MUNGU MKUU 48


 

SCENE 48: -

RUMANDE: -

(Jioni yake, Miriam yupo na rafiki yake waliokutana jela wanazungumza mawili matatu huku Miriam anaonekana bado anajisikia vibaya)

Rafiki: una nini lakini miriam mbona sikuelewi? Nasikia ulijisikia kichefuchefu mahakamani

Miriam: hata sijui eliza

Eliza: umeona siku zako?

Miriam: zimepitiliza sijaona…kwani vipi?

Eliza: unaweza kuwa mjamzito

Miriam: haiwezekani

Eliza: kama ulitembea na shemeji ndo majibu yake

Miriam: hii ni aibu… jamani sikutegemea na siku hiyo tulijisahau hata haikuwa lengo na ilitokea mara moja tu

Eliza: (anatabasamu) hiyo mara moja sasa ndo imetuletea habari njema

Miriam: Mungu wangu...

Askari: Miriam una wageni

Miriam: oh, kama ni Jeremy mwambie siwezi kumuona

Askari: wamekuja watu kama saba ni ndugu zako…

Miriam; (ananyanyuka na kutoka anapiga hatua mpaka walipo ndugu zake)

(Miongoni mwa wageni hao wapo wazazi wa Mary, Jeremy, Vanessa, dada wa Mary na mwanaume mmoja wa makamo ya mzee Ken)

Miriam: shikamooni

(Wanaitikia)

Vanessa: hello Miriam

Miriam: mambo?

Miriam: poa

Mary: unaendeleaje mama?

Miriam: bado najisikia kizunguzungu

Mary: pole mama

Jeremy: pole sana…utapona

Miriam: asante…

Mary: Miriam...nimekuja na hawa watu leo walikuwa wanataka kukuona

Miriam: (anatabasamu)

Mary: hawa ni bibi na babu yako

Babu: mke huyo

(Wanacheka)

Miriam: (anamkumbatia)

Bibi: mke mwenza…

Miriam: (anamkumbatia)

Mary: huyu ni mama yako mkubwa ni dada yangu

Miriam: (anamkumbatia)

Mary: na huyu ni baba yako mzazi

Miriam: mlikuwa mnawasiliana?

Mary: hapana mama…niliunganishwa na bibi na babu yako kwa miaka mingi kumbe alikuwa anakutafuta…waliponipata mimi ndo nikaona nije nikutambulishe

Miriam: sawa nimefurahi kusikia…mimi naitwa Miriam

Baba: (anacheka) nakujua… mimi naitwa Vincent na wewe ni mwanangu wa pili na wa mwisho

Miriam: nina kaka au dada?

Vincent: kaka

Miriam: (anamkumbatia)

(Wanafurahi)

Vanessa: shoga una familia mbili

Miriam: (anacheka) Mungu amenipendelea

Askari: (anakuja)

Miriam: muda umeisha?

Askari: hapana nimeleta majibu yako hapa mpo wote naona ni muda mzuri kusema

Mary: majibu ya nini?

Askari: Miriam ni mjamzito

Jeremy: (anafurahi kupita kiasi) oh My God…naenda kuwa baba…Oh God

Miriam: (anakaa kimya)

Mary: Miriam

Miriam: mama hata sikupanga haki ya Mungu mama nisamehe

Mary: kwani mimi nimesemaje?

Dada: hongera sana mwanangu najua umeipata bila kuwa na ndoa ila ni Baraka hongera sana

Miriam: mnasema kweli? Ila sasa ndo naenda kunyongwa naombeni niitoe hii mimba

Vincent: nani kasema unaenda kufungwa mwanangu? Hufungwi wala kunyongwa bado upo sana embu niachie mke au mume mwenza nijidai mimi…

(Wanacheka)

Jeremy: thank you my love…kwenye wakati mgumu kama huu tumepata jambo jema

Miriam: (anatabasamu)

Babu: hongera mke kwa habari hii njema…tutailea ni kwa bahati mbaya sana hatukukubali wewe maana mama yako nae alikuzaa akiwa bado mtoto mdogo sana alituudhi tukamfukuza hii dhambi inatutafuna …sasa kwako tutamlea huyo mtoto…

Bibi: (anamshika tumbo) aje huyo kiumbe atakayekuwa Baraka kwa ulimwengu mzima

Miriam: oh, bibi jamani…asante kwa Baraka zako

Vanessa: hongera sana rafiki yangu

Jeremy: hongera (anamkumbatia)

Miriam: (anamkumbatia pia)

Mary: nitawaambia Keddy na Ken

Jeremy: asante Mungu (anambusu Miriam)

Miriam: (anaona aibu)

Vincent: oh mwanangu...nimefurahi kukuona na Zaidi kusikia habari hii kuwa naitwa babu baada ya miezi kadhaa

Mary: asante Mungu

Vincent: tukija tena tutakuja na kaka yako…

Miriam: mlete kabla sijanyongwa

Jeremy: honey please

Miriam: just kidding…nendeni sasa

(Wanacheka)

Jeremy: (anambusu) kesho

Miriam: haya tuopo jamani

(Wanaondoka)

Miriam: (anarudi rumande)

Post a Comment

0 Comments