MUNGU MKUU 11

 


SCENE 11: -

(Jioni ya siku nyingine tena, Jeremy yupo chuoni kwa kina Miriam anamsubiri Miriam amesimama nje ya gari yake na anaonekana hana haraka kabisa hata ikitokea Miriam amechukua muda mrefu, baada ya kusimama hapo muda mrefu hatimaye Miriam na rafiki yake Vanessa wanatoka darasani)

Vanessa :( anamuona Jeremy) ona baby kaja

Miriam :( hajamuona) baby gani?

Vanessa: Jeremy

Miriam :( anamuona Jeremy baada ya kuangaza kwa muda)

Vanessa: Jeremy baby

Miriam: sikiliza nikwambie kitu Vanessa Jeremy sio baby wangu na sitaki awe baby wangu sijui nimeeleweka au bado?

Vanessa: kamwambie sasa...ila sikia huyu kaka anakupenda na anachofanya sasa hivi anakufuatilia sana na anataka uwe wake na anaonekana yupo serious wewe si ulisema ana kampuni zake sasa embu jiulize kwanini anaacha kazi zake anakufuatilia kasungura kama wewe…mpe nafasi

Miriam: wewe una kichaa shoga yangu unajua kabisa Mimi na dada yangu tunahangaika kuyaweka mahusiano yetu vizuri halafu sasa hivi unanishauri utumbo acha ujinga huyu kaka ni shemeji yangu na sitawahi kuwa mpenzi wake hata iweje sitaki kuwa mpenzi wake mimi ndo nimeamua

Vanessa: sawa haina shida shoga yangu

Jeremy :( anawafata) hamjambo warembo

Vanessa: hatujambo shikamoo

Jeremy: marahaba (kwa Miriam) Miriam?

Miriam: shikamoo... (Huku anaangalia pembeni)

Jeremy: marahaba…

Miriam :( Kwa Vanessa) Vanessa twende

Jeremy: wapi?

Miriam: nyumbani kwani wapi tena?

Jeremy: Miriam nimekuja kukuchukua

Miriam: unipeleke wapi?

Vanessa: acha kumjibu hivyo jamani

Jeremy: Miriam, unajua ninavyokupenda wewe mtoto...kwanini usinipe nafasi?  nakupenda na nipo serious

Miriam: kaka hilo neno umeshaniambia mara nyingi sana ila sikutaki nina mpenzi wangu naomba uendelee na maisha yako mimi sikutaki...huelewi nini? Sitaki mimi jamani

Jeremy: Miriam…

Miriam: wewe ni shemeji yangu naomba ibaki kuwa shemeji yangu kila mtu atashangaa kuona eti shemeji ni hawara yangu

Jeremy: sina mpango wa kuwa hawara yako nataka kuwa mumeo nataka uwe malkia wa himaya yangu

Miriam: dada yangu ndo malkia wa himaya yako sio mimi naomba basi uelewe jamani kwani nini tatizo?

Jeremy:(kwa Vanessa) kwani kupenda ni kosa? (kwa Miriam) basi kama ni kosa niadhibu nipo tayari kuchukua adhabu yeyote ila tu (anashusha pumzi) …naomba nafasi

Miriam: jamani kaka haiwezekani

Jeremy: dah…Miriam…naomba please

Miriam: (kwa msisitizo) no!!!

Vanessa: Miriam, mpe mwenzio nafasi jamani kwani nini tatizo?

Miriam:(anajikuta anapandwa na hasira) wewe Vanessa kama unamuonea huruma si umchukue? mimi sitaki matatizo na familia yangu, ukweli ni kwamba huyu kaka ni mchumba wa dada yangu…na alikuja nyumbani ili amuoe dada yangu yaani hapa walipo wapo kwenye hatua na maandalizi ya harusi…halafu wewe leo unaniambia nimpe nafasi huyu

Jeremy: dada yako sina mahusiano nae yeyote na yeye mwenyewe anajua hilo

Miriam: dada yangu anakupenda sana Jeremy mno na mno na ndoto zake ni kuoana na wewe

