SCENE 5: -
IJUMAA: -
(watu wamekaa mahakamani kwaajili ya kuanza
kusikiliza kesi inayomkabili Liliana, mtuhumiwa anawasili akiwa na mapolisi na
msoma mashtaka nae anawasili, familia ya bwana Robert nayo inawasili kwa ajili
ya kusikiliza mashtaka yanayomkabiri Liliana, baada ya muda kidogo kila mtu
kuingia hatimaye anaingia hakimu na kila mtu ananyanyuka ishara ya heshima kwa hakimu.
hakimu anapofika kwenye kiti chake anawaruhusu watu kuketi nao wanatii)
Hakimu
:(kwa msoma mashtaka) tafadhali
endelea
Msoma
mashtaka :( anainama kuonesha heshima)
Asante mtukufu hakimu…siku ya jumanne tulikutana hapa kusikiliza mashtaka
yanayomkabili bibi Liliana Kadoke mkazi wa Mpanda mkoa wa Katavi…tulisikiliza
kidogo baade akawa ameugua kidogo na mahakama ikawa imeamua tusikilize tena leo
ijumaa baada ya bibi Liliana kupata afadhali… (kwa mwanasheria wa upande wa kina Robert na familia) tafadhali
karibu kama una maswali yoyote…
Mwanasheria:
naitwa Bw. Bryson Lameck…ni mwanasheria upande wa washtaki… (anamsogelea Liliana)
habari yako, dada Liliana
Liliana:
salama…
Bryson:
unaendeleaje? Maana ulipata mshtuko kidogo na tukakukimbiza hospitali…vipi hali
yako leo?
Liliana:
naendelea vizuri Sana…asante kwa kuuliza
Bryson:
kwahiyo tunaweza kuendelea?
Liliana:
ndio…tunaweza
Bryson:
sawa (anaenda kuchukua karatasi Fulani
katika dawati alilokuwa amekaa kisha anamrudia Liliana) ah…mara ya mwisho
ulituambia kuwa ulikuwa na mahusiano na marehemu na alikufanyia mambo mabaya
yaliyokusukuma kumuua
Liliana:
ilikuwa ni hasira tu…mheshimiwa
Bryson:
tunaomba tusikie labda na sisi tutaelewa hiyo hasira…maana kwa sasa hatuelewi
kabisa hiyo hasira iliyokufanya kumuua Bw. Robert na kuchoma nyumba yake….
Liliana:ni
hadithi ndefu sana
Bryson:
tunataka kuisikia
(Familia ya Bw. Robert nao wapo
hapo wakisikiliza Kwa umakini yote yanayoendelea hapo)
Liliana:
labda nianze Kwa kuhadithia maisha yangu Kwa ujumla ili ilete maana kama
nitaruhusiwa
Hakimu:
unaruhusiwa…
Liliana:
asante mtukufu (anainama kidogo kisha anainua kichwa) mimi naitwa Liliana
nilikuwa ni mtoto wa pekee wa Mr. Peter na Mrs.Paulina Lukupe…wazazi wangu
walikufa kwenye ajali mbaya na kuniacha chini ya uangalizi wa shangazi na
mjomba wangu… (anainama na kuanza kulia)
Bryson:
jikaze…
FLASHBACK: -
(Usiku mtulivu, kaupepo mwanana
kanavuma na kila kitu kinaonekana kipo sawa, Mr. Peter yupo pamoja na mke na
mwanae wa kike, wanasafiri maana wapo kwenye gari wanaongea na wanaonekana
wanaifurahia sana safari hiyo)
Peter:
vipi mbona mmenyamaza si muongee jamani au mnasinzia?
Paulina
:( mke wa Peter) hatulali…basi tu
hatuna cha kuongea…ndo maana tupo kimya…
Peter:
pigeni tu hadithi zozote hata za chui na simba
Paulina
:( anacheka) yaani wewe kwani Mimi
nimekuwa Liliana
Liliana
:( mtoto wa miaka kati ya sita na saba)
Peter
:( kwa Liliana) eti mama na wewe huna
cha kusema?
