IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 52

 


SCENE 52: -

(Jioni nyingine tulivu na njema jua linaanza kuzama, Christina yupo nyuma ya nyumba yao ameweka kiti na anaonekana ni mtu anayehitaji utulivu maana amekaa kipweke sana, anasoma kitu Fulani kwenye simu yake)

Christina: mambo ni mengi sana kwenye hii dunia... (anashusha pumzi) kila mtu ana mtu wake kasoro mimi…(anasikitika)Peter simuelewi, nimeshaamua kuachana na Raymond lakini pia hata baba yake Raymond nimeamua kumuacha watu na familia zao…tusije tukajikuta sisi ndo tunaoharibu nyumba za watu acha tu nitulie kwanza ukiwa ni mtu wa kulazimisha vitu huwezi kuwa na Amani

(Sauti nzito ya kiume inatokea nyuma yake)

Sauti: mambo...Nimekutafuta sana

Christina :( anageuka) wow (anafurahi Sana) Peter…

Peter :( anatabasamu) Tina… (Anamuendea na kumkumbatia)

Christina :( anamkumbatia pia) umekuja?

Peter :( anavuta kiti anakaa) unadhani nisingekuja? Tina umenifukuza mara nyingi sana ila siwezi kuondoka na kuenda mbali mpenzi wangu nakupenda sana

Christina :( anatabasamu) mbona mara ya mwisho uliniambia kuwa hunitaki tena?

Peter: ah…niliona tu umemkazania Sana Raymond

Christina: nini kimekurudisha?

Peter: siwezi kuishi bila wewe Christina sijui umenipa nini nashindwa kabisa kuishi bila wewe…nipo tayari kuwa hata spea tairi kwako ilimradi tu usikae mbali na mimi

Christina :( anacheka kisha anaguna) eti spea tairi…una vituko wewe

Peter: vituko tena mwenzio nateseka wewe unaniambia nina vituko?

Christina: Peter nakupenda pia tena sana mpenzi wangu…Ni kweli nilikuwa namkomalia sana Raymond ni kwasababu kwanza alikuwa mchumba wangu wewe si umenikuta na Raymond

Peter: ndio

Christina: lakini pili niliona Raymond ni wangu tu yaani hata kama simpendi kimapenzi atabaki kuwa wangu maana nina mamlaka juu yake…(anasikitika)nilikosea sana kama shangazi alivyosema kuwa Raymond ni wa Angelina, na Bembele ni wa Glory na Peter ni wa Christina

(Wanacheka)

Christina: mapenzi hayalazimishwi halafu mtu akishapenda haijalishi kapenda nani kilema, maskini au tajiri kitu upendo kinabaki kuwa upendo tu...kwa mfano Raymond si alikuwa mchumba wangu tumekaa kwenye mahusiano kwa muda ila tukawa hatupendani kuna kipindi mimi nikakutana na wewe nikawa nalazimisha niendelee kumpenda Raymond

Peter :( anamsikiliza kwa makini sana)

Christina: hata ningefanyaje nisingeishia na Raymond maana mimi sikuwa nampenda napenda tu mali zake na jina lake hapa mjini lakini pia hata yeye njiani akakutana na Angelina akampenda tena akampenda sana kuliko hata alivyowahi kunipenda mimi, baba yake akapinga sana lakini wapi, mimi mwenyewe nikapinga sana kwa kujaribu kuyaharibu mapenzi yao yaani mpaka nilimroga Raymond kwa kujaribu kurudisha akili yake nyuma lakini wapi

Peter: aisee

Christina: kwahiyo mapenzi bwana…sijui nisemeje

Peter: nakuelewa sana mpenzi

Christina :( anavuta pumzi kama mtu aliyechoka sana) nakupenda sana Peter wewe ni wa kwangu

Peter: hautarudi kwa Raymond

Christina: hapana…tumeshaachana nimegundua kuwa wewe ni wangu na Raymond ni wa Angelina

Peter:(anatoa kitu Fulani mfukoni)

Christina:(anatabasamu) nini Peter?

