I KILLED MY LOVER 4

 


SCENE 4: -

(Ni asubuhi nyingine ya siku nyingine wiki kadhaa zimepita tangu binti Liliana akamatwe na kuwekwa rumande, anafika mahakamani yeye pamoja na mwanasheria wake pamoja na maaskari waliomshika mmoja mkono wa kulia na mwingine mkono wa kushoto, baada ya kumfikisha kizimbani, anakaa na kusikiliza mashtaka yanayomkabili)

Msoma mashtaka:(kwa hakimu ambae amekaa kimya katika kitu chake) mheshimiwa hakimu, mbele yako ni bibi Liliana Kadoke mkazi wa mpanda na mkoa wa Katavi, anashtakiwa kwa kosa la kumuua Bw. Robert Michael kisha kuchoma nyumba yake mnamo tarehe moja mwezi wa tano...hii imethibitishwa na uchunguzi wa polisi nay eye mwenyewe mshtakiwa kukiri kosa hilo (anakaa kimya)

Hakimu :( kwa mshtakiwa) je umesikia mashtaka yako?

Liliana: ndio…

Hakimu: je unakubaliana nayo au hapana?

Liliana: ndio nakubaliana nayo

(Watu waliopo mahali hapo wakiwemo majirani na familia ya marehemu Robert wanaanza minong’ono ya chini chini)

Hakimu :( anagonga meza kuamuru utulivu) order, order naomba utulivu

(Kuna utulivu wa ghafla)

Hakimu :( Kwa Liliana) unaweza kuiambia mahakama kwanini ulifanya vile…

Liliana: Ni hadithi ndefu sana nyie toeni tu hukumu msiniulize chochote maana ni maelezo marefu sana

Hakimu: tunataka tuyasikie maana hatuwezi kutoa hukumu huku hatujasikia upande wako

Lydia :( yupo kimya wakati wote huo)

Liliana: hapana, mengine ni ya siri sana

Hakimu: ndo tunataka kuyasikia tafadhali toa ushirikiano, kwanza swali ambalo nilitakiwa kukuuliza tangu mwanzo ni kwanini ulimuua Robert Michael?

Liliana: ilikuwa hasira…

Hakimu :( anaandika kitu kwenye karatasi yake)

Liliana:Robert alikuwa ni bwana wangu,alinipenda na kunithamini sana atleast hilo ndo lilikuwa ndo tumaini na mawazo yangu kuwa alinipenda sana,alinipa kila kitu nilichotaka…alinipeleka sehemu mbalimbali nilizotaka (anakumbuka kitu kisha anasikitika sana)kwa kifupi alinipa kila kitu na kuniahidi kuwa atanioa,baadhi ya ndugu zangu walimjua na kumheshimu na kumpenda sana,nilimpenda na  yeye akanionyesha kuwa ananipenda(kimya kidogo huku anakumbuka kitu)…kimbembe kilikuja nilipobeba ujauzito na kwenda kumwambia kuwa nina ujauzito wake alinikataa katakata na kusema hayuko tayari kuipoteza familia yake yaani mke na watoto wake huku ni kwamba wakati tunaanza mahusiano alinihakikishia kuwa hana mke wala watoto na alisema mke na watoto wake walikufa katika ajali

(minong’ono)

Mama Neema: kumbe alikuwa na  yeye ana mapungufu yake loh…

Lydia :( anamuangalia mama Neema bila kusema jambo lolote)

Hakimu :( anagonga meza kuamuru utulivu) endelea…nini kilitokea baada ya hapo…?

Liliana: ilinisumbua sana maana ukiangalia mimi ni yatima sina mama wala baba…yaani nipo peke yangu katika hii dunia

Hakimu :( anamsikiliza kwa umakini mkubwa sana)

Liliana:basi alipoikataa mimba nikaamua tu niondoke maana tayari nishakataliwa unadhani nitafanya nini tena,nilipoanza kliniki ya mama wajawazito nilijigundua kuwa nina maambukizi ya virusi vya  UKIMWI,nikaja kumwambia basi angalau anilee mimi(anaanza kulia)na mtoto sitamuingilia katika maisha yake na  familia yake….alinijibu vibaya a kunifukuza kama mbwa…sikuwa na kitu cha kufanya niliondoka na kuanza kufanya kazi nyingi ilimradi nipate kula maana natumia dawa…kila mara nilimpigia simu akawa hapokei hata nikipiga kwenye namba mpya anapokea akisikia sauti yangu haraka anakata simu na ananiambia nisimtafute maana mke na watoto wake wanakaribia kuja,nilichomwambia ni kwamba nahitaji tu msaada na sio vinginevyo,akawa hataki…hiyo ndo sababu ya hasira yangu nikaamua tu nimuue(anafuta machozi)maana ndo niliona ni njia nyepesi ya kupunguza maumivu yangu,tafadhali nimeshawaeleza mengi naomba nikapumzike mnihukumu kifo nife…maaana sina maana tena ya kuishi duniani nimepoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu(Analia)