Liliana
:( anatabasamu)
Peter:
sawa ila mimi nina cha kukuambia nisikilize…
Liliana
:( anaonyesha umakini kwenye kumsikiliza)
Peter:
nakupenda sana mwanangu mzuri…sana…wewe ni malkia wangu…nakuombea maisha marefu
sana…mwanangu…na mimi Mungu anijalie maisha marefu sana…ili nije niwaone watoto
wako na wajukuu
Liliana
:( anatababasamu)
Paulina:
hata Mimi nakupenda Sana mama yangu…
Liliana
:( anatabasamu)
Peter
:( anamuangalia mwanae)
(Mara ghafla linakuja Lori
linagonga USO Kwa uso na gari waliokuwepo Peter na familia yake)
Paulina:
mwanangu (anamrushia Liliana nje kupitia
dirishani)
Liliana:
mamaaaaaaa
Peter
:( anahangaika kuokoa maisha ila
anashindwa na hatimaye gari linapinduka na kulipuka)
Liliana:
babaaaaaaa, maaamaaaaaa (Analia Sana)
(Watu waliokuwa maeneo hayo
wanakuja huku wanakimbia)
Mmoja
ya watu: dah…ajali mbaya Sana yaani aisee…sijui kama kuna mtu amepona…
Liliana
:( Analia)
Mwanamke
1: eh…kuna mtoto hapa…(anambeba)wewe
umetokea wapi?
Liliana:
mama Na baba yangu wamekufa…kwenye ajali
Mwanamke
2: dah…aisee pole sana, ngoja tuite polisi ili kwanza huyu mtoto apelekwe
hospitali halafu baadae wampeleke nyumbani (anapiga
simu polisi simu inaita mwisho inapokelewa) hello…. Mi ni raia mwema kuna
ajali imetokea mbaya sana hapa katikati ya Tabora na singida…
Polisi:
Asante Kwa taarifa tutawafikia hapo…
Mwanamke
2: Asante… (Anakata simu) polisi
wanakuja baada ya muda tukae tusubiri kidogo…
Mwanamume
1: dah…pole Sana mtoto…kwenu wapi.
Liliana
:( huku Analia) Mpanda…
Mwanamke
1: na ndugu zako je wako wapi?
Liliana:
shangazi yupo Tabora…
Mwanamke
2: pole Sana Mungu akutete katika maisha yako ya uyatima
Mwanamke
1: pole
Liliana:
Asante…
(Baada ya muda Fulani polisi
wanafika)
Polisi
1 :( anawakaribia watu) habari zenu
jamani
Wote
:( wanaitikia) salama
Polisi:
tumepata taarifa kuwa kuna ajali imetokea na imeua watu
Wote:
ndio…
Polisi
1: imegongana nini na nini?
Mwanamke
2: imegongana Lori na gari ndogo (ananyooshea
Kwa kidole) gari lenyewe lile pale limeungua na sidhani kama watu wamebaki…
(Mapolisi
wanaendea gari na kujaribu kuangalia na wanagundua kweli watu wamebaki majivu
tu)
Polisi2:
aisee hii ajali ni mbaya sana yaani hata miili yao haikuonekana kabisa
Polisi
1 :( anamuangalia Liliana) Na huyu mtoto
ni nani?
Mwanamke
1: ndo mtoto wa marehemu hao…amenusurika
Polisi
1: pole Sana…tutakufanyia mpango ufike Kwa ndugu zako, si unapajua nyumbani?
Liliana:
ndio…
Polisi
2: usijali…tutakufikisha mpaka nyumbani na tutawaita ndugu zako waje wachukue
hili gari… (Kwa mwanamke 2) yaani
hakuna mwili ni majivu tu
Mwanamke
2 :( anasikitika Sana) aisee…
Polisi
2: lakini tutafanya mpango na kila kitu kitakuwa sawa (wanampandisha Liliana kwenye gari na kuondoka nae)
Polisi
1: tunamchukua tunaenda kufanya mpango wa kumfikisha kwa ndugu zake
Watu (wanatawanyika kila mmoja wao anarudi majumbani kwao)

0 Comments