ON MY WEDDING DAY 11


 

SCENE 11: -

BAADA YA WIKI MBILI: -

(Ni asubuhi nyingine njema machoni pa bwana, Olivia amekaa katika mgahawa mmoja ambao yeye na Patrick walipenda kwenda kunywa chai pamoja au wakati mwingine kupata chakula cha mchana pamoja, amekaa pale lakini anaonekana hana raha kabisa ya kila kitu, anaonekana kumkumbuka Patrick kwani mara nyingi aliitazama picha ya Patrick iliyokuwa ipo katika simu yake)

Olivia:(huku anaiangalia picha ya Patrick) my love…nimekukumbuka sana, nini kilitokea kwetu mpaka mambo yetu yakaharibika

(Wakati huo Patrick nae anaingia mahala pale, tararibu anaenda kukaa meza iliyokuwa haina mtu kisha anamuita mhudumu)

Olivia:(anasikia sauti ya Patrick na kugeukia inapotokea) Patrick?

Patrick:(anaangaza huku na huku akiwa ana nia ya kumtafuta mhudumu lakini anajikuta macho yake yameangalia kwa mtu mmoja nae ni Olivia) Olivia…baby(anamuendea)mambo vipi Olivia?

Olivia:(anatabasamu) safi za siku?

Patrick: nzuri…hupokei simu yangu Olivia…kwanini lakini?

Olivia…. sio hivyo mambo ni mengi Patrick…

Patrick:au bado umechukia kitendo cha mimi kukuficha?

Olivia: embu karibu kwanza uketi ndo tuongee…

Patrick:(anavuta kiti kisha anakaa)

Olivia: wifi hajambo

Patrick: nani sasa agnes au Halima?

Olivia: mpenzi wako

Patrick:(anacheka) sina mpenzi, mimi mpenzi wangu ni wewe ingawa umeamua kutafuta mpenzi mwingine

Olivia:(anashangaa) wewe Patrick, iam single and very single sina mwanaume wala nini

Patrick: unasema kweli? mimi niliambiwa na Edwin kuwa una mtu wako na mna mipango ya ndoa…

Olivia:(anacheka) mimi Monica aliniambia kuwa ulienda kwa huyo mpenzi wako mpya na kutoa mahari…

Patrick: halafu Olivia bana unapenda sana kumuamini Monica

Olivia: she is my friend

Patrick:(anamuangalia kwa muda kisha anasimama na kumkumbatia mpenzi wake huyo) I missed you so much, tusahau hayo ya Monica sijui Edwin wana lengo la kututenganisha

Olivia: sasa kwanini wafanye hivyo?

Patrick: sijui kwakweli si uchawi tu

Olivia:(anacheka) yaani wewe

Patrick: nakupenda naomba turudiane…nilete mahari kwenu ili tuoane

Olivia: uko serious unataka kuwa mume wangu Patrick?

Patrick: Zaidi ya serious…

Olivia:(anatabasamu) I love you Patrick…mwanaume wa moyo wangu

Patrick: nami nakupenda Zaidi mke wangu

Olivia:(anacheka)

Patrick:(anatabasamu)

Mhudumu:(anakuja) kaka karibu…

Patrick: asante sana…nipe tu supu ya kuku na chapatti mbili

Mhudumu: sawa(anaondoka)

Patrick:(anamgeukia Olivia aliyekuwa anamuangalia muda wote wakati anaagiza) wewe vipi? mbona unaniangalia sana

Olivia: nilikukumbuka sana na tangu tuachane hii ni wiki ya pili nimekuwa nikija hapa kupata chakula nikiwa na matumaini ya kukuona mpenzi wangu

Patrick: hata mimi huwa nakuja hapa kila siku nikiwa na tumaini la kukuona maana nilikuwa naogopa kuja kwenu nikihofia nitamkuta mpenzi wako mpya halafu nilivyo na wivu sijui tu ingekuwaje?

Olivia:(anacheka) nani alikuambia?

Patrick: Edwin…

Olivia: na yeye…mmbeya huyo amenikera

Patrick: labda anakutaka

Olivia: ah…wapi?

Mhudumu:(analeta supu na kuitenga hapo kisha anaondoka)

Olivia: nitamwambia monica kuwa nimerudiana na wewe atafurahi kweli

Patrick: usimwambie

Olivia: baby…Monica ni Zaidi ya rafiki yangu yaani ni kama dada yangu kabisa…nampenda kama dada

Patrick: rafiki yako ndo adui yako my love…usimwamini sana Monica

Olivia: lakini kama kunidhuru angekuwa ameshafanya hivyo siku nyingi

Patrick: kila mtu ni mtu mbaya kutokana na mazingira yaliyomchochea kuwa mtu mbaya

Olivia:mi hata sikuelewi

Patrick: kama kweli unanipenda basi naomba unielewe kuwa sitaki Edwin wala Monica wajue tumerudiana

Olivia: yaani sitaki maugomvi na wewe kwahiyo nitakutii…

Patrick: asante (kimya huku anakunywa supu yake)

Olivia:(anacheka kidogo) umekonda baby

Patrick: mawazo…chezea kukosa mke wewe

Olivia:(anacheka huku anatoa simu yake na kutaka kujipiga picha yeye na Patrick)

Patrick: hapana, najua unataka kumtumia Monica, baby ukifanya hivyo mipango yetu itaharibika…kunywa chai twende kwa dada Agnes na Halima maana wamekukumbuka kweli yaani

Olivia:mi nimeshamaliza kunywa chai nakusubiri wewe love (anajipiga picha)

Patrick: I love you

Olivia:(bado anaonekana kunogewa na kupiga picha) umeshaniambia…kuwa unanipenda baby…

Patrick: nataka nishinde nakwambia hivyo ili usiniache tena nataka uniamini mimi na usiamini unachoambia hasahasa na Monica

Olivia: poa baby…

Patrick:(ananyanyuka na kwenda kunawa) twende…

Olivia:(ananyanyuka pia na kwenda kunawa)

Patrick: nakupenda Olivia

Olivia:(anacheka kisha anamwagia maji usoni)

Patrick: wewe acha watu wanatushangaa(anacheka)twende nyumbani (anamuita mhudumu)

Mhudumu :( anakuja)

Patrick:(anatoa noti ya shilingi elfu kumi) wawili, mimi na mke wangu

Olivia:(anacheka)

Patrick :(kwa mhudumu) keep change (kwa Olivia) twende

Olivia :( anamfuata nyuma)

(Kwa pamoja wanatoka na kuelekea mpaka katika maegesho ya magari na kupanda gari la Patrick)

Patrick: nimekuja peke yangu naondoka na mke

Olivia :( anacheka)

Patrick :( anacheka) umefurahi eeh…najua hata wewe ulikuwa umenimisi (anaanza kuendesha gari taratibu)

Olivia: (anaonekana kufurahia sana uwepo wa mpenzi wake)

(Wanaendelea kufurahia maisha kwa pamoja huku kila mmoja wao anatoa ya moyoni na wanaonekena kuwa walikumbukana sana baada ya kupotezana kwa takribani wiki mbili)

Post a Comment

0 Comments