Peter:(anapiga goti moja)

Christina: sikuelewi unajua?

Peter: siwezi kuishi bila wewe Christina...miaka mitatu iliyopita pamoja na kwamba nilijua wewe ni mpenzi wa mtu mwingine nilikupenda hivyo hivyo

Christina:(anatabasamu) jamani maajabu haya

Peter: nilikusubiri ugeuze moyo wako na uwe kwangu…nilitembea na pete hii mara zote mara baada ya kukupenda kwa dhati …sina mali ila ninakuhakikishia nitakutunza Christina kama mke wangu na mama wa watoto wangu

Christina: Oh My God!!!(anataka kulia)

Peter: nitajitahidi niendane na maisha uliyoyazoea…nitakuwa mume mwema hata wewe utaona…

Christina: nakupenda sana Peter (Analia)

Peter: Christina mpenzi…Will You Marry Me?

Christina: yes…

Peter:(anamvalisha pete ya uchumba kisha anamkumbatia) …asante sana mpenzi kwa kunikubali…asante pia kwa kutambua thamani ya upendo kwamba mapenzi hayalazimishwi na wala mapenzi hayabagui…karibu katika ulimwengu wangu Christina

Christina:(anambusu) asante baby

(Shangazi, mama na baba yake Christina wanachungulia tukio lote kupitia dirisha kubwa linalotazamana na walipo Christina na mchumba wake mpya)

Mama:(anacheka) sasa mwanangu amekuwa… (anacheka tena) kama filamu eeh kamkomalia Raymond kwa muda kweli…mwisho wa siku yeye mwenyewe kaona ujinga

Baba: hamna lolote nyinyi ndo mlikuwa mnapa bichwa

Shangazi: yeye mwenyewe ndo alikuwa anatupa bichwa

(wanacheka)

Mama: kiukweli yeye na Peter wanaendana ingawa alikuwa anaendana na Raymond pia ila

Baba: ila nini mbona hueleweki?

Mama: Raymond na Christina wameachana kimzaha

Shangazi: wale ilikuwa imeandikwa tu ni lazima waachane ...ila (anaguna)mtoto kajua kumpambania mwanaume ambae hata alikuwa hampendi

Mama: yaani…(anacheka)yaani ukimkuta alivyoshupaa utasema anampenda kuliko anavyompenda huyu...

Baba: kwahiyo mnamsema vibaya Raymond

Shangazi: wala hatumsemi vibaya kaka wa watu nay eye ni maisha tu...ni mapenzi tu

Baba: uzuri wake yeye alijiengua mapema alipojua tu kuwa kamuangukia msichana wake wa kazi akaona aseme tu mapema ila mwenzenu huyo (anamnyooshea kidole Christina) alikuwa anataka kote...

Shangazi: ingemgharimu na bora tu alivyojifanya mjinga ona sasa hivi anavyofurahi

Baba :( anatabasamu) hivi Raymond anamuoa lini huyo hausigeli?

Mama: wewe nae hiyo ni kazi ya kina Bembele huko wewe subiri mahari ya mwanao

Shangazi: umeona eeh…(anacheka)nani alijua kama siku moja sisi na kina Bembele tutakuwa tunapanga mipango ya harusi kwa pamoja? ila sasa sio kwamba watoto wetu wanaoana ni kwamba watoto wetu wanaoa na kuolewa na watu wengune kwa wakati mmoja

Mama :( kwa shangazi) wifi umejuaje kuwa Peter anamuoa Christina hivi karibuni

Baba: si ametuambia…

Shangazi: yeye ndo aliyenishawishi kumwambia Christina aachane na Raymond sio wake…yeye ndo aliyehakikisha Christina anajitambua…na kuacha utoto

Mama: Kumbe…

Shangazi: ndo hivyo na yote hiyo ni kusema kuwa anataka amuoe atulie

 Baba: Safi Sana

(Wanarudi sebuleni na kuendelea kufanya mambo yao)

Peter: I love you so much

Christina: nakupenda pia kipenzi cha moyo wangu

 (Wanakumbatiana)

Post a Comment

0 Comments