IAM IN LOV E WITH MY HOUSEGIRL 51

 


SCENE 51: -

(asubuhi ya siku ya jumapili kama ilivyo kawaida ya Raymond kukaa bustanini kwake akiperuzi mtandaoni na kipenzi chake anafanya usafi na kazi nyingine. Nje ya geti kunasikika honi na haraka Ramadhani anafungua geti hilo na kuruhusu gari la Christina kuingia ndani. Christina anaegesha gari lake kisha anashuka kwenye gari, Angelina nae anatokea ndani hivyo wanakutana)

Angelina: shikamoo...Dada

Christina: marahaba…Raymond yuko wapi?

Angelina: bustanini… (Anamuongoza njia)

Christina :( anamfuata)

(Wanafika)

Raymond :( akiwa hajamuona Christina anamshika mkono Angelina na kupeleka kidevuni kwake) we mbona kama bado unaniogopa? mimi ni mumeo unajua(anacheka)

Angelina: dada Christina anakuja

Raymond :( anamuachia) ndo maana unaogopa au?

Christina :( anafika alipo) habari yako Raymond

Raymond: salama shikamoo…?

Christina: marahaba...za hapa?

Raymond: nzuri tu… (kimya kidogo) karibu uketi

Christina :( anaketi kiti cha pembeni kidogo na Raymond)

Raymond: karibu

Christina: Nina mazungumzo na wewe…

Raymond: okay…karibu nakusikiliza… (Anaacha kuperuzi na kumsikiliza)

Christina: wawili Mimi na wewe, naomba Angelina utupishe

Raymond:(anacheka kidogo) labda hujui au labda umesahau…ni kwamba, Angelina ni mchumba wangu yaani mke mtarajiwa sasa unapomwambia mazungumzo ni yetu na atupishe unamvunjia adabu unajua? hakuna cha kufichana kati yangu mimi na Yeye...

Christina: samahani

Angelina: ngoja nikalete vinywaji (anaondoka)

Christina: sorry

Raymond :( anamuangalia sana) enhe sema shida yako tafadhali

Christina: naomba unisamehe

Raymond: nitakusameheje huku sijui kosa lako? Nikusamehe nini?

Christina:(anacheka kidogo) maisha bwana…nilijaribu kukurudisha akili yako nyuma miaka miwili ili ukumbuke penzi letu na lengo lilikuwa nikurudishe kwangu na tufunge ndoa iliyokuwa imepangwa kama miezi nane iliyopita (anacheka) ila kwa bahati mbaya, moyo ukazidi akili… (Kimya huku anamuangalia Sana Raymond) ukadhihirisha kuwa moyo wako ni wa Angelina na hata tufanye nini hatuwezi kubadili hilo

Raymond :( anamuangalia Sana)

Christina: najua hunielewi

Raymond: nakuelewa…vizuri Sana Christina na tulikuwa tunajiuliza nani atakuwa amenifanyia hivyo…akili ilikuwa sio yangu kwa siku kumi zilizopita sijui nilisumbua watu hapo sijui

Christina: naomba unisamehe sana Raymond nilikosea sana

Raymond: nimeshakusamehe ile tu wewe kugundua ulichofanya ni kibaya tayari umeshatubu makosa yako nimekusamehe mama…yaishe

Christina :( analengwa na machozi) its funny right? Yaani tumekaa almost six years lakini hatukuwa na mapenzi baina yetu kila mtu alikuwa anawaza yake mimi nilimpenda Peter na wewe njiani ukakutana na Angelina na kumpenda sana, its funny eti eeh

Raymond :( anacheka kidogo) sometimes ni hivyo…maisha ndivyo yalivyo...Unaweza kukaa na mtu muda mrefu halafu sio ubavu wako na ukakutana na mtu wiki mbili tu akawa ubavu wako

Christina :( anacheka) ni kweli

Raymond :( anacheka pia) nimefurahi umejua hilo…wewe ni mwanamke mrembo you deserve pure happiness...kama mimi nilivyopata furaha kwa kukutana na Angelina na nikampenda regardless hatufanani kitabaka

Christina: hata Mimi na Peter

Raymond: exactly…go girl…go and fight for your love and get it back wewe na Peter mnapendana na kila mtu anajua hilo…

Christina:(anaguna) samahani tena

Raymond: nini tena?

