ON MY WEDDING DAY 07


 

SCENE 7: -

(Usiku wa siku hiyohiyo ya jumamosi, Patrick na mpenzi wake wameshafika nyumbani kwa Patrick, wao pamoja na marafiki zao, kila mtu yupo kwenye chumba chake isipokuwa Patrick na Olivia wamekaa chumba kimoja)

Olivia: baby… (Anaweka kichwa chake begani kwa Patrick) umemwambia mama kuwa nitalala huku?

Patrick: nishamwambia baby

Olivia: Asante nime enjoy sana leo…

Patrick: usijali nipo kwa ajili yako

Olivia: asante…nina kiu…naomba maji ya kunywa...

Patrick :( anaiendea friji ndogo iliyopo chumbani humo) huwa kuna maji humu ngoja nikupe (anaifungua anagundua kuwa hakuna maji) kumbe hawajaweka

Olivia: kachukue…

Patrick :( anacheka kisha anaelekea jikoni, baada ya hatua chache anafika jikoni anafungua friji)

Monica :( anakuja akiwa amevaa khanga moja nyepesi Sana iliyomfanya kuonyesha asilimia kubwa ya maungo yake ya ndani) ah…samahani Shem…sijui nimekosea?

Patrick :( anaonekana kutojali anachokiona mbele yake) unataka nini Shem?

Monica: natafuta maji ya kunywa Shem...

Patrick: yapo chumbani huko angalia kwenye friji

Monica :( anabana sauti inakuwa Kama ya mtoto anayemdekea mama yake) hamna maji kwenye friji

Patrick: ah! Itakuwa dada Halima alisahau kuweka ngoja nimwambie

Monica :( anamvuta mkono)

Patrick :( Kwa mshangao) vipi?

Monica: nyumba yako nzuri kweli Shem

Patrick: nashukuru

Monica: (anang’ata midomo yake) nzuri kweli Kama wewe

Patrick :( anaondoka kuelekea chumbani kwake)

Edwin:(anapita maeneo ya chumba cha Patrick, anakuta mlango wa Patrick uko wazi kidogo na Olivia yupo anabadilisha nguo ingawa haonekani vizuri ila mwili wake kwa nyuma unaonekana vizuri sana, Edwin anabaki anashangaa kuona umbo zuri vile) wow…

Patrick :( anatokea kwa nyuma yake) Edwin…vipi?

Edwin :( anashikwa na kigugumizi) ha…mna kitu, nilikuwa natafuta maji

Patrick :( anacheka) masihala mengine hayafai unajua eeh...

Edwin: kwanini…

Patrick: maji chumbani kwangu na mpenzi wangu kwani wewe ni mara yako ya kwanza kuja katika hii nyumba usijue maji yanakaa wapi? anyways kaa tu chumbani da Halima anakuletea sasa hivi

Da. Halima :( anaweka maji kila chumba)

Patrick: nadhani yapo tayari

Edwin: poa usiku mwema (anaenda chumbani kwake)

Monica :( anapita na khanga yake moja mbele ya Patrick)

Patrick :( anaingia chumbani kwake, anakaa pembeni ya Olivia)

Olivia: vipi?

Patrick: ah…poa (anajisemea moyoni) yaani hawa watu siwaelewi…sijui nimwambie Olivia…ah ngoja nipotezee ikiendelea ndo nitamwambia

Olivia: Patrick hauko sawa

Patrick: kwanini…

Olivia: sijui ila nakuangalia usoni nakuona umebadilika mara baada ya kutoka kuchukua maji kuna tatizo?

Patrick: ah usijali my darling nipo poa …

Olivia: hujapenda nini baba nambie

Patrick: usijali mbona Mimi nipo poa…labda itakuwa usingizi

Olivia :( anatabasamu kisha anadeka kidogo) lala basi baba

Patrick :( anatabasamu) Kwa kudeka (anacheka)

(Olivia anamlalia kifuani wanaendelea kuzungumza huku kila mmoja wao akionekana kufurahia faragha ile)

Patrick: lala na wewe…mbona umekodoa macho tu

Olivia :( anacheka)

Patrick: Olivia mke wa Patrick…naitamani hiyo siku

Olivia: hunishindi Mimi jinsi navyotamani kuwa mkeo

Patrick: ifike bwana maana hapa tunamkosea bwana tunazini

Olivia :( anainuka) chumba cha wageni kiko wapi nikalale huko

Patrick :( anacheka) wewe embu lala

Olivia: au nilale chini

Patrick :( anacheka) lala

(Wanaendelea kutaniana huku kila mmoja wao anafurahia faragha hiyo)

Post a Comment

0 Comments