ON MY WEDDING DAY 10


 

SCENE 10: -

(Asubuhi ya kesho yake siku moja baada ya Monica kuja kumwambia Olivia maneno mengi yamhusuyo Patrick, Olivia amekaa sebuleni kwao huku akionekana hana raha hata kidogo na Mawazo mengi yanaonekana kuwepo kichwani kwake)

Olivia:(anajisemea moyoni)yaani wanaume(anasikitika kidogo)wapo kama wamezaliwa na mama mmoja yaani wana uongo mwingi sana mioyoni mwao sijui wana shida gani jamani(ananyamaza kidogo)yaani Patrick ni wa kunificha na kunidanganya kuwa hajawahi kufanya kosa lolote kwamba yeye ni msafi…yote hiyo ni uongo mkubwa yaani sitaki hata kumuona,alikuwa anauza madawa ambayo yana madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo na kuua kabisa inamaana Patrick ni muuaji…(anasikitika)kwahiyo ni muongo aliposema yeye ni mlokole alidanganya pia(anasikitika)

Mama :( anakuja mahali pale) Olivia… (Anakaa pembeni yake) nakuona tangu Jana huna raha nini tatizo mama yangu

Olivia: sina shida mama…kuwa na Amani mama mimi nipo poa tu mama usijali mama yangu

Mama: hauko sawa mrembo wangu

Olivia: wasiwasi wako tu mama

Mama: nimegundua kuwa tangu Monica aondoke umekosa raha kabisa mama, mimi ni mama yako nan do mtu na rafiki yako wa karibu na wa kweli naomba uniambie tafadhali

Olivia: Patrick…ni muuza madawa ya kulevya…sio kuuza tu anayatumia mama

Mama :( anabaki mdomo wazi) hapana Olivia huo ni uongo mkubwa…wewe nani amekwambia?

Olivia: Monica…ameambiwa na mpenzi wake ambae ni rafiki wa karibu wa Patrick…anasema lakini alikuwa anayauza zamani na mpaka akafungwa

Mama: sasa mwanangu hiyo si ilikuwa ni zamani kwani bado anayauza?

Olivia: hata Kama hayauzi mama ilikuwa ni jukumu lake kuniambia mi mbona sijamficha chochote? na isitoshe kwanini anaficha? inamaana anayauza bado...

Mama: Olivia…

(Anakatishwa na sauti ya kengele ya mlangoni)

Mama: nani tena?

Olivia: ngoja nikafungue (ananyanyuka kwenda kufungua) oh…Shem karibu…

Edwin: Asante…mambo vipi shemeji yangu.

Olivia: Safi… (Simu yake inaita anaiangalia anagundua kuwa ni Patrick anakata) karibu ndani shem

Edwin :( huku anaingia) Asante

Olivia :( simu inaita tena anaamua kuipokea) unasemaje Patrick…nimeshakuambia kuwa tuachane…sikutaki tena

Patrick: naomba nafasi nyingine nitayarekebisha yote hayo mke wangu…nakupenda Olivia…

Olivia: usiniite mke wako Patrick maana Mimi sio mke wako (anakata simu kwa hasira)

Mama: samahani Kwa kukuingilia lakini hivyo sio jinsi ya kumjibu mwanaume aliyekusaidia na mengi Olivia…nakuomba umuombe msamaha hata kama amekosea hutakiwi kumjibu hivyo

Olivia: hapana mama simuombi msamaha Patrick

Mama: Olivia...

