani

Colton: huyo dada…yupo jela kwa kosa ambalo hata sio kosa

Vincent: nikupe nini ili ulale mwanangu? Kesho ukiamka utaenda kwa dada yako mtaongea atakushauri cha kufanya

Colton: yes, dad…ngoja nikaoge nilale

Vincent: hauli?

Colton: No dad…sili lakini kabla ya kesho natamani kwenda kanisani nimuombe Mungu wangu msamaha kwa kujifanya nimekufa…ili mtu mwingine ateseke

Vincent: pole mwanangu

Colton: ila kwanini naumia sana…kwanini naumia kupita kiasi?

Vincent: sababu wewe sio mtu mbaya hata kama tukilazimisha

Colton: (machozi yanamtoka)

Vincent: (anamfuta machozi) acha kulia mwanangu…(anamkumbatia) baada ya kuonana na dada yako tutafanya mpango huyo binti uliyemsingizia atoke gerezani

Colton: okay dad… (ananyanyuka na kwenda chumbani kwake)

Vincent: maskini mwanangu ila najua kesho akikutana na mdogo wake atakuwa sawa tu

Post a Comment

0 Comments