MUNGU MKUU 26


 

SCENE 26: -

JIONI YAKE: -

(Wapendwa wa Miriam wamekusanyika nyumbani kwa Mr. Ken na mkewe wakisubiri hatima ya Miriam)

Ken: yaani kila sehemu tumemuangalia hatujamuona…sio sehemu ya tukio wala mochwari…(Analia)sijui nini kimemtokea huyu mtoto…sijui aliungua akabaki majivu (Analia sana) sielewi

Jeremy :( Analia Sana)

Ariana :( anajifanya kulia)

Keddy :( Analia)

Mary :( Analia Sana)

(Kwa mbali wanasikia geti linafunguliwa)

Ken: nani tena? Hatutaki wageni

Sauti :( Kama ya Miriam) ma mdogo nifungulie

Mary:(anashangaa) Miriam? (kwa wote) huyo ni Miriam? jamani nasikia sauti ya Miriam (anafuta machozi) jamani Miriam…

Sauti: da Ariana?

Ariana :( anashangaa) Miriam?

Ken :( ananyanyuka na kufungua mlango)

(Tazama ni Miriam, kila mmoja aliyekuwepo hapo anapigwa na butwaa)

Jeremy :( bila kutegemea anamkumbatia Miriam mbele ya wazazi) oh My God Miriam…Asante Mungu

Mary: MUNGU MKUU…haya ni maajabu yake

Ken: ulikuwa wapi Miriam embu kaa

Miriam: vipi kwani? (anaangalia nje) Vanessa, Naila njooni ndani

(Vanessa na Naila wanaingia ndani)

Jeremy: Naila...mlikuwa wapi nyie mmetutesa...

Miriam: tulikuwa chuoni

Ken: embu nihadithie mwanangu imekuwa vipi mpaka mpo hapa?

FLASHBACK

(Miriam na Naila wanapanda kwenye basi)

Miriam: yaani mimi unajua sijisikii kwenda hii trip

Naila: najua kwanini hutaki itakuwa kwasababu ya Vanessa

Miriam: wala sio utani haki ya Mungu yaani siwezi kabisa kwenda bila Vanessa na yeye sasa nampigia simu unadhani hata anapokea sijui ana janga gani

Naila: twende kwao

Miriam: halafu gari litatusubiri utasema gari la baba zetu?

Naila :( anacheka) wewe nae hata hivyo si hutaki kwenda trip kwanini tusiende kwa kina Vanessa hii wikiendi nyumbani watajua tupo trip kumbe tupo mjini hapa hapa

Miriam :( anacheka)

Naila: twende zetu

Miriam: let’s go

Naila :( Kwa dereva) anko tuache hapa

Dereva: kuna nini?

Miriam: wewe tushushe tu

Dereva: shukeni

(Wanashuka kwenye basi)

Dereva :( anawaona) naomba niwaambie kitu…yaani sisubiri ndege wa mtu hapa

Naila: nyie nendeni tu

Dereva: haya... (Anaondoa gari)

Miriam: ngoja basi nimwambie hata da Ariana kuwa sijaenda tour

Naila: tutawaambia tukifika kwa Vanessa

(Wanapanda daladala)

BAADA YA KAMA DAKIKA 15: -

(Naila na Miriam wanafika nyumbani kwa kina Vanessa)

Vanessa :( anawaona) karibuni nyie vimburu

Naila: yaani ungejua hatujaenda tour kwa ajili yako wewe kimbulu mchanga

Vanessa: Mimi si niliwaambia hamuwezi kwenda bila mimi, mimi nina vibe najua kuchangamsha

Miriam: halafu mbona hupokei simu?

Vanessa: nilikuwa nafua nimefua nguo utasema sijui nini yaani sasa hivi ndo nimemaliza kufua

Miriam: naomba maji ya kunywa kwanza

Vanessa: kaeni (anaelekea jikoni baada ya muda anarudi na glasi mbili za maji, moja anampa Miriam na nyingine anampa Naila)

Vanessa: sasa tupike halafu twende

Miriam: wapi?

