MUNGU MKUU 27


 

SCENE 27: -

BAADA YA WIKI MOJA: -

(Majira ya saa moja usiku, Ariana amesimama katika jumba Fulani ambalo linaonekana ni bovu na wala halina mtu anayeishi humo, amesimama anaonekana kama ni mtu anayesubiri kitu Fulani kwa hamu sana, baada ya kusimama kwa dakika kadhaa hatimaye mtu aliyekuwa anamsubiri kwa hamu si mwingine ni Miriam)

Miriam: dada yamekufika yapi mbona umeniita kwa haraka sana na mbona--- (anapashangaa) mbona tupo hapa?

Ariana :( anamuangalia kwa hasira mithili ya simba mwenye njaa anataka kumeza mtu au kitu)

Miriam :( anamshangaa) dada kuna tatizo?

Ariana: lipo…au nikuambie kuwa yapo? Mengi tu

Miriam :( anazidi kumshangaa) sikuelewi

Ariana: tangu umekuja maishani mwangu nimekuwa sina hata Amani (anatembeatembea)

Miriam: usiseme hivyo dada Mimi ni mdogo wako naanzaje kukukosesha amani?

Ariana :( anacheka kwa kejeli) eti mdogo wangu…nani alikuambia kuwa mimi ni dada yako (anacheka kwa dharau) wewe sio mtoto wa baba na mama yangu

Miriam :( anapigwa butwaa) eti?

Ariana: itika Miriam maana nimekuita…

Miriam: unanidanganya…dada kwanini unanichukia hivyo (analengwa na machozi)

Ariana: nakuchukia sio kidogo wewe Malaya…tangu wazazi wangu wamekuokota nje ya mlango wetu…umekuwa ni kuzuizi cha furaha yangu wazazi wangu wamekuwa wakikupenda wewe Zaidi ya mimi…haya nilipopata mchumba nae ukamchukua…

Miriam: dada kuhusu Jeremy si tumeshamaliza? Wewe si ulisema huna pingamizi na mahusiano yetu

Ariana: wewe ni mshenzi, muuaji Malaya unayetafuta njia yoyote kuharibu furaha za watu...Upo Kama mama yako

Miriam: mama yangu ni nani kama mama yangu si mama yangu

Ariana: mama yako ni Mary

Miriam: ma mdogo Mary?

Ariana: ndo hivyo

Miriam: ulijuaje? na kwanini unaniambia hivyo leo?

Ariana: mama yako ni fala kama wewe tu…aliniambia mwenyewe sasa sijui ili iweje? (Anacheka kwa dharau)

Miriam :( Analia) lakini dada Ariana...

Ariana: bado najibu maswali yako...Umeniuliza kwanini nakuambia haya sababu wewe Leo unaenda kufa mshenzi wewe

Miriam: usinifanyie Mimi hivyo dada pamoja na kwamba umesema kuwa mimi sio mdogo wako lakini tumekuwa pamoja tumelelewa kama ndugu kabisa dada sasa leo hii ukitaka kuniua

Ariana: utafanya nini?

Miriam: sina cha kukufanya

Ariana :( anapiga makofi mara mbili)

(Wanakuja wanaume wawili walioshiba vizuri kwa lugha nyingine mabaunsa)

Ariana: pigeni hii mbuzi mpaka muue sina hasara… (Anavuta kiti kisha anakaa)

Miriam :( anamuangalia kwa huzuni) dada

Ariana: :( anacheka) unaumia mwenyewe…unaogopa? (Anacheka kisha anakunja uso ghafla) hata mimi naumiaga Zaidi na Zaidi nikikuona wewe na Jeremy

Miriam :( Analia) dada jamani

Ariana :( Kwa mabaunsa) pigeni huyo…

(Mabaunsa wanachukua fimbo kubwa kila mmoja wao na kuanza kumpiga Miriam bila huruma)

Miriam :( Analia) dada… (Anamuangalia Ariana usoni) dada…

Ariana: nakuchukia Sana yaani kufa mshenzi wewe

Miriam: dada …naumia (analia)

(Mabaunsa wanaendelea kumpiga)

Miriam :( anatoka damu puani)

(Simu ya Miriam inaita)

Ariana:(anampokonya) nani(anaangalia)eti king bae(anafyonza)huna hata haya… (kwa baunsa mmoja) embu njoo…unaona hii simu ijibu…mjibu vibaya sana…mwambie wewe ni mpenzi wa Miriam na hapa mlipo mnakula starehe asiwasumbue mwambie pia unajua yeye ni sponsa amenunua gari na yupo mbioni kununua nyumba

Miriam :( anasikitika Sana)

Ariana :( Kwa baunsa) kaongelee kwenye utulivu

Baunsa :( anaipokea simu huku anaelekea sehemu tulivu kidogo) hello? Nani?

Jeremy :( anashangaa) wewe ni nani umeshika simu ya mke wangu?

Baunsa :( anacheka kwa dharau) eti mke wako…huna hata haya wewe mshenzi...Miriam ni mke wangu kaka oh nimekumbuka wewe ndo yule sponsa wake uliyemnunulia gari na upo kwenye mchakato wa kumnunulia nyumba…oh My God sponsa tunashukuru kwa upendo wako…haya kama hutojali jifunze kuheshimu wapenzi wa watu wewe kwa Miriam ni sponsa tu

Jeremy: Mimi sio sponsa braza wewe ndo sponsa kwa taarifa yako

Baunsa :( anacheka kidogo) embu achana na mpenzi wangu wewe… (Anakata simu)

Jeremy: hello

(Simu imekatwa)

Jeremy :( anapiga ukuta Kwa hasira) shit…damn this woman!!!!…Miriam ni wa kunifanyia hivi mimi jamani…I hate her… (Anatupa simu pembeni Kwa hasira)

(Upande walipo Ariana, mabaunsa na Miriam)

Ariana :( kwa baunsa) umenipa raha sana...na mimi lazima nikupe raha baby...Twendeni disco halafu baadae tutaenda kulala pamoja

Baunsa 1 :( anatabasamu) sawa boss...

Ariana: ila nitafurahi na kuwapa wote raha mkimuua huyu mjinga

Miriam :( amelegea hana hali nzuri)

Baunsa 2 :( anampiga)

Miriam :( anazimia)

Ariana: kafa…kafa (anashangilia) kafaaaaa… (Anaenda kumuangalia)

Miriam: (ametulia)

Baunsa 1: hajafa kazimia tu

Ariana :( anachukua chupa ya maji anammiminia Miriam) amka wewe usijifanye umekufa (kwa baunsa 1) baby umenifurahisha...Nipe mkanda wako mara moja

Baunsa 1 :( anavua mkanda na kumpa Ariana)

Ariana :( anaupokea na kumnyongea Miriam kwa nguvu zake zote)

(Mabaunsa wanampa moyo kwa kumshangilia)

Baunsa 1: ndo maana yake mama…fanya mambo mama

Ariana :( anamnyonga mdogo wake kwa nguvu zake zote)

Miriam :( anatapatapa Kama mtu aliyezama kwenye maji na kukosa pumzi)

Baunsa 2: uaa huyo hana adabu…uaaaaa

Ariana :( anaendelea kumkaba)

Miriam :( hatimaye anaishiwa nguvu na kutulia)

Ariana :( ananyanyuka) Safi...Haya twendeni, atakuwa amekufa sasa

Baunsa 1: tukamzike...

Ariana: tusihangaike…tuondoke

Baunsa 1: ulale pema peponi mrembo(anacheka)

(Wanaondoka na kumuacha Miriam akiwa hajitingishi)

Post a Comment

0 Comments