SCENE
47: -
BAADA
YA MWEZI MMOJA: -
MAHAKAMANI:
-
(Asubuhi
iliyo njema kwa watu kasoro kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Miriam ambao wana
huzuni nyingi kwa lile lililopo mbele yao, Ariana nae yupo na anajifanya kuwa
na huzuni kama walivyo wengine)
Mwanasheria:
(anashusha pumzi) hata sijui nifanyeje
Jeremy:
kwanini?
Mwansharia:
rekodi inayoonyesha rekodi ya simu za Miriam zimepotea
Ariana:
Mungu huyo yaani mlikuwa mnanisingizia mimi kuwa niliongea na Miriam jioni ile
ona sasa yamepotea
David: (baba
yake Jeremy) nani alikusingizia?
Ariana:
si Miriam
David:
aisee
Keddy: (amekonda
kwa mawazo) mimi sijui nachotaka mwanangu tu awe huru ameteseka mwezi mzima
Ken:
acha tu
Mary:
mimi namuachia Mungu tu naamini mwanangu kwa vyovyote vile atakuwa huru
Mwanasheria:
hatuna cha kujitetea kwa upande wetu…na hilo ndo tatizo
Vanessa:
vipi nguo za Miriam alizokuwa amevaa jioni ile?
Mwanasheria:
haijulikani ziko wapi…
Mary:
Mungu wangu mwanangu
Mwanasheria:
njooni ndani naona inataka kuanza
(Wanaingia,
wote wanakaa upande atakaokaa Miriam)
Miriam: (anaingia akiwa na unyonge, pembeni
yake kuna askari magereza wawili)
Mary: (anamuangalia
mwanae) Mungu ulinipa mtoto pekee huwezi kumchukua mapema huwezi kumchukua
mwanangu nakuomba Mungu…mama na baba yangu wako wapi niliwapigia simu wakasema
wanakuja kumuona mjukuu wao kwa mara ya kwanza tangu azaliwe wako wapi
jamani…wangekuja labda wangenipa nguvu (anapokea ujumbe kwenye simu yake)
dada…amesema wapo hapo nje… (kwa mwanasheria) naomba nikawachukue watu hapo nje
mara moja…
Mwanasheria:
sawa ila usichelewe hakimu akiingia usiingie
Mary:
(anatoka haraka anapofika nje anamuona dada yake pamoja nawazazi wake)
asante kwa kuja nilikuwa nawahitaji sana
Mama:
hujambo mwanangu?
Mary: Mary:
shikamoo mama, shikamoo baba, shikamoo dada
(Wanaitikia)
Dada:
pole mdogo wangu ila Mungu yupo
Mary:
asante…haya twendeni ndani…
(Wanaingia)
Hakimu:
(anaingia)
Watu: (wanasimama)
Hakimu:
(anaketi)
Watu: (wanaketi
pia)
Dada: (kwa
Mary) mtoto ni yule pale mbele…
Mary: (kwa
kunong’ona) ndio
Dada:
mnafanana
Mary: (anatabasamu)
Huyu (anamshika Jeremy) mkwe wetu
Dada: oh,
baba hujambo?
Jeremy:
sijambo shikamoo mama
Dada:
marahaba… poleni yatapita tu haya
Jeremy:
nina uhakika
Mary:
haya tusikilize
Mwendesha
mashtaka: Miriam Kennedy…anashtakiwa na jamhuri ya muungano wa tanzania kwa
kosa la kumuua kwa kumshambulia kwa kisu bwana Colton Mshana usiku wa tarehe
13/04… (kwa Miriam) kweli sio kweli
Miriam:
(amekaa pembeni ya mwanasheria wake) sio kweli
(Minong’ono)
Hakimu:
naomba utulivu tafadhali
(Utulivu)
Mwendesha
mashtaka: basi tukusikie mwanasheria upande wa mshtakiwa
Mwanasheria:
(ananyanyuka) asante mheshimiwa hakimu…mnamo tarehe 13/04 saa moja jioni
mteja wangu alipigiwa simu na dada yake akitakwa waonane kuna maongezi kidogo
wanataka wafanye bila kusita mteja wangu alichukua usafiri mpaka eneo
waliokubaliana alipofika dada yake alimwambia asubiri anakuja lakini ghafla
mteja wangu alisikia mtu anambana pua na hatimaye akaanguka chini alipoamka
alikuta marehemu amelala pembeni yake na mikono yake imejaa rangi inayofanana
na damu
(Minong’ono)
Hakimu:
(anagonga meza kuamuru utulivu)
(Utulivu)
Mwanasheria:
hajakaa vizuri polisi wakafika na kumkamata kwa kosa la mauaji… ni hivyo tu
mheshimiwa (anainama kisha anaenda kukaa)
Hakimu:
mwanasheria upande wa Jamhuri
Mwanasheria
2: (ananyanyuka) asante mheshimiwa (kwa mwanasheria 1) umesema
kuwa mteja wako alipigiwa simu na dada yake…
Mwanasheria
1: ndio
Mwanasheria
2: wewe ni mwanasheria wa utetezi …tuone basi rekodi za simu ya huyo mteja wako
Mwanasheria
1: zimepotea
Mwansheria
2: zimeenda wapi?
