SCENE 3: -
(Asubuhi ya siku nyingine Mary
yupo jikoni akiwaandalia watoto na wenye nyumba chai na kumuandaa Ariana kwa
ajili ya shule)
Keddy
:( anakuja akiwa amembeba mtoto Miriam)
za asubuhi Mary…
Mary:
salama dada shikamoo…
Keddy:
marahaba…umeamkaje?
Mary:
salama tu…
Keddy
:( anamuangalia mtoto) yaani ana njaa
kweli huyu, fanya mpango wa maziwa nadhani yapo kwenye friji fanya hivyo mdogo
wangu
Mary
:( anajikuta anaropoka ghafla) mlete
nimnyonyeshe…
Keddy:
(anashangaa) umnyonyeshe? (Anacheka kidogo) utamnyonyeshaje?
Mary
:( anajichekesha) unajua…dada…Mimi
mwenyewe nimetoka kujifungua yaani sina hata wiki…
Keddy:
mtoto yuko wapi?
Mary
:( anasikitika kidogo) amefariki…
Keddy:
Oh…maskini pole Sana…najua inavyouma kwa mama kumpoteza mtoto wake…Mungu
atakutetea usijali mdogo wangu
Mary:
Asante dada… (Anamchukua mtoto)
maskini kaone kanavyotetemeka...
Keddy:
njaa mbaya…tangu amekuja tunamnywesha maziwa ya ng’ombe maana Mimi sio mama
yake nadhani nilikuambia ila nitamlea Kama mwanangu wa kumzaa kabisa
Mary:
Mungu akakubariki wewe na familia yako milele na milele kwa kumtunza huyu
kiumbe ambae hamjui hata ametokea wapi…
Keddy:
Mimi na mume wangu tumetafuta mtoto huu ni mwaka Zaidi WA kumi, Ariana
alitusumbua kuwa anataka mdogo wake mpaka tukajuta ila Mungu amejibu maombi
yetu kwa kutuletea huyu mtoto…
Mary
:( huku anakaa Ili amnyonyeshe mtoto)
mungu ni mkuu na fadhili zake ni za milele na pia njia zake hazichunguziki
kabisa…
Keddy:
hakika…
Ariana
:( anakuja akiwa anatokea chumbani kwake)
shikamoo mama…
Keddy:
marahaba mwanangu umeamkaje mama?
Ariana:
salama… (Anamuangalia Mary) shikamoo…anti
Mary:
marahaba…
Ariana:
iiii, mama mbona anamnyonyesha mtoto?
Mary
:( anacheka kidogo) Mimi mwenyewe
nimetoka kujifungua juzi juzi tu ila mwanangu amefariki
Keddy:
usiogope…mwanangu…Miriam ni mdogo wako tu (Anatabasamu
huku anamshika nywele zake)
Ariana:
Mimi nataka tu mdogo wangu wa tumbo moja…mama kwani haiwezekani?
Keddy
:( anamuangalia)
Ariana:
nataka tu mdogo wangu wa tumbo moja
Keddy:
Ariana tafadhali usianze tena shida zako we mtoto
Ariana
:( anavuta mdomo)
Keddy:
naomba ukaoge uwahi shule…
Ariana
:( anaingia chumbani kwake)
Mary
:( amekaa kimya)
Keddy:
yaani huyu mtoto…
Mary:
Ni utoto tu dada hata usijali kabisa na kila kitu kitakuwa sawa na unaweza
kushangaa akaja kumpenda kama mdogo wake wa tumbo moja kikubwa ni kumvumilia tu,
mpeni muda tu dada
Keddy:
sawa bwana kama unachosema kitakuwa basi Bwana akubariki
Mary
:( anacheka) narudia kusema usimkatie
tamaa
Ariana
:( anatoka kuoga anakuja jikoni) chai
iko wapi mi nataka kwenda shule
Keddy
:( anatabasamu) yaani unawahi huku
anayekupeleka hajaamka bado
Ariana:
inamaana hunipeleki wewe?
Keddy:
hapana…Mimi nabaki na mtoto
Ariana
:( anashikwa na hasira sana)
Mary:
usijali…Ariana…mama atakupeleka (anamgeukia
keddy) dada mpeleke tu…Mimi nitabaki na kichanga nitamuangalia vizuri…
Keddy:
sawa… (Anaingia chumbani kwake) mume wangu
(anamgusa) amka baba…mbona leo
umelala sana?
Ken
:( anajigeuza) ah…uchovu tu mama…vipi
Ariana ameshaenda shule?
Keddy:
ndo naoga nimpeleke
Ken:
Miriam atabaki na nani? Acha tu nimpeleke hata hivyo nataka kwenda kazini sasa
hivi
Keddy:
Ariana anataka apelekwe na mimi…
Ken:
Ariana nae ana masharti kweli…haya mpeleke ngoja na mimi nijiandae niende
kazini
Keddy:
sawa, ngoja nioge haraka (anaingia
bafuni)
(Upande wa Ariana na Mary)
Ariana:
ila huyo mtoto ni wako eti ee?
Mary:
(anashtuka) kwanini unasema hivyo?
Ariana:
mbona unamnyonyesha Kama sio mwanao?
Mary
:( kimya)
Ariana:
nakuuliza…nijibu
Mary
:( anajichekesha) Ariana bwana…si
nimekuambia kuwa nimejifungua juzijuzi tu na bado natoka maziwa…kwanini yakae
hivyohivyo huku kuna mtoto anayahitaji?
Ariana:
haya bwana Kama ni hivyo
Mary:
uko darasa la ngapi?
Ariana:
la Saba…
Mary:
kumbe unamalizia…
Ariana:
ndio… (Anamalizia kunywa chai)
Mary:
Ariana mpende Sana mdogo wako huwezi jua Mungu ana makusudi gani kwa kumleta
huyu
Ariana:
kwani Mungu ana makusudi gani?
Mary
:( anakaa kimya)
Ariana:
nachojua huyu sio mdogo wangu na hata siku moja sitampenda kama mdogo wangu
Keddy
:( anatokea chumbani na kusikia maneno
yale) Ariana…
Ariana:
siwezi kujifanya kumpenda huyu mtoto…siwezi tu kufanya hivyo nisameheni Kwa
kweli
Keddy:
umeingiwa na nini Ariana?
Ariana:
sio mdogo wangu tumbo moja…mama hata hatumjui katoka wapi na mama yake ni nani
je wakiwa ni watu wabaya?
Keddy:
Miriam ni malaika tu mwanangu hana hata hatia yoyote…ni zawadi ambayo Mungu
ameamua kutupatia wewe huoni fahari kuwa na mdogo mzuri?
Ariana:
mama nachelewa shuleni…
Mary
:( anajisemea moyoni) hili ni
tatizo…eeh…Mungu mnusuru mwanangu na Ariana…
Keddy:
Mary…kaa na mtoto nakuja baada ya muda kidogo ngoja nimpeleke huyu shuleni
Mary:
sawa dada
(Keddy na Ariana wanatoka nje na kupanda kwenye gari na mara baada ya
kukaa kwenye gari, Keddy anawasha gari na bila kupoteza muda wanaondoka
kuelekea shuleni huku kila mmoja wao amekaa kimya na hataki kumuongelesha
mwenzie)
Keddy :( anavunja ukimya) nakupenda mwanangu
Ariana :( kimya huku anaangalia pembeni)
Keddy: (anaamua kukaa kimya)
0 Comments