Edwin:(anajisemea moyoni) huyu maza nae vipi…anataka kumshawishi Olivia amsikilize Patrick na akimsikiliza tu wanasamehana na kurudiana na mimi sitaki hivyo hata kidogo (kwa mama) shikamoo mama

Mama: marahaba baba hujambo na wewe ni…

Olivia: rafiki wa karibu wa Patrick

Mama: sawa karibu…ungependa nini asubuhi hii maji, kahawa, juisi au chai

Edwin: Asante mama ila mimi tayari nimeshakunywa chai, asante mama labda siku nyingine

Mama: sawa baba ngoja niwaache... (Anaondoka na kuingia chumbani kwake)

Edwin: iam so sorry…mi nilijua tayari Patrick keshakuambia kuwa alikuwa muuza na mtumiaji wa madawa ya kulevya ndo maana nikaropoka…samahani

Olivia: haina shida shemeji… (Anakaa kimya)

(Upande wa Patrick amekaa na Monica na Monica anaonekana kumpa faraja shemeji yake kwa kumshika bega)

Patrick :( anampigia tena Olivia) dah…hakuna mtu mbishi Kama Olivia…yaani mpaka aniruhusu kuongea nae ndo nitakuwa na Amani

Monica: yaani navyomjua rafiki yangu akishatema harudishi tena kinywani…yaani ni mbishi sana huyu mtoto

Patrick :( anaiweka simu sikioni inaita mwisho inapokelewa)

Monica :( anaongea kwa sauti ya mahaba Fulani kama mtu ambae yupo na mtu wake) Patrick…

Olivia: Oh, umenipigia simu kuniringishia kwamba una demu mpya kwamba unabandika na kubandua…ok baba maisha mema…

Patrick: come on Olivia…acha utoto basi…naomba unisikilize mpenzi wangu…

Olivia :( anakata simu Kwa hasira)

Edwin: nini tena?

Olivia: yupo na demu mwingine yaani bandika bandua…

Edwin :( anajisemea moyoni) good job Monica…sasa ngoja nicheze nafasi yangu…tuone yatatokea yapi… (Kwa Olivia) yaani hawezi kubadilika Patrick…bado tu ni playboy…si ana hela…?

Olivia: kwahiyo Mimi ananipigia ili iweje?

Edwin: labda Kama ulivyosema kuwa anajaribu kukuringishia kuwa humbabaishi kwa lolote ana pesa na akitaka mwanamke hata kutoka uarabuni anapata

Olivia :( anashikwa na hasira)

(Upande walipo Patrick na Monica)

Patrick: sijakuelewa kwanini umeniita Kwa hiyo sauti tena hasa pale ulipogundua kuwa Olivia kasha pokea simu?

Monica :( anacheka) Shem…una stress kaa utulie mi mbona nimekuita kawaida Sana

Patrick: hii ni mara ya pili unafanya vituko mara ya kwanza ulikuja jikoni kwangu umevaa khanga moja huku maungo yako yanaonekana vizuri na unajua mimi ni mwanaume…

Monica :( anacheka tena) shemeji bwana…Mimi sikujua Kama nitakukuta jikoni…kwani Mimi ni malaika kujua leo majira ya usiku nitamkuta shemeji yangu jikoni

Patrick :( anamkazia macho) Olivia ni mpenzi wangu na ni Mungu mwenyewe ndo kapanga awe wangu…na atakuwa mke wangu…sio wewe sio nani atakayeweza kunitenganisha na Olivia…haya nayo yatapita….na mimi na yeye tutakuwa wapenzi tena sio wapenzi tu wachumba ambao tutakuwa tayari kuoana

Monica :( anachukia Sana)

Patrick: sasa dada…kwanza sijui kwanini upo hapa ila wakati huu nataka uondoke na sitaki kukuona tena labda uje na Olivia na ikijitokeza hii tena nitamwambia Olivia…now…get out…

Monica: mi sina nia mbaya lakini

Patrick :( kwa sauti ya ukali kupita kiasi) leave…au huelewi? Ondoka mama yangu sitaki nikuone hapa mama…kabla sijachukia Zaidi toweka

Monica :( anatoka nje)

Halima: vipi mdogo wangu…tatizo nini…mbona umechukia Sana?

Patrick: nimegombana na Olivia na hanitaki tena…

Halima: kisa nini?

Agnes :( huku anakuja) ila mi Patrick ninakuambia kila mara tena tangu nimemuona huyu dada…yaani huyu dada ni kimeo ndo aliyekuharibia mahusiano yako na mpenzi wako

Halima: yaani siwaelewi kwani kuna nini?

