SCENE 6: -
BAADA YA MWEZI MMOJA (BAADA YA MSIBA)
(Ni alfajiri, Liliana amelala katika chumba
chenye mfano wa stoo, maana kuna makorokoro mengi sana, na cha kushangaza
amelazwa chini na ukiangalia hii ni nyumba aliyoachiwa na wazazi wake, wakati
amelala anaingia shangazi yake akiwa amejawa hasira sana)
Shangazi:
we Liliana mbona umelala mpaka sasa hivi na unajua kuwa hatuna mfanyakazi na
wanangu wanahitaji kwenda shuleni
Liliana:(anaamka akiwa anatetemeka) samahani
shangazi na leo nimejisahau kuamka mapema shangazi yangu nisamehe
Shangazi:(anampiga kofi la nguvu) pumbavu!!!!sana
wewe kila siku unakosea ni lini utaelewa kuwa wewe ni mfanyakazi humu ndani na
unatakiwa uwahi asubuhi kupika chai na kuwatayarisha wanangu
Liliana:
lakini shangazi hata mimi ninatakiwa niwe naenda shule
Shangazi:si
unaenda za serikali kwani huendi shule?
Liliana:
lakini baba yangu si aliacha hela ya mimi kusoma?
Shangazi:(anamsukuma kwa nguvu) embu katayarishe Watoto
wenye wazazi wao…wewe si huna mama wala baba?
Liliana:(anaenda huku Analia, anafika jikoni anakaa
na kuanza kukumbuka mapenzi aliyokuwa anaonyeshwa na mama na baba yake,
anajikuta machozi yanamtoka sana)
Shangazi:(anakuja) mbona wewe mtoto ni mvivu sana?
Liliana:(ananyanyuka na kuanza kupika chai kisha
anatenga mezani anawaamsha watoto wa shangazi yake) amkeni mkanywe chai
Bella:(mmoja wa watoto wa shangazi yake) we
mjinga nini…unaingiaje chumbani kwetu bila hodi?
Shangazi:
nenda kamuamshe na mjomba wako anywe chai aende kazini
Liliana:
sawa shangazi… (anagonga mlango) hodi
Mjomba:
karibu
Liliana:(anaingia)
Mjomba:(anajikuta kumtamani hivyo anajikuta analamba
midomo) karibu Lily…(anamvuta)
Liliana:
niache mjomba…
Mjomba:
nitakukamata…tu
Liliana:(anatoka anakimbia)
Shangazi:
umeona nini? Mbona umetoka mbio kama mtu kaona mzimu?
Liliana:
hamna kitu shangazi…
(watoto wa shangazi yake wamekaa
mezani wanakunywa chai huku Liliana anaenda nje kufagia uwanja, ameinama
anafagia huku anaimba nyimbo za huzuni za kuwakumbuka wazazi wake)
Shangazi:(analeta
mabaki walioacha mume na watoto wake) kula chakula hiki na uende shuleni usije
ukasema hatukusomeshi…
Liliana:(anachukua na kuanza kula)
Shangazi:(anarudi kwa wanae) haya fanyeni haraka
niwapeleke shuleni wanangu…
Bella:
mama, mimi huyo Liliana ananiudhi kweli…siku hizi hata hafui nguo zetu
Anna:(anaguna) Bella acha uongo mbona anatufulia?
halafu mama mbona hii ni nyumba yao halafu analala stoo
Shangazi:
kelele mshenzi mkubwa wewe…huna adabu wala shukrani
Anna:
mama Mungu hapendi lakini
Shangazi:
atajua mwenyewe awe anapenda asiwe anapenda atajua mwenyewe…
Anna:(anabaki anatikisa kichwa ishara ya
kusikitika)
Shangazi:
fanyeni haraka… (ananyanyuka na kwenda
nje kwenye gari)
Bella
na Anna:(wanamfuata)
Anna:(kwa Liliana) fanya haraka uende
shule…mdogo wangu…
Shangazi:(kwa ukali) embu panda kwenye gari
Anna:
mama lakini
Shangazi:(anawasha gari kisha analiondoa kwa kasi
sana)
Anna:(anamchungulia Liliana kupitia kioo cha nyuma)
maskini!!! Kwani kosa lake ni nini jamani?
