MUNGU MKUU 6

 


SCENE 6: -

BAADA YA MIAKA 18: -

(Usiku mwingine mtulivu sana, nyota zinaonekana kwa wingi angani kila mtu anaonekana kalala, Ariana ambae kwa sasa amekuwa mtu mzima kidogo anaonekana yupo disko anacheza huku anakunywa pombe, yupo na vijana wengi wanaonekana kutapanya pesa bila mpangilio. Kwakuwa amekuwa mtu mzima sana amebadilika sana pamoja na njia zake mbaya anaonekana mrembo sana)

Rafiki yake: ila unawatesa wazazi wako…huna mwelekeo rafiki yangu

Ariana: Angelica we kunywa kama umechoka kalale…usinichoshe…wazazi wangu waliamua kuniletea kitoto eti mdogo wangu na wakafanya kila kitu kuonyesha kuwa wanampenda yeye na sio mimi mtoto wao waliomzaa wenyewe, sasa unadhani nina faida gani kwao kama kwa midomo yao wamekuwa wakimsifu huyo mpumbavu mbele yangu…kila kitu nilichofanya ni kosa sana kwao unadhani nitafanyaje…acha niponde raha mama zikiisha nitaongeza

Angelica: lakini rafiki yangu unajikomoa mwenyewe na sio wazazi wako kwanini usitafute njia nyingine…wewe fanya yaliyo mema hata kama wazazi wako hawaoni…Mungu atakusaidia rafiki yangu lakini unavyofanya hivi unawaudhi wazazi wako na Mungu pia

Ariana: umemaliza? okay tutaonana kesho… (anatoka nje na kupanda gari lake alilokuwa ameliegesha nje na kuliondoa, anaenda kwa muda na hatimaye anafika nyumbani)

Miriam:(binti mrembo sana na anaonekana kuwa ni mcha Mungu, ni yuleyule mtoto aliyeokotwa nje ya geti miaka 18 iliyopita na kulelewa kwa upendo mkubwa kama mtoto aliyezaliwa kwenye familia hiyo) dada... (anafungua mlango)

Ariana: embu nipishe huko (anamsukumia pembeni)

Keddy:(amebadilika anaonekana ni mama wa makamu na mvi zinaanza kutokea) Ariana… (anamfuata alipokuwa amesimama) unatoka wapi sasa hivi?

Ariana:(anafyonza) acha kunizingua, wewe unajali nini? wewe si unamjali sana huyo zawadi uliyopewa na Mungu…sijui mimi ni zawadi uliyopewa na shetani

Mary:(na yeye anaonekana ni mama wa makamu na mvi zinaanza kutokea) Ariana...

Ariana: kelele…na wewe mfanyakazi uliyeishi kwetu miaka 18 utasema ndo nini sijui…usiniongeleshe sina muda huo wa kusikiliza ushenzi...

Ken:(anaonekana ana mvi) Ariana (anamzaba kibao)

Ariana:(anashika shavu) embu niacheni… (anaingia chumbani kwake kwa hasira)

Ken:(anakaa kwenye sofa) sijui tumfanye nini huyu mtoto jamani jinsi miaka inavyoenda ndo anazidi kuwa mtata
keddy: mume wangu acha kufikiria haya…

Mary: tumsamehe tu

Keddy: Mungu alitupa zawadi ya mtoto tena wakati ambao ulikuwa muafaka (anamuangalia Miriam) mwanangu, mvumilie dada yako…ni dada yako wa tumbo moja embu sahau yote na umpende hivyo hivyo

Miriam: sawa mama (anaachia tabasamu zuri)

Mary:(anajisemea moyoni) mwanangu nimzuri sana, ingekuwa vipi kama ningetoa mimba, au ningekuacha tu upate tabu mpaka ufe mwanangu…kweli Mungu ni mkuu alinielekeza mpaka kwa hawa wazazi wenye upendo mwingi…nakupenda mwanangu na ninawapenda hata wazazi wanaokulea kukusomesha na kukupa malezi mazuri

Keddy:(anamshtua) mwenzangu vipi mbona unaonekana una mawazo mengi tatizo nini mama?

Mary: hapana dada…ni kawaida tu

Keddy:au unamuwaza Ariana?

Mary: Ariana muacheni tu atakuja kuwa mtulivu

Keddy: mpaka lini…leo hii ana miaka 30 lakini hajishughulishi kwa chochote katika haya maisha jamani atakuwa mgeni wa nani? siku tukitoweka hapa duniani?

Ken: basi kwa maana hiyo aondoke nyumbani kwangu...

