SCENE
25: -
(Majira
ya saa nane mchana wa siku hiyohiyo Jeremy yupo ofisini kwake anaonekana
kuhangaika kupiga simu)
Anita :(
anaingia alipo Jeremy) boss vipi? Mbona kama una kitu kinakusumbua?
Jeremy:
simpati Miriam…sijui kwanini (anajaribu tena)
Anita :(
anaguna) unaonekana yaani hujazoea kukaa masaa mengi bila kumpata my
lady wako
Jeremy:
exactly Anita yaani kuongea nae ni mfano wa dozi yaani asubuhi mchana na usiku
bila kukosa
Anita: (anacheka)
Jeremy:
wewe embu acha nipambane nimpate ananichanganya huyu jamani
(Simu
haipatikani)
Jeremy:
jamani huyu mtu yuko wapi?
Anita:
hata TV hutaki kuangalia (anawasha runinga)
(Habari
zilizotufikia hivi punde)
Jeremy:
embu sogea tuone hiyo habari
Msoma
habari: basi lililobeba wanafunzi wa chuo cha sheria limepinduka vibaya na
kulipuka na kuua wanafunzi wote…
Jeremy :(
anapiga kelele) Miriam… (Analia Sana) jamani mpenzi wangu…Miriam…Miriam
wangu…Miriam No…No... No…no Miriam baby but why God why? (analia sana)
Anita:
Mungu wangu (anazima runinga)
Jeremy:
(anazimia)
Anita:
boss…boss…boss (anatoka nje kuomba msaada) jamani naombeni msaada boss kazimia
huku…
(Watu wanakuja kumsaidia Jeremy)
Kaka 1:
boss
(Upande
wa familia ya kina Miriam, kama ilivyo kwa Jeremy nao wana wasiwasi juu ya Miriam)
Mary:
mbona Miriam hana tabia ya kuacha kupiga simu tangu asubuhi hajatupigia simu
kutuambia kama kafika au kakwama
Ken:
yaani hata sijui jamani huyu mtoto
Ariana
:( anajisemea moyoni) si afie huko (anafyonza)
Keddy:
maskini mwanangu…sijui amepatwa na nini asipige simu
(Jirani
mmoja anakuja)
Jirani: hodi
jamani Habari za hapa jamani (anaonekana ana wasiwasi sana) hivi yule
binti yenu mdogo si alikuwa anasafiri kwenye basi Fulani sijui walikuwa
wanaenda kwenye masomo
Keddy:
ndio kwani vipi?
Jirani:
nimesikia kwenye habari kuwa basi limepinduka na kuua wanafunzi wote
Mary :( anapiga
kelele) mwanangu (Analia Sana)
Keddy:
mwanangu… (Analia Sana)
Ken :( anapata
shinikizo la moyo) ah
Ariana:
baba…baba (anamuwahi baba yake) Mungu wangu… (Anakimbilia chumbani
kwa baba yake anachukua vidonge vyake vya presha) Mungu ananipenda…yaani
sijafanya chochote Miriam kafa... (Anacheka) sasa kila kitu kitakuwa cha
kwangu peke yangu (anarudi sebuleni) baba...Kunywa vidonge vyako baba (analeta
maji ya kunywa) kunywa baba utulie baba yangu
Ken :(
anakunywa) Asante mwanangu (anainuka kidogo) Ariana embu mpigie
mdogo wako simu muulize yuko wapi mbona anachelewa kurudi nyumbani
bwana…mwambie tunaogopa (anaanza kulia) mwanangu hawezi kuwa amekufa
jamani… (Analia) hawezi kuwa amekufa jamani
Jirani:
yaani baba Ariana yaani wamesema kuwa wanafunzi wote waliokuwepo wote
wamekufa…yaani gari limelipuka...Na unavyoujua moto huwa hubakizi mtu yaani
kwanza hapa watu wameshafika kuangalia miili ya watoto wao
Ken :( Kwa
