IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 2

 


SCENE 2: -

( Asubuhi nyingine tena tulivu jua kwa mbali jua limeanza kuchomoza kila mtu maeneo yale anaonekana anafanya mambo yake na hakuna hata mmoja mwenye muda na mwenzie,Raymond na rafiki yake wa karibu wanaingia katika mjengo mmoja wa kifahari naposema wa kifahari niamini ni wa kifahari kweli,geti tu ni la kufunga na kufungua kwa rimoti,mara baada ya kuingia kwenye mjengo huo wa kifahari ambao kwa sasa ni mali halali ya Mr.Raymond Bembele…mtoto wa kwanza na wa mwisho wa tajiri Bembele na mkewe.Raymond na rafiki yake wanashuka kwenye gari ambalo pia ni zawadi ya Raymond kutoka kwa wazazi wake)

Edmond :( rafiki kipenzi wa Raymond) eh! Bwana dah!!Bonge la mjengo...dah! Mond...

Raymond :( huku anacheka) nambie Mond...

Edmond: huu mjengo mwanangu bonge la kitu haki ya Mungu tena sikudanganyi, hii nyumba mwanangu ni fireeeee

Raymond :( anatabasamu) au sio… (Anacheka tena)

Edmond: ndo maana yake…dah!!Mpaka nakutamania mwanangu dah!!Yaani na mimi ningekuwa na wazazi dah!!

Raymond: usiseme hivyo Mond kazi ya Mungu haina makosa yeye akipanga hakuna wa kupangua cha msingi ni kuwaombea tu wazazi waendelee kupumzika kwa amani

Edmond: ofcourse, sema nini Mond…wewe ni Zaidi ya ndugu yangu mwanangu mi nilijua kuwa ukishapanda cheo na mimi utanisahau na uwalimu wangu lakini dah!!Umenikumbuka my brother hata kwenye sherehe yako nilikuwepo…dah na leo umekuja kufungua nyumba yako kwa mara ya kwanza umeniita kweli wewe ni Zaidi ya ndugu

Raymond: usijali Mond…tupo pamoja msela wangu...na tutazidi kuwa pamoja

Edmond: Asante Sana rafiki yangu (anaendelea kushangaa jumba lile la kifahari)

Raymond :( anamshika begani) poa tuingie ndani

Edmond: dah!!Huko ndani sipapatii picha mwanangu

Raymond :( anacheka) ndo ngoja tupacheki maana hata Mimi sijapaona mwanangu (anafungua mlango)

(Kwa pamoja wanaingia ndani)

Edmond: Oh My God!!...hii ni nyumba au paradise niambie tu mapema matendo yangu mazuri yamenileta hapa...aisee nimefika mbinguni mwenzenu

Raymond: acha zako Mond…hapa sio mbinguni ni nyumbani kwangu…ghetto langu

Edmond: getto???!!!Hili mbona jumba hili mwenzangu...

Raymond; mi bado bachela…sina mke

Edmond: utakuwa nae hivi karibuni mzee wako Jana katutangazia kuwa utakuwa mume wa mtu baada ya miezi kadhaa…najua umefurahi sana maana sio kwa kumpenda Christina huko (anamuangalia usoni) si umefurahi eeh!!!

Raymond: Edmond we ni mshikaji wangu wa miaka na wewe unaelewa fika kuwa mimi sitaki kuoa sasa hivi na unaelewa kabisa jamu zangu na huyu demu leo hii unaniuliza kama nina furaha ya kuwa mume wa Christina, kweli hilo swali unaliona liko sawa kweli?

Edmond: nisamehe Raymond mi nilikuwa nakutania tu mtu wangu nisamehe Sana kaka yaishe

Raymond: usijali my brother Mimi na wewe hatuwezi kuzinguana

Edmond: ndo maana yake ila embu nambie kitu hapa nielewe kwanini usimsamehe tu Christina na umuoe tu...

Raymond; kumsamehe nilishamsamehe lakini sioni kama anaweza kuwa mke wangu ni kweli nilikuwa nampenda lakini kwa kitendo alichonifanyia…mimi nilimheshimu ila yeye akanifanyia vile alivyofanya na hapo ni mpenzi akiwa mchumba je au mke si ataniua…christina sio mwanamke nayemtaka yaani she is not for me kabisa tutapotezeana muda tu ila ukweli ni kwamba kama mama alivyosema kwa kuwa dad…ndo kaamua basi ni kuwa mpole tu sina jinsi

Edmond :( anaguna) ila mwanamke mshenzi

Raymond: sio kidogo nakwambia

Edmond :( anabadilisha mada) nionyeshe vyumba…

Raymond:(anacheka) umeanza… (anacheka tena) mimi mwenyewe sipajui kabisa hapa nababia tu (anafungua chumba kimoja) wow...

