IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 60 (MWISHO)

 

SCENE 60:-


FINALE: -

BAADA YA MIEZI TISA: -

(Ni mchana mwingine mtulivu, maisha yanaonekana kuendelea vizuri, Angelina ambae sasa ni mama mwenye nyumba ile ya kifahari anaonekana ni mama mjamzito ambae anaweza kujifungua wakati wowote, anajikongoja taratibu kwenda jikoni)

Angelina: Esther mdogo wangu naomba chai yaani nasikia tumbo linauma kweli (anaugulia)

Esther :( msichana wa kazi) sawa dada…nikupashie maji pia?

Angelina: nimeshajimwagia maji si kuna hita bafuni…wewe nipe chai (anasikia maumivu) maamaaaaa...Esther muite shemeji yako…mpigie simu (anaanza kulia) naumia (anakaa chini sakafuni)

Esther: dada nini tena?

Angelina: naumia, tumbo linauma sana…muite Rama…

Esther :( anakimbia) kaka Rama…kaka Rama

Ramadhani: nini tena?

Esther: njoo dada anaumwa?

Ramadhani :( huku anakimbilia ndani) mpigie Ray simu haraka

Esther :( anachukua simu iliyopo getini na kupiga namba ya Raymond) shemeji…shemeji dada anaumwa tumbo

Raymond: kafanyaje…nakuja sasa hivi (anakata simu kisha anatoka nje anapanda gari na kuliondoa haraka)

(Upande wa kina Angelina)

Angelina: mama (anasugua mapaja) inauma Sana…inauma Sana jamani acheni

Esther :( anakuja akitokea nje) shemeji anakuja

Angelina: nyie hapana naomba twendeni atatukuta hospitali jamani…twendeni tumkute kwanza hukohuko nyie hamjua tu maumivu ninayoyapata

Esther: kaka Ramadhani, huu hapa ufunguo wa gari…tumpeleke

(Catherine, Edmond, Christina na Peter wanafika)

Christina: jamani Raymond kanipigia simu anasema huyu kapata uchungu…sasa mbona mmesimama tu?

Angelina: nisaidieni jamani nakufaaaa

Catherine: kufa hufi Mimi mwenyewe niliipata freshi miezi miwili iliyopita wewe usijali bwana utakuwa sawa

Christina: kabisa hata Mimi nilijipa moyo sasa hivi Nina libaba langu akha mwenyewe sina shida

Peter: mnaongea Sana mwenzenu anaumwa Sana

Catherine: tunampa moyo

(Raymond anafika akiwa anaonekana amepaniki)

Edmond: embu tulia

Raymond :( Kwa Angelina) mke wangu (anambeba na kumpeleka kwenye gari) naelekea hospitali kwangu

(Edmond, Catherine, Christina, Peter, Ramadhani na Esther wanapanda magari waliokuja nayo na kumfuata Raymond nyuma.)

Raymond :( akiwa anaendesha gari Kwa kasi Sana) basi mke wangu vumilia tunafika sasa hivi hospitali

Angelina: Ray…fanya haraka

Raymond: najitahidi mke wangu

(Raymond anaendelea kuendesha gari Kwa kasi kubwa Sana na baada ya mwendo kidogo hatimaye wanafika katika hospitali kubwa ya Raymond.)

Raymond :( anashuka kwenye gari haraka anambeba mkewe kisha anaingia nae ndani) jamani nyie mpo wapi…huyu chupa imeshapasuka

Nesi: jamani mke wa bosi chupa imeshapasuka

Angelina :( anaishiwa nguvu)

Raymond: comeon baby…you can do it…jitahidi mama…you can do it

(Madaktari, pamoja na manesi wanakuja na machela na kumbeba Angelina na kumkimbiza katika wodi ya wazazi)

Daktari :( Kwa Raymond) tulia dokta Leo acha tufanye wenyewe… (Anaondoka na kuelekea walipompeleka Angelina)

(Edmond, Catherine, peter, Christina, Esther na Ramadhani wanafika aliposimama Raymond)

Edmond: vipi Mond?

Raymond: ameingia leba…

(Mr and Mrs Bembele nao wanafika)

Mr. Bembele: hamjambo

Wote: hatujambo shikamoo…

Mrs.Bembele: hamjambo?

Wote: hatujambo shikamoo

Mr & Mrs. Bembele: marahaba

Mrs.Bembele: vipi huyo anaendeleaje?

Raymond: ndo ameingia leba…chupa tayari imeshapasuka

Mr. Bembele: huyo tayari keshaleta habari njema

(Wanacheka)

Raymond :( anaonekana kuwa na wasiwasi sana, anazungukazunguka mara achungulie dirishani, mara atake kuingia ndani ya chumba hicho)

(Upande wa Angelina kazi imeanza, anajitahidi kusukuma kwa nguvu zake zote)

Daktari: shemeji jitahidi…

Angelina :( anajitahidi kusukuma kwa nguvu na hatimaye anajifungua)

(Mmoja wa madaktari anatoka nje ya chumba hicho akiwa na furaha sana)

Daktari: hongereni Sana…shemeji amejifungua salama, mapacha wa kike na wa kiume

Raymond :( anashangilia kisha Analia kwa furaha sana)

Mr. Bembele: Asante Mungu…

Mrs.Bembele: Asante Mungu…mkwe kaniletea mke mwenza na mume…loh kaniweza (anajikuta Analia kwa furaha huku anamkumbatia mume na mwanae)

Christina :( anafurahi pia)

Peter :( anafurahi)

Catherine: wow…mdogo wangu kawa mama wa watoto wawili kwa mkupuo…

Edmond :( anamkumbatia Raymond) hongera Sana Mond…umekuwa baba sasa uache kudeka

(Wanacheka)