Vanessa: kwenu…

Naila: sisi tumekuja kukaa mpaka kesho jioni…

Vanessa: be my guest

(Wanacheka)

Miriam: tuonyeshe pa kuanzia…halafu muziki tafadhali

Vanessa: una kichaa?

(Wanacheka na kufurahi, wanawasha muziki wanaanza kucheza na kuenjoi)

SAA NANE MCHANA: -

Miriam: sasa tumekula tumeshiba time for TV

Naila: weka ITV

Vanessa: sasa ya nini?

Naila: kuna marudio ya tamthilia ya wiki nzima

Vanessa:(anaweka)

(habari zilizotufikia hivi punde)

Naila: embu sikilizeni breaking news

Msoma habari: habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa basi lililokuwa limebeba wanafunzi wa chuo cha sheria waliokuwa wanaenda trip kwa ajili ya kujifunza limepinduka vibaya na kulipuka na kuuwa watu wote waliokuwemo humo

Miriam: My God…(anashangaa)Mungu ni Mkuu sana…MUNGU MKUU

Naila: kabisa…duh na sisi tusingemuwaza Vanessa tulikuwa tunakufa eeh Mungu

Miriam: twendeni chuo

(Wanatoka na kwenda chuoni)

END OF FLASHBACK

(Walipo Miriam na familia yake)

Miriam: ndo mambo yalikuwa hivyo

(Watu wanashusha pumzi na kumtukuza Mungu)

Ken: nina maswali…maana tulikuwa tumechanganyikiwa watu tumeshinda tunalia kama wajinga shemeji yako amelia kama mjinga

Miriam:(anacheka)

Ken: mbona simu yako ilikuwa haipatikani?

Miriam: simu ilizima chaji sikuwa na chaja kwa bahati mbaya niliacha chaja nyumbani

Naila: ila nakumbuka tulikuja sema mlikuwa hampo

Keddy: ndio kuna kipindi tulienda eneo la tukio

Mary :( anamkumbatia Miriam) namtukuza Mungu hata kwa hili leo amejidhihirishia ukuu wake, nimefurahi kukuona mwanangu…(anambusu)nakupenda sana mama

Miriam: asante ma mdogo, nakupenda pia ma mdogo(anatabasamu)

Jeremy:(anashusha pumzi) naona mimi niende maadamu Miriam amesharudi nina Amani sasa

Ken: haya baba…karibu tena (kwa Miriam) msindikize shemeji yako

Miriam: sawa baba (anaongoza njia)

Jeremy:(anamfuata nyuma)

(Wanafika nje)

Jeremy: I cried for you my love nilidhani nimekupoteza my queen

Miriam: comeon baby nilikupigia simu kutumia namba ya Naila mara nyingi sana

Jeremy: sikuiona…iam so sorry (anambusu mdomoni)

Miriam: tupo nyumbani na unajua hilo

Jeremy: iam so sorry

Ariana :( anawachungulia kupitia dirisha la chumbani kwake) hawa washenzi bora hata Miriam angekufa...ona wanavyojifanya kupendana

(Walipo Jeremy na Miriam)

Jeremy: I swear ningejiua, Kama ungekuwa ni mmoja wa wanafunzi waliokufa

Miriam :( anamuangalia usoni)

Jeremy: nini mbona unaniangalia hivyo?

Miriam: macho yako yamevimba kweli

Jeremy: nimelia, nimezimia yaani siku yangu imekuwa mbaya kweli…wazazi wangu wamesafiri ila nimewaambia yaani wamechanganyikiwa ila nikitoka hapa nitawapigia…tutafanya conference call nao

Miriam: iam so sorry baby nimewasumbua

Jeremy: it is okay (anatabasamu)

Miriam: haya nenda tutaongea

Jeremy: okay bye baby… (anaondoka)

Post a Comment

0 Comments