ON MY WEDDING DAY 06


 

SCENE 6: -

JUMAMOSI

(Jioni nyingine tulivu kabisa…kuna upepo Fulani mwanana unavuma, mbali na upepo kuna hali ya kama mvua kutaka kunyesha, Patrick na rafiki yake kipenzi wamekaa katika mgahawa Fulani na unaonekana kuwa ni wa gharama, wanaongea huku wanapata vinywaji taratibu)

(Simu ya Patrick inaita)

Patrick :( anatabasamu kidogo)

Edwin: vipi? Mbona unatabasamu mwenyewe?

Patrick :( anapokea simu) honey…vipi mmeshafika?

Olivia: ndio baby mpo wapi?

Patrick: ngoja natoka kuja kuwachukua…

Olivia: poa tunakusubiri hapa getini

Patrick: sawa my Queen… (Anakata simu kisha anamgeukia Edwin) mwanangu tayari wameshafika…ngoja nikawachukie nakuja sasa hivi

Edwin: poa hamna noma (anaendelea kunywa kinywaji chake)

Patrick :( anatoka nje moja Kwa moja anaenda mpaka walipo Olivia na rafiki yake)

Monica :( anaangalia huku na huku anaona kwa mbali mtu kama Patrick) shemeji huyo

Patrick :( anatokea anaachia tabasamu mara baada ya kumuona mpenzi wake) baby (anambusu Olivia mdomoni)

Monica :( anamuangalia Patrick Kwa tamaa kisha anajisemea moyoni) dah…huyu mwanaume mzuri jamani

Patrick :( anamshika mkono Monica) shemeji mambo vipi?

Monica: poa vipi?

Olivia :( anatabasamu muda wote)

Patrick: poa (anawaongoza njia) njooni huku maana sie tumejificha mbali Sana

(Kwa pamoja wanaenda mpaka alipokuwa amekaa Edwin)

Patrick: Wale tulikokuwa tunawasubiri Kwa muda wa masaa karibia mia hawa hapa

Olivia :( anacheka) jamani baby kwani tumechelewa Sana?

Patrick: vibaya Sana… (Anafyonza kisha anacheka) muone (Anacheka tena)

Edwin :( anamuangalia Olivia Kwa tamaa pia na yeye anajisemea moyoni) mrembo Sana…duh...Sasa huyu anafaa kuwa mke wangu na sio mwingine…Patrick jiandae kumpoteza huyu mwanamke…she is mine

Patrick: warembo karibuni mketi

(Wanawake wanakaa, Olivia anakaa pembeni ya Patrick na Monica anakaa pembeni ya Edwin)

Patrick: hii inaitwa double date…

Edwin :( anacheka huku anamuangalia Sana Olivia)

Monica :( anamuangalia Sana Patrick)

Patrick: ok naomba niwe ndo msemaji maana naona wote mnaogopa ogopa…ok…baby huyu (anamuonyeshea Edwin) ni rafiki yangu wa pete na kidole anaitwa Edwin…yaani ni kama kaka yangu, tumesoma wote tumehangaika wote (kwa Edwin) eti si tumehangaika ee (anacheka)

Edwin :( anaguna) tumehangaika wapi huku wewe ulikuwa mtoto wa kishua usinitanie (anacheka kidogo)

(Wanacheka)

Patrick: unaniaibisha brother

Edwin :( anacheka) pole mwaya

Olivia :( anaachia tabasamu Safi linalowachanganya wanaume wote hapo) nashukuru kukufahamu Shem (anampa mkono)

Edwin :( anaupokea kisha anamuangalia usoni na kumpa tabasamu la kichokozi)

Olivia :( anakuwa hayuko huru na tabasamu hilo)

Patrick:(anacheka) mzoee tu… (kwa Edwin tena) brother… (anamuangalia Monica) huyu ni rafiki wa mke wangu anaitwa Monica

Monica :( anaachia tabasamu)

Edwin: Oh, she is beautiful

Monica :( anacheka)

Olivia :( anatabasamu) jamani dah!!!Mnafaa kweli kuwa mtu na mtu wake (anacheka) au nasema uongo baby boo

Patrick: (anatabasamu) sawa kabisa (anamuangalia Monica) na shem…kwa kuwa rafiki yako hajataka kunitambulisha naomba nijitambulishe…naitwa Patrick Kalenzi ni mume wa miss Olivia

Olivia :( anatabasamu) jamani nilikuwa najiandaa kukutambulisha mbona umejiwahi (anacheka)

(Wote wanacheka)

Monica :( anampa mkono Patrick huku na yeye anaachia tabasamu Fulani la kitata)

Patrick :( anakuwa Kama anashangaa kidogo ila anaona apotezee tu)

Edwin: karibuni ladies na agizeni chochote, hapa ni kuparty mpaka majogooo… (Anakunywa kinywaji kidogo)