mkewe) twende mama Ariana…twende tukaangalie mwili wa Miriam wetu kama
utakuwepo
Ariana:
baba hali yako sio nzuri kwanini usitulie tu
Ken:
niache Ariana nataka nikamuone mwanangu nataka kumuona Miriam wangu mwanangu...Niletee
ufunguo wa gari haraka
Ariana
:( anakimbia ndani kuuchukua ufunguo wa gari) huu hapa baba ila utaweza
kuendesha acha niendeshe
Ken:
sawa ila fanya haraka
(Familia
nzima wanaelekea kwenye gari tayari kwa ajili ya kwenda eneo la tukio la ajali
mbaya ya gari lililogharimu maisha ya wanafunzi)
Mary:(Analia
sana) Miriam… (anajisemea moyoni) Mungu onekana baba yangu, onyesha
ukuu wako mfalme wa Amani mwanangu hawezi kuwa amefariki tena kabla hajajua
kuwa mimi ndo mama niliyemzaa (Analia)Mungu nakulilia leo Mungu
wangu…namhitaji mwanangu Mungu wangu
Ariana
:( anajisemea moyoni) mapigo Kama haya huwatokea wenye dhambi tu (anacheka
moyoni) yeye aliniibia bwana Mungu kampa pigo… (Anaendelea kujisemea
moyoni) sijafanya chochote ila Mungu ameshaniondolea pingamizi (anacheka
moyoni)
Ken:
Ariana bado hatujafika tu?
Ariana:
baba tulia...
(Safari
inaendelea na baada ya mwendo wa dakika kadhaa wanafika eneo la tukio)
Ariana:
watu ni wengi
Ken :(bila
kupoteza muda anatoka kwenye gari na kukimbilia ilipo miili ya wanafunzi)
Miriam… (anamuona Jeremy) Jeremy...Shemeji yako (Analia)
Jeremy
:( macho yamevimba kwasababu ya kulia sana) baba…
Ken:
mbona uko hapa? baba kuna ndugu yako
Jeremy:(machozi
yanamtoka kwa wingi) hapana baba…nimekuja kumtafuta Miriam
Ariana:(anaingilia)
amekuja kumuona shemeji yake...
Ken: oh,
una roho nzuri sana baba...
(Jeremy
na Ariana wanaangaliana)
Ken:
sasa hapa umemuona?
Jeremy:(bado
machozi yanamtiririka) sijamuona baba
(Mary
na Keddy wanakuja walipo)
Keddy: Jeremy...upo
hapa baba
Jeremy :(
Analia kwa uchungu)
Ken:
mbona una uchungu sana Jeremy una shida gani?
Jeremy:
sina shida baba…
Ariana:
walikuwa wana mahusiano mazuri na shemeji yake naona ni mshtuko tu huo…
Jeremy:ni
kweli baba ni mshtuko tu
Ken: oh
sawa…mwanangu… (Anaangaliangalia) inamaana hawa ndo wanafunzi
waliokuwepo?
Jeremy:
inavyoonyesha
Ken:
basi baba usilie bwana unajua umelia Sana ni wakati wako sasa kutulia kwani
polisi wanasemaje?
Jeremy:
hawajasema kitu…
Ken: dah
Keddy:
labda twende mochwari sasa hapa hata hatumuoni Miriam
Mary :( Kwa
keddy) dada tuendelee kumuangalia
Keddy:
hayupo hapa …Miriam hayupo hapa angekuwepo tungemuona Mary
Mary :( Analia)
Miriam uko wapi mwanangu…uko wapi mama?
Jeremy
:( Analia kwa uchungu)
Ken :( Kwa
Jeremy na Mary) mbona mnaonekana mna uchungu kuliko sisi?
Keddy:
baba Ariana maswali gani hayo? Kila mtu anajua kuubeba uchungu wao…waache hiyo
ndo jinsi wanavyobeba uchungu wao…
Ken:(anashusha
pumzi) sawa haya twendeni huko mochwari
(Familia inaondoka kuelekea mochwari)
0 Comments