Mwanasheria
1: siwezi kufahamu (anageuka na kumuangalia Jeremy)
Mwanasheria
2: hujui eeh hivi kwanini nakuuliza wewe … (kwa hakimu) naomba nimuite
mtuhumiwa ndo nimhoji maana yeye ndo alikuwepo
Hakimu:
fanya hivyo
Miriam:
(ananyanyuka na kwenda kizimbani)
Mama Mary:
(anamuangalia kwa upendo) mjukuu wangu mrembo…
Jeremy:
(anamuangalia kwa upendo sana) be strong my love…
Miriam:
(amesimama kizimbani)
Mwanasheria
2: mtetezi wako amesema kuwa ulipoamka ukakuta rangi inayofanana na damu…
Miriam:
ndio
Mwanasheria
2: ulijuaje?
Miriam:
ilikuwa sio damu…
Mwanasheria
2: unatudanganya ee
Miriam:
hapana
Mwanasheria
2: (analeta nguo za Miriam) hizi ndo nguo zako?
Miriam:
ndio
Mwanasheria
2: zina damu na damu yenyewe ni ya mwanadamu na mwanadamu huyo ni Colton
(Minong’ono)
Hakimu:
(anagonga meza)
(Utulivu)
Mwanasheria
2: (anampelekea nguo hizo hakimu)
Hakimu:
(anaziangalia) kweli zina damu na vipimo vinaonesha kuwa ni damu ya
Colton
Mwanasheria
2: sasa je unapotuambia kuwa uliona rangi
Miriam:
haki ya Mungu tena nasema ukweli
Mwanasheria
2: unasema uongo kujitetea
Miriam:
sio kweli
Mwanasheria
2: nimemaliza… (kwa hakimu) mtuhumiwa anadanganya na anafanya juu chini
kujitetea ili aepuke adhabu naomba mahakama yako tukufu impatie mtuhumiwa
adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wote…alimuua yule mwanaume ili atunze
penzi lake na hawara yake mwingine mwenye pesa Zaidi
Jeremy:
mimi hawara tena? (anatikisa kichwa)
Miriam:
kila neno unaloongea ni uongo…ninampenda mwanaume aliyenichumbia na pia
sikuwahi hata siku moja kumsaliti kwa kumuangalia mwanaume mwingine huyo Colton
nilikuwa simfahamu nilimfahamu siku alipoletwa na dada Ariana
(Minong’ono)
Hakimu: (anagonga
meza kuamuru utulivu)
(Utulivu)
Mwanasheria
2: usitumie nguvu nyingi maana tayari imeshajulikana kuwa wewe ni muuaji na
sababu yake ni hiyo
Miriam:
usiusemee moyo wangu
Hakimu:
(kwa Miriam) acha kujibizana na mwanasheria…
Ariana:
(anacheka)
Jeremy:
(anamuona) sasa nini kinachekesha hapo?
Ariana:
eeh jamani kwahiyo hata kucheka napangiwa
Jeremy:
Mungu akusamehe Ariana
Ariana:
embu niacheni mie
Dada
yake Mary: (anamuangalia Miriam) maskini ameshalia mpaka amekinai…
Miriam:
(anataka kutapika)
Hakimu:
naomba niahirishe hili mpaka baada ya siku kumi na baada ya kusikia ushahidi
wote mahakama hii ipo tayari kutoa hukumu yake labda kama kuna mabadiliko
ambayo naamini hayapo (anagonga meza anasimama na kuondoka zake)
Watu: (wanasimama
pia)
Jeremy:
(anamkimbilia Miriam) baby are you okay… (anamkumbatia)
Miriam:
najiskia vibaya…
(Askari
magereza wanamchukua na kuondoka nae)
0 Comments