Patrick :( anatania) boss kasema (anamshika mkono Olivia wake)

(Monica na Edwin wanaangalia chinichini na wanaonekana hawafurahii kitendo kile cha wawili wale kuonyesha mapenzi yao vile maana kila mmoja amevutiwa na shemeji yake, yaani Monica amempenda Patrick na Edwin amempenda Olivia)

Patrick: Shem agizeni…Olivia agiza…mbona mmepooza jamani…

Olivia: hatujapooza honey...Tunasubiri mhudumu…

Edwin :( anamuangalia Sana Olivia)

Patrick: ok my dear…hamna shida (anamshika Olivia kidevu)

Mhudumu :( anakuja kuwasikiliza) karibuni jamani

Patrick :( anamuangalia Olivia kisha anatabasamu)

Olivia: ah…Mimi nitakula chipsi na kuku na coca zero

Patrick: eeh…kuna watu hawanywi pombe kabisa…walokole

Olivia: umeanza uchokozi wako

Patrick: pole mama…(anacheka)

Olivia :( anajifanya kudeka)

(Wanacheka)

Monica: Na Mimi hivyo hivyo

Patrick: Mimi nataka ugali na samaki freshi kabisa najua ndo mahali pake hapa (anacheka)

Edwin: naomba ugali pia na nyama kavu

Mhudumu: sawa (anaondoka kuelekea jikoni)

Patrick: sasa…Edwin vipi brother?

Edwin :( anatabasamu huku macho yote yapo kwa Olivia) kuhusu nini…?

Patrick: Monica huyu hapa

Edwin: she is very beautiful…ningependa kuwa nae (anamuangalia Olivia Kama ni kwamba anamaanisha Olivia)

Patrick: she is mine…naona unamuangalia Sana Olivia

Edwin: hapana mi naongea tu wala simaanishi yeye…natamani ningekuwa na Monica

(Wote wanacheka)

Olivia: wow…hiyo nzuri--nimependa

Edwin :( anajisemea moyoni) ungejua kwamba nimevutiwa Na Olivia na nipo radhi kufanya kitu chochote ili niwe nae

Olivia: (Kwa Monica) vipi kuhusu wewe best…?

Monica: Ni mzuri hata Mimi ningependa kuwa nae

(Wote wanafurahi tena)

Monica :( anajisemea moyoni) nakupenda Patrick, nakupenda wewe tu…wewe ni mzuri sana

Patrick: kwahiyo Mimi na mke wangu tumewaunganisha marafiki zetu wawe mke na mume…

(Wote wanacheka)

Mhudumu :( analetea chakula mezani na kuwapa kila mtu jinsi alivyoagiza)

Patrick: sasa Leo wote mnaenda kulala kwangu, msidanganye maana kesho hakuna anayenda kazini…si ndio Olivia mama?

Olivia: yes...ni wazo zuri sana (kwa Monica na Edwin) eti mnalionaje?

Edwin: Ni wazo zuri

Olivia: ila ubaya sijamuaga mama…

Edwin: utamuaga tu…

Patrick: hakuna kitu kibaya kitakachotendeka hatukuui wala kukuchuna ngozi kuwa na Amani

Olivia: sawa sijakataa...ila mama ni lazima nimwambie

Patrick: nitamwambia

Olivia: usisahau…

Patrick: siwezi (anaendelea kula) siwezi kuacha kumwambia mama yangu mrembo yule

Olivia :( anaguna kisha anacheka)

Monica: kwahiyo mlikutana mtandaoni…

Patrick: yes…

Monica: hivi watu wanaokutana mitandaoni huwa wanadumu na wao?

Patrick: mapenzi ni upofu, unaweza ukampenda mwanamke uliyekutana nae njiani tu ukamsalimia akakuitikia vizuri ukamgeukia na kumuangalia ukajikuta unampenda sembuse iwe kwa watu wanakutana instagram wanachat sio chini ya mwaka mzima wataachaje kupendana

Edwin: mna bahati mmekutana…mkapendana, kuna watu wanakutana hivyo halafu wanadanganyana

Patrick: nampenda…she is just perfect for me na sioni wa kunifanya niachane nae

Edwin :( anaangalia chini)

Olivia: nakupenda pia my baby…

Patrick: asante love…

Monica; mapenzi mubashara eti eeh

Olivia :( anacheka)

Patrick: kuleni tuondoke maana tumekaa muda mrefu Sana

(Wanaendelea kula huku kila mmoja akionekana na furaha isipokuwa kwa Monica na Edwin maana mara nyingi wanaonyesha kuchukizwa na kitendo cha Olivia na Patrick kuonyesha mapenzi yao hadharani, wanaendelea kunywa na kula huku wakiburudika na miziki mbalimbali iliyokuwa ikisika mgahawani hapo)

Post a Comment

0 Comments