IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 3

 


SCENE 3: -

(Asubuhi ya siku ya pili yake ambao pia ni asubuhi ya kwanza ya Raymond nyumbani kwake mara baada ya kukabidhiwa nyumba na wazazi wake. Raymond kalala fofofo huku simu yake ya mkononi aina ya iphone 13 pro max ikiwa inaita mfululuzo bila kupokelewa, inaita sana kitendo kinachomfanya Raymond kushtuka kutoka usingizini, anaitazama simu yake na anagundua kuwa imeita sana na simu zote zimetoka kwa baba yake)

Raymond; oh My God…missed calls ishirini na tano? (Anashangaa Sana) halafu zote za dad…Mungu wangu, ngoja nimpigie (anapiga)

(Simu inaita)

Mr. Bembele: (anapokea) wewe mtoto wa Gloria unalala sana baba, kwanini lakini?

Raymond: iam sorry dad…

Mr. Bembele: nakupa dakika 10 uwe umefika ofisini wafanyakazi wako wanakusubiri boss wao ufike haufiki naomba uvae haraka uje nakusubiri

Raymond:(huku anashuka kitandani) ok dad… (anaingia bafuni anaoga haraka kuliko kawaida baada ya muda anatoka haraka anavaa nguo zake za ofisini KISHA anachukua ufunguo wa gari anatoka nje, anapanda gari lake na kuliondoka kwa mwendo wa kasi sana, baada ya kama dakika kumi na tano anafika ofisini kwake ambapo kwa sasa yeye ndo bosi)

Mr. Bembele :( anamuona kwa mbali, anawageukia wafanya kazi ambao walikuwa wamesimama wakimsubiri kwa hamu boss huyo mpya) jamani anakuja

Raymond :( anaingia ofisini)

Wafanyakazi :( wanamwagia Maua wenye kumtupia Maputo nao wapo) welcome boss…

Raymond :( anatabasamu) jamani asanteni Sana jamani

Mr. Bembele: karibu Sana…boss

Raymond: Asante…

Mwanamke 1 :( Kwa sauti ya chini) dah!!!Boss handsome huyu jamani

Mwanamke 2: yaani acha tu da. Pendo…yaani mwanamume mzuri huyu cheki tabasamu duh...

Pendo: wewe Rachel naomba umheshimu huyu ni shemeji yako

Rachel ;( anacheka) yamekuwa hayo?

Pendo: twende tukamshike hata mkono mwenzangu

Raymond :( anatabasamu huku anaendelea kushika watu wote mikono) asanteni jamani

Pendo: jamani kaka umependeza

Raymond: Asante dada

Mr. Bembele :( anamshika mwanae mkono) boss…naomba sasa uje ofisini kwako tumalize hili zoezi

Raymond: ok dad…

(Mr. Bembele na mwanae wanaelekea ofisi iliyokuwa imewekwa kwa ajili ya Raymond, wanapofika ofisini humo Raymond anavutiwa sana na uzuri wa ofisi ile)

Raymond: wow dad, this ofisi is so beautiful

Mr. Bembele: ya kwako mwanangu nimeiweka kwa ajili yako…wewe ndo boss from now on wards mpaka uzeeke na nina Imani utaipeleka mbele hospitali yetu mwanangu

Raymond: haswa…

Mr. Bembele :( anamuwashia runinga kubwa iliyokuwa imebandikwa ukutani mara baada ya kufanya hivyo anamuwashia laptop KISHA anamvutia kiti) tafadhali keti boss…nakukabidhi rasmi ofisi yako

Raymond: oh...Dad…Asante Sana mzee wangu

Mr. Bembele: usijali mwanangu...Please enjoy sasa acha Mimi niende…nikapumzike nyumbani

Raymond: ok dad…Asante dad, ofisi nzuri Sana…nimependa samani zote zilizopo humu ni nzuri sana

Mr. Bembele: usijali tupo pamoja mwanangu (anatoka na kwenda zake nyumbani)

Raymond; oh…my God…am I in heaven? mbona ofisi nzuri hivi? (anatabasamu mwenyewe) nakushukuru Mungu wangu kwa Baraka hii ya wazazi wanaonipenda kiasi hiki…ingawa huwa tunagombana gombana sana na dad…hiyo ni kawaida maana hakuna aliye mkamilifu ila wewe tu Mungu wangu…asante sana (anachukua simu yake anampigia Edmond)

(Simu inaita mwisho inapokelewa)

Raymond: Yes, Mond...Guess what?