Christina: muda wote huo nilikuwa natembea na baba yako, nilifanya vile sababu ya uroho wa mali na pesa… (anasikitika) yaani najisikia vibaya sana...

Raymond: its okay Christina…na sijui nikwambieje naishukuru ile siku hata kama ilikuwa ni ngumu kumeza ila baada ya hapo matokeo yake yalikuwa mazuri (anacheka kidogo) baada ya hapo badala mahusiano yangu na baba yangu kuwa mabaya yamekuwa mazuri na baba amekuwa akinisikiliza sana…yaani amebadilika sana mpaka mama anashangaa …

Christina:(anacheka)

Raymond: ilikuwa mbaya lakini imetoa matokea mazuri sasa mimi na baba yangu hatugombani hovyo...Amekuwa hana gubu Kama zamani

Christina: ndo hivyo bwana mambo hubadilika na unakuta kitu kidogo ndo kimesababisha

Raymond: kweli kabisa

Christina:(kimya huku anamuangalia) nitakukumbuka lakini maana nilikuwa nimekuzoea sana

Raymond: pamoja na yote tutabaki kuwa marafiki wazuri tu my dear

(wanakumbatiana)

Angelina:(anakuja akitokea ndani akiwa amebaba vinywaji kwenye trei anapoawaona anakosa raha na wivu unampanda anaamua kurudi ndani)

Christina:(anamuona Angelina) mama mwenye nyumba unaenda wapi?

Angelina:(anarudi) nilikuwa naenda ndani

Christina:(anamfuata na kuchukua glasi moja ya kinywaji) yaani juisi tu umeenda kuchukua mwaka tangu tumeanza mazungumzo mpaka tumemaliza

Raymond:(anacheka)

Angelina: nilikuwa natengeneza juisi

Raymond:(anachukua kinywaji) muda wote huo?

Christina: Angelina naomba umtunze Raymond na usipomtunza nitamrudia

Angelina:(anacheka)

Raymond:by the way…nichukue nafasi hii kukukaribisha kwenye harusi ya Edmond na Catherine

Christina: oh (anaweka kinywaji mezani) nitakuja...ni lini?

Raymond: mwezi ujao

Christina: sawa…nitakuja…

Raymond: karibu sana...

Christina: sawa…ngoja niwaache jamani

Raymond: haya bwana sie tupo

Christina: nawatakia kila la kheri katika mipango yenu ya harusi na Maisha pia

Angelina na Raymond: asante sana (wanatabasamu)

Christina: (anaondoka)

Angelina: huyu ni Christina?

Raymond: ndo yeye...au kwanini usimkimbilie umuulize

Angelina: amekuwaje?

Raymond: nahisi amechoka tu

Angelina: kwakweli

Raymond:(anampakata)

Angelina:(anamkalia huku anamuangalia kimahaba)

Raymond: unataka kufanya nini

Angelina: wapi?

Raymond: nimeagiza msichana mwingine…

Angelina: umekumbuka hilo?

Raymond: Ramadhani aliniambia kuwa nilimuagiza nikajua labda nilimuagiza wakati akili imehamia miaka miwili iliyopita

(wote wanacheka)

Raymond: sasa huyo dada akija nataka uwe unafanya kitu Fulani

Angelina: mimi si hausigeli?

Raymond: ulikuwa…ila sasa wewe ni mchumba wangu na ninakupenda sana na utakuwa mke wangu hivi karibuni nataka uwe na kazi yako

Angelina: Mimi unajua sijasoma

Raymond: ah akili tu mke wangu…utaniambia unataka kufanya nini?

Angelina: sawa...Nitakuambia

Raymond: enhe…nambie

Angelina: mama amefurahi sana kukuona umerudi kwenye hali yako ya kawaida

Raymond: mama yako au mama yangu

Angelina: mama yako

Raymond: eti eeh… (Anamuangalia usoni) yaani wewe mrembo

Angelina :( anaona aibu)

Raymond: nataka nikakununulie gauni moja matata kwa ajili ya harusi ya Edmond na Catherine

Angelina: Asante, nitafurahi sana

Raymond: eti ee (anambusu ishara ya upendo wake kwa Angelina)

(Wanaonekana wapo kwenye mahaba mazito Sana)

Post a Comment

0 Comments