Shangazi:(kwa Anna) naomba ukae vizuri wewe Anna
Bella:
yaani anajifanya kumuonea huruma
Shangazi:
tukimfanya awe mwenye nyumba tutaikosa hii nyumba mwanangu ndo maana tunatakiwa
tumfanye aogope
Anna:
lakini mama hii ni nyumba yao na pia hili ni gari lao, kwani tukikaa nae vizuri
hatutaishi?
Shangazi:
naomba unyamaze we mtoto usie na adabu kwa mama yako…acha tu enjoy muda wetu ndo
huu
Anna:(anaona akae kimya)
(Upande wa Liliana huku amebaki
peke yake na mjomba wake maana bado hajaondoka kwenda kazini)
Mjomba:(anamuendea alipokuwa amekaa anakula mabaki yao)
pole maskini unakula mabaki…
Liliana:(kimya huku anamalizia kula)
Mjomba:
naweza kukufanya kuwa unakula vizuri ukinikubali…niwe mpenzi wako…
Liliana:(anamuangalia) mjomba mimi ni mtoto mdogo
sana na ndo kwanza nipo darasa la tatu mjomba nitakuwaje mpenzi wako?
Mjomba:
unanibishia?
Liliana:
siwezi kuwa mpenzi wako mi bado mdogo sana na pia ni ndugu yako
Mjomba:
poa we jifanye sasa mjeuri utakula jeuri yako na kuanzia sasa hivi utateseke
mpaka uombe kifo…kwani tatizo nini, si nalala na wewe kidogo tu nakuwa nakupa
chakula kizuri
Liliana:
sitaki…mjomba sitaki (anaingia ndani)
Mjomba:(anamuangalia kwa tamaa) mtoto mzuri sana
jamani lazima niwe nae, dada nae alizaa mtoto mzuri jamani mwee
Liliana:(anatoka amevaa sare za shule za shule ya
msingi za serikali amebeba na ufagio wake)
Mjomba:
kwahiyo Lily…unasemaje?
Liliana:
hapana mjomba…
Mjomba:
hautakuwa unafanya kazi nyingi…nikubalie nitamwambia shangazi yako akupunguzie
kazi
Liliana:
nimekataa mjomba kwakweli sitaki tena sitaki kwelikweli huwezi amini na
ukiendelea kuniuliza na kunisumbua nitamwambia shangazi…
Mjomba:
unadhani atakuamini? (anacheka kwa kejeli)
hawezi kukuamini…yaani wewe mkombozi wako ni mimi na sio shangazi yako ndugu
yangu
Liliana:
mjomba wewe si mdogo wa mama yangu? utasemaje niwe nalala na wewe …hunionei
huruma nimepoteza wazazi hata arobaini yao bado tayari mmeshaanza kunitesa
kimwili na hata kiakili
Mjomba:
kumbe wewe huna akili eeh
Liliana:
nitamwambia ma mdogo…
Mjomba:
hakuna anaekufikiria hata mmoja ndugu yangu we kubali yaishe mama
Liliana:
nachelewa shule (anaondoka zake)
Mjomba:
kinajifanya kijanja sio? nitakaonyesha tu…
Liliana:
Mungu wangu naomba unisaidie(anatokomea)
Mjomba:
unadhani siwezi kumpata huyu mtoto naweza sana tu na hakuna atakayenizuia Liliana
jiandae kuwa mke wangu wa pili haijalishi wewe ni mtoto wa marehemu dada
yangu…sijali nachojali sasa ni kwamba mama yako kafa…kwahiyo hatuna undugu (anacheka kisha anapanda kwenye gari na
kuliondoa kuelekea kazini)
Liliana:(yuko njiani anatembea taratibu huku anaonekena ana mawazo sana )yaani
mama na baba yangu waliacha pesa nyingi ili nisome leo natembea kwa miguu na
kwenda shule ya serikali huku shangazi yangu na watoto wake wanatembelea magari
ya baba na mama yangu jamani(anajikuta
Analia sana)kwanini baba ulikufa?kwanini mama uliniacha mdogo…ndugu zako
wakaanza kugombania mali zenu kidogo wauane,mama wadogo hawaji tena…yaani
nimebaki mpweke sana sina rafiki Zaidi ya Anna(Analia huku anaonekana kukaribia kufika shuleni)nimewakumbuka sana
wazazi wangu wapendwa jamani…(Analia
sana) Maskini mimi sijui Maisha yangu yatakuwaje baada ya hapa sijui
nitaishije mimi (anafuta machozi)
0 Comments