Miriam: baba…tafadhali usimfukuze dada (anapiga magoti pembeni ya baba yake) tafadhali baba…

Ken: ndo uamuzi wangu…mimi ni mtumishi wa Mungu na nyumba yangu inatakiwa imtumikie Mungu na sio anachofanya Ariana binti yangu mkubwa

Miriam: baba tafadhali… (machozi yanamlenga)

Mary:(anajikuta anamuonea huruma mwanae) basi mwanangu baba yako atamsamehe  

Keddy: baba Ariana msamehe mwanao tafadhali

Ken: hapana…siwezi, unless abadilishe mienendo yake ndo nitamsamehe nampa wiki hii nzima...

Ariana:(anatokea chumbani kwake na mabegi) wala usijisumbue wiki nzima ya nini…?

Miriam:(anamfata Ariana) dada

Ariana: mimi sio dada yako…wewe mbwa

Mary: Ariana…

Keddy:(Analia) mwanangu jamani…mbona umekuwa hivi nilikuzaa ukiwa ni mtu mwenye upendo hukuwa mjeuri

Ariana:(anawapuuzia wote)

Ken: kwanini uko hivyo…?

Ariana: nipoje? niwatendee nini…miaka hii yote nimewaridhisha kwa nguvu zangu zote lakini hamjawahi kuridhika kila mara huyo mtoto wenu ndo kawa kipaumbele…kila kitu kizuri ni yeye na kila kitu kibaya kimefanywa na mimi…niwafanyeje…ndo maana nimechagua kupita hii njia sijali chochote nafanya nachojisikia naondoka na kama huyo Mungu wenu mnaomuabudu kila siku humu ndani yupo basi atanisaidia na mimi hata kama ni mbaya na sina utakatifu wa huyu mtoto wenu mpendwa

Keddy:(anamshika mkono) mwanangu nisamehe mimi mama yako yamkini ni kweli kabisa, nilikusahau naomba msamaha na kukuahidi sitarudia tena nitakujali nitakuheshimu mwanangu…yamkini ni kweli kabisa napitiwa kibinadamu naomba msamaha wako mwanangu na ninakuahidi kuwa utaishi vizuri tu mama

Ariana: mumeo amenifukuza…na mimi natii sheria ya mfalme na kukuahidi kuwa nitafanya kama ulivyamrisha

Ken:(anaamua kujishusha) mwanangu sasa hivi ni usiku mama unadhani utaenda wapi? naomba unisamehe mimi baba yako kwa haya niliyosema nimetumia hasira tu

Miriam: dada msamehe baba, nisamehe hata na mimi

Ariana:(anamsukuma) usizoee kuniita mimi dada…umeelewa?

Mary: Ariana…usifanye hivi…huyu ni mdogo wako…

Ariana:(anakaa kimya)

Keddy: sawa mama…rudisha vitu vyako ndani ikapumzike tutazungumza kesho asubuhi…

Ariana: nendeni tu…nimeshawaelewa nitakaa tu hapa nyumbani…mpaka

Ken: pale utakapoolewa

(Kila mtu anaonekana amesahau lililotokea kwa muda kidogo)

Mary: walisema watakuja…kutoa mahari hivi karibuni

Keddy: tunawasubiri kwa hamu

Ken: harusi yako itakuwa nzuri sana mwanangu na ya kifahari sana

Miriam: nitacheza sana…siku hiyo jamani

Ariana: lakini sikuwapa jibu kama nataka kuolewa au lah…

Keddy: mimi ukiniahidi kuwa utaolewa ukifika miaka 30…yule kijana anakupenda sana na ana haraka ya kukuoa…

Ariana:(anaweka mizigo pembeni yake kisha anakaa maana muda wote huo alikuwa amesimama) sijawahi kuwa na mahusiano na huyo mtarajiwa wangu mnaniambiaje niolewe nae?

Ken: yeye anakujua na anataka kukufanya uwe malkia katika himaya yake

Ariana: haya, sawa nitamuona…

Keddy: utanipa jibu mwanangu…anakuja nahisi kesho…wanakuja na washenga…kuomba undugu

Ariana:(anaguna kidogo) bado sijampenda sasa atakujaje na washenga

Miriam: nina uhakika kuwa utampenda, ni mwanaume wa dizaini unayoipenda, mrefu, mzuri na Zaidi ya yote ana hofu ya Mungu

Ariana:(anajisemea moyoni) yaani huyu nae sijui nani kamwambia nataka mwanaume mwenye hofu ya Mungu?

Miriam:na pia ana uwezo wa kimaisha kwa kweli yupo vizuri ni mtoto wa rafiki wa baba

Ariana: okay…nimewaelewa (ananyanyuka na kwenda chumbani kwake)

(Wanaobaki sebuleni wanaonekana wana furaha na kusahau ugomvi uliotokea muda mfupi uliopita)

Ken:ni kumvumilia tu…ni mtoto wetu hatuna jinsi… (anacheka kisha ananyanyuka na kuingia chumbani kwao)

(Miriam, Keddy na Mary nao wanaingia kila mmoja wao chumbani kwake)

Mary: kila kitu kitakuwa sawa hata sijali (anajifunika shuka na kulala)

Post a Comment

0 Comments