Jeremy:lakini,sina hisia zozote juu yake nakiri kwamba ni kweli mimi na wazazi wangu tulikuja kwenu tukiwa na lengo la kumchumbia Ariana lakini nilipokuona I swear moyo wangu ulikupenda wewe na sikuwa tayari kunyamaza kimya juu ya hili…hata wazazi wangu nitawaambia,sio kosa nina uhakika hata dada yako ataelewa jamani kuwa moyo huamua yote na sio kichwa,ni kweli kichwa changu kinasema nimuoe Ariana lakini nini kitatokea baada ya mimi kumuoa Ariana?nitajuta maisha yangu yote kwamba sikuwa tayari kupambana na akili yangu ili niishi kwa furaha…

Miriam: familia yangu inanipenda Sana…na sitaki kuharibu uhusiano nilionao nao mimi na familia yangu tafadhali sana

Jeremy: wazazi wetu watatuelewa tu,

Miriam: wewe ndo unaona kuwa watatuelewa, ila hakuna mzazi atakayekubali kuwa mwanaume alikuja kumchumbia mtoto wake mkubwa halafu mwisho wa siku akawa na mahusiano na mtoto mdogo…naomba uelewe kuwa hatuwezi kuwa na mahusiano hata kwa siri

Jeremy: Miriam unaogopa nini?

Miriam: kwanza wewe ni mkubwa sana kwangu hatuendani

Jeremy: Miriam hiyo haijalishi mapenzi hayaangalii umri

Miriam: nimekataa sitaki

Jeremy: Miriam nampigia baba yangu simu sasa mbele yako namwambia kuwa sitaki kumuoa Ariana

Vanessa: maskini kaka wa watu mpaka anatia huruma

Miriam: sasa unampigia simu ili iweje?

Jeremy: ngoja (anatoa simu yake aina ya iphone 14 na kutaka kumpigia baba yake)

Miriam: acha ujinga…Jeremy unadhani haya ni rahisi?

Jeremy: nakupenda Miriam…

Miriam: hatuwezi kuwa pamoja katika haya maisha

Jeremy: Miriam

(Miriam anamvuta Vanessa ili waondoke, Jeremy anapanda gari lake haraka kisha anawafata kwa nyuma)

Jeremy: Miriam…ngoja nikwambie okay sitamwambia mtu, itakuwa siri yetu wawili please…na sitafanya kitu chochote ambacho hutotaka…the fact kwamba wewe ni girlfriend wangu itatosha sana

Miriam:(anasimama) siri??!!halafu…?

Jeremy: ndugu zetu watajua tu mbele kwa mbele

Miriam: hapana Jeremy

Vanessa: mbona mwenzio katoa wazo zuri tu…mpe mwenzio nafasi

Jeremy: ukinipa nafasi nitakutunza sana na utapenda

Miriam: hapana…(anakimbia)

Jeremy:(anashuka kwenye gari kisha anamkimbiza) sikiliza Miriam

Miriam: nakuomba sana sitaki kugombana na dada yangu…nihurumie Jeremy

Jeremy: wewe ndo unihurumie…hurumia moyo wangu, hurumia hata shughuli zangu…sasa umekuwa kama ugonjwa umekuwa kama chakula siwezi kuishi bila kukuona…nakupenda my queen(anamkumbatia)

Miriam:(anajikuta anamkumbatia pia) una kichaa hujui baba anaweza kuja wakati wowote kuja kunichukua

(Gari la baba yake linakuja)

Miriam: Kama niliota baba huyo hapo naomba niende…

Jeremy: okay nitakupigia baadae mazungumzo yetu hajaisha

Miriam: naomba usinipigie simu

Jeremy: namwambia baba yako kuwa nakupenda sana...nitatoboa siri hapa sasa hivi sema suu…

Miriam: sawa nipigie…

Jeremy: (anatabasamu kidogo) okay bye…

Miriam :( anaondoka kuelekea gari la baba yake lilipo) Vanessa twende

Ken: nimemuona mtu Kama Jeremy anafanya nini?

Miriam: ana ndugu yake hapa, amekuja kumpitia

Ken: okay…Mimi nawahi sitamsalimia (anapanda kwneye gari na kuliondoa)

Post a Comment

0 Comments