MUNGU MKUU 10

 


SCENE 10: -

(Asubuhi nyingine njema, Miriam anaonekana ndo ametoka kuamka maana anajiandaa na usafi wa asubuhi hususani, usafi wa mwili wake, anapiga mswaki huku anajiangalia kwenye kioo, anacheza, anafurahi, wakati huo mama yake anakuja, kwakuwa anacheza na kuimba kwa sauti hasikii na wala hagundui kama kuna mtu kaingia)

Keddy:(anasimama mlangoni na kumuangalia mwanae) yaani huyu mtoto sijui nini kimemfurahisha asubuhi yote hii

Miriam:(anaendelea kucheza na kufurahi)

Keddy: Miriam…

Miriam:(anaendelea kucheza)

Keddy:(anamkaribia na kumshika bega) Miriam

Miriam:(anageuka) mama(anamkumbatia)

Keddy:(anamkumbatia pia) nini mwanangu mbona una furaha sana …. nishirikishe nami nifurahi

Miriam: hapana mama kawaida…leo nimeona niamke hivi…si kwa jambo lolote la msingi

Keddy: eti ee

(Wakati huo simu ya Miriam inaita na jina linaonekana kuwa ni Jeremy)

Keddy: mbona shemeji yako anakupigia simu wewe?

Miriam: hapana mama huyu sio shemeji ni kaka Fulani tunasoma nae nae anaitwa Jeremy

Keddy:ni rafiki yako?

Miriam: hapana mama nadhani anataka labda notes kidogo

Keddy: pokea sasa

Miriam:(anaangalia inaelekea kukata anaiacha) hata hivyo imekata nitampigia nikimaliza kuoga

Keddy: sawa... (anaanza kupiga hatua ilia toke nje ya chumba cha binti yake) fanya haraka leo baba yenu anataka kujumuika nanyi katika kifungua kinywa…katuamsha mapema tumepika kama wajinga kwahiyo fanya haraka

Miriam: haya mama

Keddy:(anatoka)

(Simu ya Miriam inaita tena ni Jeremy)

Miriam:(anaipokea haraka) shemeji…shikamoo?

Jeremy: marahaba…hujambo…uko wapi mbona hupokei simu?

Miriam: nipo nyumbani leo sina kipindi chuo hivyo nitakuwa nyumbani tu kwani vipi shemeji

Jeremy: naomba tujumuike pamoja katika chakula cha mchana

Miriam: haiwezekani shem...…siwezi wewe ni shemeji yangu watu watachukuliaje?

Jeremy: sijali kuhusu watu…naomba nikupitie mchana…tafadhali

Miriam: hapana…. shemeji wewe unatarajia kumuoa dada yangu…mpigie yeye ndo mjumuike pamoja na sio mimi

Jeremy:Miriam nakupenda sana…nakupenda mno…

Miriam: ah…ah hapo sasa umevuka mipaka unajua ee

Jeremy: tangu siku ya kwanza nakuona haki ya Mungu nafsi yangu ilikiri kuwa nakuhitaji wewe na sio Ariana ni wewe ndo nataka kukuoa ni wewe ndo nakupenda please nipe nafasi najua familia zetu hazitakubali ila kila kitu kitawezekana kwa Imani…please Miriam nikubalie

Miriam: samahani kwa kusema haya ila nahisi una wazimu

Jeremy: wazimu wa mapenzi juu yako Miriam…

Miriam: Mungu akusamehe sana kwa kutaka kumuoa dada yangu huku wakati huo huo unanitongoza mimi

Jeremy: nipo tayari kuwaambia wazazi wangu kuwa nakupenda wewe na nitakuoa wewe mpenzi wangu mzuri jamani naomba nafasi

Miriam: nina mpenzi wangu na tafadhali sana acha kuwa unanipigia isije ikawa msala kwangu (anakata simu kwa hasira)

Jeremy:(bado anaongea) baby nao… (anagundua simu imeshakatwa) hello…Miriam hello (ananyanyuka kutoka kwenye kiti chake alichokuwa amekalia ofisini hapo) oh shit… (anapiga tena)