Edmond: chumba chumba jamani chumba kweli ndugu yangu

Raymond: hiki sijui ni chumba changu

Edmond: embu endelea kufunga na kufungua vyumba tutakipata tu cha kwako

Raymond :( anaendelea kufungua na kufunga vyumba na hatimaye anakipata chumba chake) wow…sasa hiki ndo chumba changu…Mond cheki kitanda hicho

Edmond: mdogo wangu oa baba hichi kitanda utakuwa unalala peke yako? Oa haraka Sana

Raymond: huyo mwanamke wa kuoa sasa bado sijamuona kabisa hata nisemeje sijampata kabisa

Edmond :( anacheka Sana) yaani wewe huna aibu kabisa yaani wazazi wako wamekuchagulia mke unakataa sasa utakaa Na nani kwenye jumba lote hili?

Raymond: hata na wewe unaonaje hiyo

Edmond: Mimi natarajia kuoa hapa nakusanya tu mahari tu…

Raymond: nitakusaidia kaka yangu we siku ukitaka kwenda Kwa kina Catherine basi niambie nitakuwa hapa kuusaidia my brother

Edmond: ah…Raymond my brother ushanisaidia Sana tu acha hili nikomae nalo kibishi tu mtu wangu

Raymond: let me help you my friend (anamshika bega ishara ya kumsihi Sana)

Edmond: sina ubishi sawa…haina shida nisaidie tu ila unanilemaza

Raymond: utakoma (anacheka)

(Mlango unagongwa)

Raymond: pita mlango uko wazi

Edmond: utakaribisha na majambazi my brother

Raymond: majambazi asubuhi yote hii?

(Kuna mtu anaingia ndani kwakuwa hawamfahamu wanamuangalia tu)

Mtu: habari zenu jamani

Kwa pamoja: salama...

Mtu: Mimi ninaitwa Ramadhani nimeagizwa hapa na Mr. Bembele

Raymond: sawa huyo ni baba yangu, ndio amekuagiza nini?

Ramadhani: Mimi ndio mlinzi wako na mali zako zote humu ndani, ila mimi nitakuwa nakaa pale getini

Raymond: oh…karibu sana kaka Ramadhani…mimi naitwa Dk. Raymond Bembele ni mtoto wa pekee wa bwana na bibi Bembele nashukuru sana kwa ujio wako maana nilikuwa nawaza sana ningepata wapi mlinzi sasa hivi ila kweli Mungu anaishi na amenisaidia kwahiyo karibu sana (anamgeukia Edmond) huyu ni rafiki yangu kipenzi yaani keshakuwa kama ndugu, anaitwa Edmond...

Ramadhani: eeh!!Raymond, Edmond…hizo Mond mwishoni mmezigundua? Au hamjazindua?

Edmond: zamani Sana

(Wanacheka)

Raymond: aisee karibu Sana Mr. Ramadhani

Ramadhani: asanteni Sana kina Mond (anacheka KISHA anaondoka)

Edmond: mshikaji anaonekana yuko vizuri Sana, mcheshi, nimemfurahia…ukiwa mpweke nenda getini ukachekeshwe

Raymond: umeona eeh…yaani napenda watu wa hivi nafurahi sana kukaa nao

Edmond :( anabadilisha mada) aisee Nina njaa kweli hakuna jiko

Raymond: we mwehu kweli yaani ushawahi kuona nyumba haina jiko sema hakuna chakula Kama una njaa Nina njaa Zaidi yako mtu wangu cha kufanya tukale nje mtaani huko maana hapa Mimi hiyo nguvu ya kuingia jikoni mara sokoni kwasasa sina kabisa, kwahiyo twende zetu magengeni

Edmond: poa mi nakusikiliza wewe boss

Raymond: nishakwambia usiwe unaniita boss sipendi hilo jina kweli yaani

Edmond: nisamehe mdogo wangu sikuiti tena (anamkumbatia)

Raymond :( anamsukuma) embu twende huko

Edmond :( anamuachia) haya twende

(Wanaondoka kuelekea nje wanapanda gari na kuondoka zao)

Post a Comment

0 Comments