Agnes: kuna mtu tena Nina uhakika kuwa ni huyu dada alienda kwa Olivia na kumwambia kuwa Patrick aliwahi kuuza madawa ya kulevya…na alikuwa anayatumia pia na kikubwa alifungwa…

Patrick :( yupo kimya)

Halima: na wewe huyo mpenzi wako bado ana akili za kitoto sasa hapo tatizo ni lipi mpaka likamfanya achukie na kukuacha

Agnes: Point Ni kwamba Olivia anasema kuwa Patrick hakumwambia Hilo

Halima: hamna bwana hizo ni hasira tu za kawaida zitaisha na atakupigia simu…sasa kilichokufanya umfukuze shemeji yako kama mbwa ni nini?

Patrick: huyu demu mjinga Sana…yaani Mimi naongea na Olivia yeye ananiita utasema mimi ni bwana wake…Olivia amekasirika kweli amedhani mimi nimeingiza mwanamke…

Halima: kumbe mjinga eeh…yaani

Agnes: mi nilimuona tu tangu mwanzo anakuja hapa yaani anamuonea wivu mwenzie bila hata kujificha…

Patrick: hanipati…kwanza dada zangu tunatakiwa tujiandae kwenda kumtolea Olivia mahari

Halima: hallloooooooooo

Agnes :( anapiga vigelegele) hayo ndo maneno leta mke hapa

Patrick :( anacheka) ILA sasa ndo nitafute namna ya kumrudisha huyo mke…kimke chenyewe kina hasira (anacheka) tufanye mpango turudishe jiko Hilo…lituivishie vyakula sie

Agnes: ndo hivyo…tufanye mpango arudi tu

Halima: atarudi tu, yaani wewe ukishindwa niite…

(Wote wanacheka)

Patrick: oh…Olivia my queen…hakuna wa kututenganisha

(Upande wa Olivia na Edwin)

Olivia: Shem…Kama hautojali naomba uniache nikae peke yangu…siko vizuri…

Edwin: sawa usijali my dear…na ukiwa na shida yoyote tafadhali niite…

Olivia: Asante

Edwin :( anatoka na kuondoka zake)

Olivia:(machozi yanamlenga)yaani Patrick ni wa kuniacha na kuchukua mwanamke mwingine hata siku mbili hazijaisha tangu tuachane kweli ng’ombe wa maskini hazai…(machozi yanamtoka)sawa bwana…na mimi Mungu atanijalia nitapata wa kunipenda…(anachukua simu yake na kufuta namba ya Patrick)maisha mema Patrick wangu…nakupenda lakini inaonekana huwezi kuacha tabia zako za kuchezea na kutupa wanawake kama takataka mara baada ya kuwachezea…yaani umenichezea mwisho umenitupa kama takataka(anaendelea kulia kimya kimya bila hata mama yake kujua kuwa analia)

Edwin:(amesimama dirishani anamchungulia Olivia kwa mbali) Olivia… (anacheka huku anatikisa kichwa) nimegongea msumali wa moto moyoni mwako nataka hasira zikupande ili umchukie Patrick na kunitaka mimi peke yangu

Olivia :( anaendelea kulia Sana)

Edwin: good job Monica…umenirahisishia kazi...Nitakuwa karibu Sana na Olivia kiasi cha kumfanya amsahau Patrick…nitamfanya aone kwamba mimi ndo mwanaume nimpendae kwa dhati na sio Patrick

Olivia :( anaangalia picha ya Patrick) Patrick but why baby…kwani nilikosa wapi badala uje tuyamalize wewe umeamua kuwa na mwanamke mwingine

Edwin :( anacheka Sana) oh… (Anapiga simu Kwa Monica)

(Simu inaita kisha inapokelewa)

Edwin: mchezo kwisha yaani hapa wala hawatatafutana tena…cheza nafasi yako vizuri usije ukapokonywa tonge mdomoni

Monica: usisahau kufanya hivyo pia(anacheka)

Post a Comment

0 Comments