MUNGU MKUU 9

 


SCENE 9: -

(Jeremy amesimama nje la gari lake yupo chuoni kwa kina Miriam na anaonekana anamsubiria mtu)

Jeremy:(anatembeatembea kama mtu anayesubiri kitu kwa shauku kubwa) mbona haji?

Miriam:(anatokea akiwa na marafiki zake)

Jeremy:(anamuona) eeh huyo hapo…

Rafiki yake Miriam:(anagundua Jeremy anamuangalia sana Miriam) eeh yule kaka anakuangalia sana….

Miriam: yupi (anageuka kumuangalia) nani… (anagundua ni Jeremy) ah…kumbe shemeji…shemeji yangu huyo anatarajiwa kumuoa dada yangu…

Rafiki:(anaguna) anakuangalia sana…mbona

Miriam:na wewe kawaida tu … (kwa Jeremy) shemeji

Jeremy:(anatabasamu)

Miriam:(anamuendea) shikamoo shemeji…

Jeremy: marahaba…hujambo

Miriam: sijambo

Jeremy:za darasani?

Miriam: nzuri… (anaangalia huku na huku) dada yuko wapi?

Jeremy: hayupo…nimekuja peke yangu…

Miriam: kumbe

Rafiki:(anawaangalia chinichini)

Miriam: okay naomba niwatambulishe...shemeji huyu anaitwa Vanessa ni rafiki yangu kipenzi yaani tupo kama mtu na dada yake

Vanesa:(anatabasamu) nafurahi kukufahamu shemeji yetu

Miriam:na huyu anaitwa Jeremy…ni shemeji yetu

Jeremy:(anatabasamu kisha anajisemea moyoni) ipo siku utasema mimi ni mpenzi wako na ni shemeji wa rafiki yako

Miriam: shemeji sisi tuna haraka kidogo umekuja kumpitia rafiki yako?

Jeremy:(anababaika kidogo)

Miriam: vipi? kuna mtu unamngojea?

Jeremy: hapana…unajua nilikuwa naenda nyumbani kwenu nikaona nipitie hapa…nikupe lifti au (anamuangalia Vanessa) au nimekosea?

Vanessa: hapana shemeji hujakosewa, Upo sahihi kabisa

Jeremy:(anamuangalia Miriam usoni kisha anatabasamu) nakupenda

Miriam:(anashangaa) nini?

Jeremy: shemeji yangu…

Miriam: aha!!

Jeremy:(anacheka) basi sawa kwanini msipande gari twendeni?

Vanessa: sawa…ila mimi mtanipitisha nyumbani sidhani kama nitafika huko kote

Jeremy:(haraka haraka) sawa haina shida

Vanessa: sawa

(Wanapanda gari na haraka Jeremy analiondoa kuelekea nyumbani)

Jeremy:je mtapenda kupata icecream…kidogo au soda?

Vanessa: ofcourse

Miriam: wewe Vanessa mimi baba na mama watakuwa na wasiwasi sana…

Vanessa: okay ngoja… (anachukua simu na kumuandikia meseji Mary) anti…Miriam atachelewa kidogo tunaenda kula icecream na shemeji Jeremy

Mary:(anaipokea meseji na kuijibu) haya lakini msichelewe sana…

Vanessa:(anapokea meseji na kuisoma kwa nguvu) haya lakini msichelewe sana, (kwa Miriam) unaona Miriam anti Mary huwa ana upendo na ni mwelewa sana…halafu nilisahau kukuuliza mbona mnafanana sana na anti Mary…

Miriam: hata mimi sijui kwakweli…

Jeremy:(anamuangalia Miriam kupitia kioo kidogo kilichopo mbele) Miriam (anajisemea moyoni) wewe ni mzuri

Miriam: abeee shemeji

Jeremy: tunaenda kwenye icecream au soda au tunaenda nyumbani?

Miriam: twende kwenye icream ila tusichelewe…

Jeremy: haina shida (anaendelea kuendesha gari huku kila mara anamuangalia Miriam kupitia kioo cha mbele)

Vanessa:(anagundua kuwa Jeremya anamuangalia sana Miriam) mmmh (anajisemea moyoni) huyu shemeji anampenda Miriam huyu…ona anavyomuangalia vizuri ila kama ni mchumba wa Ariana Miriam hata asijaribu kumkubali huyu kaka ikitokea amemtongoza

(Hatimaye wanafika katika mgahawa mmoja)

Jeremy:(huku anakaa) hapa sidhani kama kuna icecream

Vanessa: hapa hapa panatosha bwana…

Jeremy: agizeni chakula...mimi sili

Vanessa: mimi nitakula

Jeremy:(huku anatabasamu) wewe Miriam je?

Miriam:mi nitakunywa soda

Vanessa: yaani huyu muoga nyie…

Miriam: hapana sijisikii tu kula

Vanessa:(kwa Jeremy) shem…hata hatujala tangu asubuhi hapa unavyotuona

Jeremy: sasa mwenzio mbona hataki kula?

Vanessa: uoga tu (anamuita mhudumu) anti…

Miriam:(anamfinya)

Vanessa:(anamtoa mikono) wewe vipi…agiza huko

Mhudumu(anafika)karibu niwasikilize

Vanessa:mi naomba chipsi kuku…na huyu hivyohivyo

Jeremy:(anatabasamu kisha anamuangalia Miriam)

Mhudumu:(anaondoka kuelekea jikoni)

Miriam:(anaonekana kuwa na wasiwasi)

Vanessa: wewe...nini? si upo na shemeji yako? nani atakuuliza?

Miriam: haya bwana (anajitahidi kuwa mchangamfu)

Jeremy:(simu yake inaita anaiangalia anaona ni Ariana anaona asiijibu)

Miriam: vipi? pokea simu shemeji…

Jeremy:si ya muhimu ni ya kazi na muda wa kazi umeisha

Miriam: aha kumbe

Jeremy: yeah…

(Baada ya dakika kumi na tano mhudumu anakuja na chakula cha Miriam pamoja na Vanessa)

Mhudumu: karibuni…

(Miriam na Vanessa wanapokea vyakula na taratibu wanaanza kula wakati huo Jeremy anaagiza kinywaji cha baridi na kuanza kunywa huku Vanessa na Miriam wanakula taratibu, wakati wanaendelea kula Jeremy anamuangalia sana Miriam, na Miriam akimtupia macho anaangalia chini na kukwepesha macho, hali inaendelea hivyo hivyo)

Mirriam: shemeji ndo umekataa kula?

Jeremy: wewe kula tu shemeji yangu usiwe na wasiwasi na mimi

Mirriam: (Anatabasamu)

Jeremy: (anaonekana kupagawa na Mirriam)

Vanessa: (anamuangalia sana Jeremy)

Jeremy: (haachi kumuangalia Miriam)

Post a Comment

0 Comments