IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 50

 


SCENE 50: -

(Asubuhi ya kesho yake Raymond anafika ofisini kwake akiwa na furaha kupita kiasi)

Raymond: Rachel, Pendo…mambo zenu

(Rachel na Pendo wanashangaa)

Rachel: kwani mwenzetu vipi?

Raymond: kwani vipi?

Pendo: mkurugenzi uko sawa?

Raymond: kabisaaaaa…

Glory:(anakuja akitokea ofisini kwa Raymond) bosi…

Raymond: umeanza...

Glory: haya mwanangu…za siku?

Raymond: siku gani? Oh, sawa nilikuwa likizo…Angelina kaniambia

Rachel: mwenzangu mbona hatukuelewi…mara ya mwisho umeondoka hapa ulikuwa hata hutukumbuki can you imagine mpaka mlango wa kutokea ulikuwa umeusahau...Yaani unatushangaa...Tunakuambia wewe ni dokta unakataa unasema kuwa bado unasoma yaani ulikuwa kama umepoteza kumbukumbu

Raymond: yaani hata siwaelewi kabisa mnajua anayway nipokeeni basi

Pendo: hujaja na zawadi, tutakupokea nini sasa?

Raymond: nimetoka likizo, nipokeeni hata begi jamani

(Glory, Pendo na Rachel wanaangaliana)

Pendo: wewe bwana sisi hatukuelewi…umeondoka hapa umetusahau unatuuliza kabisa kwani nyinyi ni kina nani?

Glory:au mwanangu ulikuwa unatudeshi

Raymond: Mimi sijui… (Anaelekea ofisini kwake) nileteeni chai

Glory: sawa mwanangu (anaelekea jikoni)

Raymond :( anaingia ofisini) oh it’s good to be back… (anajitupa kwenye sofa) ngoja nimpigie Edmond(anapiga)

(Simu inaita)

Edmond: Mond…

Raymond: mambo Mond?

Edmond: poa…

Raymond: yaani nimekumisi wewe jamani… (Anaguna)

Edmond: jamani wewe nae si tumeonana juzi tu hapo?

Raymond: Mimi na wewe?

Edmond: ndio

Raymond: yaani hapa nilipo siwaelewi kabisa…kila mtu ananichanganya...Anyway mi nimekupigia simu kale ka inshu vipi brother?

Edmond: kapi?

Raymond: kupeleka mahari kwa kina Angelina bila yeye kujua

Edmond :( anacheka kidogo kisha anaguna) si umeshamwambia

Raymond: wewe…sijathubutu kumwambia

Edmond: Raymond unajua sikuelewi?

Raymond: hata mimi sikuelewi...

Edmond: mimi nani?

Raymond:si Edmond

Edmond: nini kipo mbele yangu?

Raymond: harusi yako wewe na Catherine

Edmond: kabla ya?

Raymond: harusi yangu na Angelina

Edmond: Angelina ni nani?

Raymond: kipenzi cha moyo wangu na pia ni mchumba wangu natarajia kumuoa mama na baba tayari wamesharidhia

Edmond: ulikutana nae wapi?

Raymond: kwangu…ulimleta Kama mfanya kazi wa ndani mimi nikampenda nakuanza nae mahusiano

Edmond: Kama wiki moja na nusu ulikuwa nae wapi?

Raymond: Serengeti

Edmond: baada ya hapo

Raymond: sijui

Edmond :( anajisemea moyoni) amekumbuka basi akili yake iko sawa sasa hivi

Raymond; kwani vipi? Mbona unanihoji maswali Kama unataka kunipa kazi au shemeji ndo kakwambia tukitaka kuoa kwao lazima tupigwe maswali?

Edmond :( anacheka kidogo) hapana unajua Kama wiki na nusu ulikuwa hata hauko vizuri ulikuwa kama umepoteza kumbukumbu kama vile akili yako imerudi nyuma miaka miwili

Raymond: unaniambia kweli au unanitania

Edmond: kweli…

Raymond :( anaguna) nilikuwa namtesa Angelina?

Edmond: cha kushangaza hapana hata hukumtesa na Zaidi tu ulimpenda tu yaani mpaka tukawa tunashangaa

Raymond :( anatabasamu) Edmond sijawahi kupenda mwanamke Kama navyompenda Angelina, yaani dah!!

Edmond: hiyo imejidhihirisha Kwa hizi siku kadhaa ulizokuwa umepoteza kumbukumbu…aliyekutengeneza alijua utarudi miaka miwili nyuma na kurudisha mapenzi yako

Raymond: wewe unahisi ni nani? Mimi nahisi ni Christina…ingawa sina uhakika sana

Edmond: wote hatuna uhakika

Raymond: nimewatesa ee

Edmond: kiasi maana msala wenyewe hata sio wa siku nyingi…sana kwahiyo poa tu…anyway welcome back brother

Raymond: thank you ingawa mwenzenu sikuwa hata na wazo

Edmond: nguvu za Giza hizo…

Raymond: sasa mama si atakuwa alikuwa anahangaika Sana

Edmond :( anaguna) sijajua ingawa Nina uhakika lazima atakuwa alikuwa anahangaika ndio ukizingatia wewe ni mwanae wa pekee lazima ahangaike

Raymond: Angelina je?

Edmond :( anacheka kidogo) yaani wewe na Angelina tu…alikonda

Raymond: ananipenda ee (anatabasamu)

Edmond: anakupenda ndio

Raymond: nafurahi Sana…poa tuonane jioni tuweke mipango vizuri ya harusi yenu au sio

Edmond: poa mwanangu…Asante umerudi mwana…

Raymond: usijali pamoja Sana

(Wanakata simu)

Glory :( anaingia ofisi akiwa amebeba kikombe cha chai na chupa ya chai)

Raymond: we nae mi mpaka njaa imeisha loh…ulikuwa unanunua? Au ulikuwa unachemshia mshumaa…khaa

Glory :( anacheka) hamna bwana mambo mengi huko jikoni acha tu mwanagu

Raymond: haya mimina mambo hayo

(Anammiminia chai kwenye kikombe, anamkaribisha kisha anatoka, Raymond anaendelea kunywa chai huku anaangalia mwenendo wa kazi ulivyokuwa siku zote ambapo hakuwepo)

Post a Comment

0 Comments