Miriam:(simu ya Miriam inaita ila hapokei)

Jeremy: Miriam naomba upokee simu yangu tafadhali jamani dah…na mimi ni mpumbavu sijui kwanini nimemuambia mapema yote hii…ila nampenda sana...nampenda mno…she is the love of my life…I don’t care namzidi mbali sana, I don’t care itabidi nimsubiri mpaka amalize shule sitajali…nitamuoa Miriam na si mwingine

(Upande wa Miriam)

Miriam:yaani vanessa aliniambia wanaume ni mbwa leo nakubali itakuwaje unataka kumuoa dada yangu wakati huohuo unataka kuniaoa mimi halafu iweje…anataka atuonje wote huyu mwanaume mjinga sana…na heshima yangu kwake ndo imefika mwisho sitaki hata kumuona(anaingia bafuni kuoga baada ya kama dakika 15 anatoka kuoga anachukua simu yake kuangalia anakuta kuna missed calls  nyingi sana za Jeremy)yaani huyu jamani ananitafutia matatizo mimi jamani…(meseji inaingia anasoma)jamani naomba tuonane tuongee kidogo tafadhali  (anajisemea moyoni)yaani huyu ananitafutia shida kabisaaaaa yaani mimi sitaki(anampigia rafiki yake simu inaita mwisho inapokelewa)hello…wewe vanessa yule kaka anataka kuniletea shida nyumbani hapa

Vanesa: kafanyaje na kaka gani mbona sikuelewi?

Miriam:si shemeji

Vanessa: ah mimi nilijua tu tangu siku ile kuwa nyinyi ni wapenzi mnapendana

Miriam: what do you mean tunapendana jamani? mimi sipendani nae hata kidogo na wala sitaki kupendana nae

Vanessa: okay amefanyaje?

Miriam: ananitongoza…

Vanesa: mkubali…kwani wewe unaogopa nini?

Miriam: una kichaa

Vanessa:(anacheka) sasa unadhani utafanyaje mwenzio ndo tayari keshakuzimikia?

Miriam:(anakata simu ghafla) yaani namwambia vanessa anacheka na kuona ni utani kweli jamani hii ni haki

(Mama yake anakuja kwa mara nyingine)

Keddy: wewe bado unafanya nini? baba yako anakutafuta…halafu shemeji yako amekuja

Miriam:(moyo unalipuka)

Keddy: vaa haraka tunakusubiri(anatoka)

Miriam: Mungu wangu amekuja kufanya nini jamani haya nayo si mateso? (anavaa haraka haraka kisha anatoka bila kupaka chochote si mafuta wala nini) shikamoo baba…

Ken: marahaba mwanangu…Hujambo?

Miriam: sijambo(anatabasamu)

Jeremy:(anatabasamu pia)

Miriam:(kwa Jeremy) shikamoo shemeji

Jeremy: marahaba

Miriam: shikamoo dada Ariana

Ariana:(amekaa pembeni ya Jeremy) marahaba

Miriam:(kwa Mary) shikamoo ma mdogo…

Mary: marahaba mwanangu hujambo?

Miriam: sijambo

Keddy: bora umekuja kila mtu hapa anakusubiri wewe

Ariana:(anabenjua midomo)

Miriam: samahani kwa kuwachelewesha

Ken: usijali mama

Jeremy:(anamuangalia sana Miriam)

(Haraka Miriam anamsaidia Mary kutenga kifungua kinywa mezani, na baada ya muda wanamaliza na kukaribisha watu kwa ajili ya kifungua kinywa hicho, watu wote wanaamka na kwenda mezani kwa ajili ya kifungua kinywa hicho)

Ken:(anawaita wanae ili waje wakae pembeni yake) naomba mniweke katikati yenu nimewakumbuka sana wanangu na cha kushangaza mkwe wangu mtarajiwa nae amekuja kuungana nasi katika kifungua kinywa hiki

Jeremy:(anacheka sana)

Mary na keddy:(wanaangaliana kisha wanacheka)

Ariana:(anaonyesha chuki na hasira)

Miriam:(anafurahi)

Post a Comment

0 Comments