SCENE 49: -

NYUMBANI KWA KEN

(Majira ya saa mbili na robo usiku, Ken na familia yake wamekaa wanapata chakula cha usiku, kila mmoja anaonekana hana raha)

Keddy: yaani sijisikii kula kabisa jamani

Ken: jitahidi mke wangu…kula kidogo Miriam anatuhitaji tukiwa wote tuna nguvu

Keddy: maskini mwanangu…

Ariana: (anajisemea moyoni) eti mwanangu…(anafyonza)

Mary: anaendelea vizuri

Ken: enhe asubuhi alijisikia vibaya…umeenda kufuatilia shida ni nini? Maana sikuweza kwenda kwa sababu presha yangu ilipanda…

Mary: pole sana…kaka niliwapeleka ndugu zangu wakamuone…na pia nilimpeleka baba yake

Keddy: kumbe mlikuwa mnawasiliana?

Mary: hata Miriam ameniuliza hivyo…No sikuwa nina mawasiliano nao siku moja mama alinipigia akasema baba Miriam ananitafuta sana…sasa sijui labda alienda nyumbani nikakutana nae ndo nikaona nimpeleke akamuone Miriam maana alikuwa anatamani kumuona Miriam

Ariana: (anabenjua midomo)

Mary: Miriam amefurahi sana

Keddy: (anatabasamu)

Mary: halafu kuna habari tumekutana nayo

Ken: ipi tena?

Mary: ni mjamzito

Ken: acha bwana

Keddy: ndo maana alijisikia kichefuchefu

Ken: huwezi kuamini hata sijakasirika sijui kwanini

Ariana: (ananyanyuka) nimeshiba

Keddy: uko sawa Ariana?

Ariana: yeah (anaingia chumbani kwake)

Keddy: shida nini?

Mary: atakuwa ameshiba kweli muache akapumzike…tuna mambo mengi sana ya kufikiria kumbuka yeye ni dada yake Miriam kama tulivyo hatuna hamu ya kula hata yeye hana hamu ya kula

Ken: kuna kitu hakiko sawa sijui ni nini ila nahisi kuna kitu hakipo sawa

Keddy: kama nini baba Ariana?

Ken: sijui

(Mary na Keddy wanaangaliana)

Keddy: sikuelewi

Ken: huwezi

Mary: fafanua

Ken: tuachane nayo

Keddy: haya bwana kama hutuambii

Ken: ila kwa yote nimefurahi tumezeeka

(wanacheka)

Keddy: kadada anatuletea ka Miriam kadogo

Mary: katakuwa ka Jeremy maana hampendi Jeremy huyo

Keddy: ee kweli

Mary: anamkataa

Ken: eeh mtoto ana balaa huyu…Jeremy anasemaje

Mary: si unamjua alivyo mpole anafukuzwa anaondoka lakini kesho anarudi tena

(wanacheka)

Keddy: habari hii imetusaulisha machungu yaani kisema cha baba Ariana wala hata sijachukia…yaani hata kama majirani watatunyooshea kidole lakini hii habari naamini imemfurahisha hata Miriam

Mary: kabisa

(Huku ndani alipo Ariana)

Ariana: (Analia) Miriam ana mimba ya Jeremy ana mimba ya Jeremy yule Malaya amepata nafasi tena ya kuwa na furaha halafu sasa kama kawaida watu wanamfurahia kwani mimi nina balaa gani hapa nimechanganyikiwa na mengi siku ile sikuukuta mwili wa Colton sijui yuko wapi yaani hata sielewi…halafu nimekaa nakula Napata habari ya kwamba Miriam mjamzito…oh comeon they must be kidding…(anajitupa kitandani) embu ngoja nihakikishe hizi habari maana huyu Mary anajifanyaga kiropo sana (anachukua simu yake na kumpigia Jeremy)

(Simu inaita)

Jeremy: (anapokea) hello shem

Ariana: ah…yes za kwako?

Jeremy: ah kama unavyojua mambo yangu sio mazuri sana…ila namtukuza Mungu nipo napumua

Ariana: okay ulienda kumuona Miriam?

Jeremy: ndio hata hapa nimetoka kumuona siwezi kumuacha hasa kwenye wakati huu…

Ariana: wakati gani?

Jeremy: Miriam is pregnant with my child…I swear Ariana iam so happy…penzi letu limezaa matunda…

Ariana: (anachukia sana)

Jeremy: Miriam is pregnant with my child

Ariana: sasa nini faida ya kuwa na ujauzito huku baada ya wiki moja anaenda kuhukumiwa kifo?

Jeremy: (anacheka)

Ariana: unacheka nini?

Jeremy: embu tuiachie mahakama iamue juu ya hilo

Ariana: ushahidi wote unaonyesha ameua

Jeremy: eeh ahata mimi niliona kuwa dogo ushuhuda wote unamuonyesha kuwa ni muuaji…ila tusubiri si bado siku kadhaa tu?

Ariana: Miriam atakufa get that in your head Jeremy and move on

Jeremy: nitakuwa na Miriam hata mpaka siku ananyongwa na kama ikiwezekana I will live in her memories I will refuse to forget her…she is the love of my life

Ariana: bora yake

Jeremy: yes…enhe ulinipigia simu kuniambiaje?

Ariana: nothing…

Jeremy: hujafurahi kusikia kuwa mdogo wangu amenibebea mimba (anatabsamu) you should see her…kang’aa kamimba kamempenda kweli yaani…(anacheka)

Ariana: (anakata simu kwa hasira) shit…that woman…damn her…I hate her… (anafuta machozi) ni sawa lakini acha wajipe moyo kwamba wataomba mahakama wampunguzie adhabu kisa ana mimba…atahukumiwa tu na mtoto ataachwa kama yatima nikiwa mama yake wa kambo nitamtesa sana yaani hawataamini… wajipe moyo tu

(Huku kwa Jeremy)

Jeremy: lets wait for that day…siku sio nyingi…dunia itashuhudia Ukuu wa Mungu …watu watakiri kwa vinywa vyao kuwa MUNGU MKUU kwa maajabu atakayoyaonyesha…Mungu wetu sio kiziwi na wala hataacha mwenye haki aibike…tusubiri hiyo siku…oh my love thank you for ths gift najua tumeenda vibaya tumezini ila Mungu amelipanga hili...nakupenda Miriam wangu…Mungu naomba uwe nasi siku ya hukumu…hakimu atusikie tunachosema

(Kwa Ariana)

Ariana: nina uhakika watashindwa watu watakuwa wanazimia kama nzi siku hiyo acha wajishaue…yaani nitacheka siku hiyo nitafurahi sana na Miriam na limimba lake hilo litoto la laana watakufa pamoja (anacheka kwa nguvu) naisubiri kwa hamu sana siku ya hukumu…

Post a Comment

0 Comments