Edmond: what?

Raymond: nipo kwenye ofisi yangu mpya rafiki yangu nakula kiyoyozi tu…

Edmond; wacha we…kula bata baba mpaka kuku waone wivu

Raymond :( anacheka Sana) yaani acha tu, sifa na utukufu tumrudishie yeye aliyeziumba mbingu na dunia na Zaidi alinipa wazazi wanaonipenda kama hawa

Edmond: haswaaaa….

Raymond: ngoja nikutumie whatsApp picha ya ofisi yangu mpya upaone

Edmond: poa Mond

Raymond :( anajipiga picha anapiga ofisi yake KISHA anamtumia picha rafiki yake) nishakutumia Mond

Edmond: poa… (Anaingia whatsApp anaangalia KISHA anampigia simu tena)

Raymond: nambie

Edmond: mwanangu bonge la ofisi duh…

Raymond; kidogo Sana tu…

Edmond: kidogo hiyo, ukubwa Kama chumba na sebule yangu

Raymond: umeanza Mond si unajua huwa sipendi unavyoyaangea hayo maneno usiwe unasema hivyo

Edmond: hiyo ndo reality ya maisha yangu, ila poa basi haina noma wangu tuyaache hayo

Raymond; poa

Edmond: poa ngoja naingia kipindi sasa hivi kwahiyo nazima simu tuonane baadae Kama kwenye saa kumi na moja hivi tubadilishane mawazo, mdogo wangu

Raymond: hamna noma kaka yangu ngoja nianze majukumu ya siku huku

Edmond: poapoa

Raymond :( anakata simu) Ah…Nina Amani Sana jamani sasa nina kazi ya kutafuta true love Christina sio true love wangu (simu yake inaita haraka anapokea) nambie

Sauti: poa…honey hujanimisi.

Raymond: dah!! Christina nipo ofisini hapa nina kazi sana mtu wangu…ungeniacha kidogo tutaongea badae

Christina: yaani siku hizi sikuelewi kabisa my love yaani tangu siku ile imetangazwa kuwa tutafunga ndoa baada ya miezi miwili nakuona kabisa huna raha na mimi kabisa kwanini?

Raymond: huo ni wasiwasi wako tu Tina mi mbona sina chochote anyway Kama nilivyokuambia nina kazi tafadhali tuonane baadae kidogo

Christina: ila tambua kuwa ninakupenda sana mchumba wangu na ninamuomba Mungu atufikishe tunapopataka

Raymond; poa (Anakata simu) yaani huyu mwanamke yaani hana kabisa sifa za kuwa mke wangu ingawa nimekaa nae huu mwaka wa sita ila nafsi yangu tu haimkubali tena mara baada ya kujua kuwa ni mzinzi na msaliti ndo kabisa sitaki hata kumsikia ila sasa unadhani nitafanyaje ndo tayari baba keshamchagua inabidi tu niwe mpole nitulize tu kipapa (anasogeza laptop yake karibu anaanza kufanya kazi) Mungu tu anaisaidie

Sekretari (anabisha hodi) habari za kazi boss, Mimi naitwa Glory ni sekretari wako samahani sikuwepo kukupokea maana kuna sehemu nilikuwa nafanya kazi

Raymond: usijali Glory wajina wa mama yangu…tupo pamoja mi naitwa Raymond Bembele

Glory: nashukuru kukufahamu boss (anacheka kidogo) sawa boss karibu sana ofisini kwetu

Raymond :( anaachia tabasamu zuri) Asante mami

Glory :( anatoka huku akimuacha Raymond anaendeleea na kazi zake)

Raymond :( anaonekana ni mtu mwenye furaha kila mara anaiangalia ofisi yake na anaifurahia sana)

Post a Comment

1 Comments