Hakimu: Hilo litaamuliwa na mahakama hata hivyo hujatueleza maisha yako ya utotoni labda tukisikia tutaelewa kwanini ulipata hasira mbaya na kufikia kumuua mwanaume kikatili vile maana mimi nilivyoambiwa kuwa Robert alikuwa ni baba mwenye nguvu zake na kila mtu alimjua kwa ukakamavu sasa kuja kuuliwa na binti… (Anaguna) hiyo imeshangaza wengi na jinsi kifo kilivyotokea hata polisi walijua kuwa ni mwanaume ndo kaua sasa ulipojitokeza wewe ndo hapo watu wakabaki midomo wazi…labda nini tatizo…

Liliana: halipo tatizo (anaanza kulia tena) nataka tu kufa mheshimiwa (Analia sana) naomba nife

Hakimu: hatuwezi kuhukumu bila kusikia chochote

Liliana:(Analia sana)

Hakimu: ukilia hatutaweza kukusaidia tafadahali elezea kila kitu, tangu ulipokuwa mdogo na kadhalika

Liliana: sipo vizuri…

Lydia :( anamkaribia na kumshika bega) binti

Liliana:(anamgeukia Lydia huku Analia)

Lydia: jikaze na utuelezee

Hakimu: mama, hairuhusiwi kuja hapa labda mpaka uruhusiwe

Lyidia: samahani mheshimiwa...

Hakimu: usijali

Liliana: ninajisikia vibaya Sana

Hakimu: tafadhali mpeni maji ya kunywa…

Liliana :( anasikia kizunguzungu)

Msoma mashtaka :( anampa maji kwenye glasi)

Liliana :( kabla hajayapokea anaanguka chini)

Hakimu: mkimbizeni hospitali

(Haraka polisi na wahusika wengine wanambeba na kumtoa nje kwa ajili ya kumpeleka hospitali)

Hakimu :( anagonga meza) order, order…tutaendelea kipindi kingine…twendeni tukaendele na shughuli zetu tukutane hapa tena ijumaa saa nne kamili asubuhi tuendelee na kesi (anagonga meza kisha ananyanyuka na kuondoka zake)

(Watu huo watu wamesimama Kama ishara ya heshima Kwa hakimu, hakimu anapokuwa ameondoka kabisa kila mmoja wakiwemo familia ya marehemu Robert wanatawanyika, wakati huo watu mbalimbali wanawateta mke na watoto wa Robert)

Gabriel :( anamuendea mmoja wa watetaji) dada…tambua kuwa hakuna mkamilifu Zaidi ya Mungu…hilo kumbuka na utambue

Dada :( kimya huku anaangalia chini Kwa aibu)

Raphael: kaka twende

Lydia: Gabriel…naomba twende mwanangu

Gabriel :( anatangulia nje)

Raphael :( anasikitika Sana)

(Kwa pamoja wanatoka nje na kwenda kwenye gari lao)

Lydia :( huku anakaa kwenye gari) wanangu tulieni mkiendekeza hasira mtagombana na kila mtu…nyie poeni sawa wanangu wazuri

Michael: sawa mama…

Gabriel :( anaanza kuendesha gari)

Lydia:(anawaza moyoni) mume wangu nakupenda sana na ninakukumbuka kila dakika tangu umefariki ila hii ya kutembea na mtoto wa watu na kumuambukiza ugonjwa tuliokuwa nao miaka mingi sio vizuri ona sasa watoto wanashikwa na hasira kutokana na kwamba watu wanawasema vibaya sana kwa kosa dogo sana ulilolifanya wewe kwa tamaa zako…kila mmoja anamuonea huruma yule mtoto wa watu uliyempa mimba na kumterekeza labda ungekubali huyo mtoto pengine mpaka sasa ungekuwepo hai mume wangu

Raphael: Mama mbona uanaonekena na mawazo?

Gabriel: sasa ataacha kuwaza baada ya kusikia mume wake aliharibu maisha ya mtoto wa watu?

Michael: nakubali daddy…alifanya kosa ila the fact kwamba auawe kisa kitu kinachozungumzika Kama hicho?

Gabriel: inategemea dad…alimsukuma vipi mpaka mwisho akaamua kuua…

Raphael: exactly

Lydia: sawa nyamazeni kila kitu tutajua hiyo ijumaa

(Wote wanakaa kimya na kuendelea na safari yao ya kuelekea nyumbani kwao)

Post a Comment

0 Comments