Angelina :( akiwa anasaidiwa na manesi anatoka nje ya chumba kile na kuelekea kwenye chumba cha mapumziko)

Raymond :( anamkimbilia mkewe na kumkumbatia) asante sana wife…asante mno mke wangu (anambusu mfululizo)

Angelina :( sauti ya kuchoka) utaniangusha (anacheka)

Raymond: pole honey…

(Wote Kwa pamoja wanaenda kumsindikiza Angelina mpaka kwenye kitanda cha mapumziko watoto wake mapacha wanawekwa pembeni yake)

Mr. Bembele: hongera Sana binti yangu

Angelina :( anatabasamu) Asante baba

Mrs.Bembele: wow…hongera Sana mama…Asante Kwa kuniletea mke mwenza na mume, loh!!Wewe nae umeniweza

(Wote waliopo wanaangua kicheko)

Raymond :( anarekodi tukio kwenye simu yake)

Christina: watoto wataitwa nani na nani?

(Raymond na Angelina wanaangaliana kisha wanacheka)

Raymond: wa kike ataitwa Angelica na wa Kiume ataitwa Reynolds

Mr. Bembele: eeh mi nikajua mmoja ataitwa Glory na mwingine Desmond…

Raymond: ah acha waitwe hivyo

Edmond: hayo majina mbona ya kizungu Sana tutakuwa tunawaitaje?

Catherine:si Anje na Ray?

Peter :( anashangaa) halafu watoto wanaitwa Kama wazazi wao ee

Raymond: Asante Peter Kwa kuwa wa kwanza kugundua hilo…

Catherine: anje mama Anje, na Ray baba Ray…wow…jamani

Mrs.Bembele: jamani inapendeza Sana hapo ukute mlipanga hata kabla ya kuzaa hawa watoto wa siku hizi

Raymond na Angelina :( wanacheka)

Mrs.Bembele: Mama Angelina hajapewa habari hizi… (Anachukua simu kisha anampigia video call mama Angelina)

(Simu inaita)

Mama Angelina :( anapokea) hello…

Mrs.Bembele: hongera Sana ndugu yangu Angelina kajifungua

Mama Angelina :( anafurahi Sana) mtoto gani?

Mrs.Bembele: wa kike na wa kiume

Mama Angelina: mapacha?

Raymond :( anaingilia) Raynolds na Angelica

Mama Angelina: Angelina na Raymond…? Jamani hayo si majina yenu wewe na mkeo

Mrs.Bembele: nakwambia…

Mama Angelina: basi asanteni Sana nitakuja kuwaona jamani

Mrs.Bembele: sawa mama (anakata simu)

Raymond: jamani selfieeee

(Wanakaa vizuri na kupiga picha ya pamoja)

Mr. Bembele :( anawabeba watoto wale mapacha) Edmond nipige picha na wajukuu zangu

(Wafanyakazi wa Raymond wa hospitali hiyo wanawavamia ndani)

Nesi: tunataka tupige picha

Glory: jamani hongereni…

Angelina :( anatabasamu) Asante Sana

Pendo: watoto wanaitwa kina nani?

Edmond: Anje na Ray…

(Watu wanaendelea kufurahia pamoja wengine wanawabeba watoto huku Raymond akijisemea myoni)

Raymond:hivi ndivyo maisha yangu yalivyogeuka kuwa…maisha yangu yamekuwa ni ya furaha sana,nilichagua kuufuata moyo wangu hata pale akili yangu ilipokataa kunipa ushirikiano…nilikutana na mke wangu Angelina katika mazingira ya kawaida sana,siku moja mara baada ya kuchoka kazi za nyumbani pamoja na kazi za ofisini,niliomba msaada kwa rafiki yangu kipenzi Edmond wa kunitafutia msichana wa kazi,nae hakusita akanipatia msichana wa kazi…moyo wangu uliripuka mara baada ya kumuona binti yule nafsi yangu haikujali kama ni  binti wa hadhi ya chini au lah…niliupa moyo wangu nafasi ya kumpenda,sikujali nani wala nani nilimpenda na  leo hii nina furaha ya kwamba sikusita kumpenda mke wangu , najiona ni mwanaume mwenye bahati sana kuwa na mwanamke kama Angelina,mimi nay eye tulitofautiana matabaka lakini hiyo haikutuzuia kuwa wamoja na leo mimi nay eye ni baba na mama wa watoto mapacha Raynolds na Angelica.it was nice falling in love with my housegirl..She turned to be perfect for me…forever I will be proud to tell everyone that I fell in love with my housegirl…I love you Angelina,I love my kids,I love all my friends and my parents

Angelina :( anamshika bega mumewe) unawaza nini baba Ray…

Raymond :( anavuta pumzi ndefu huku anaangalia watu wote waliopo hapo) love doesn’t ask why…inatokea tu wakati wowote na katika mazingira yoyote…haichagua kabila, dini, tabaka wala nini. Ikija inakuja na hatuna budi kupokea zawadi hiyo. Nilikutana na mke wangu akiwa hana kitu chochote tabaka lake na langu vilikuwa ni vitu viwili tofauti

Watu :( wanamsikiliza Kwa makini)

Raymond: ilitokea tu…niliamua kuipokea zawadi hiyo na leo hii imenipa furaha ya ajabu (anambusu mkewe kwenye paji la uso) My Angelina, mama Angelica (anatabasamu)

Watu: wow… (Wanapiga makofi)

Mr. Bembele: wow…overall, we are all happy…si ndio jamani wote si tuna Amani?

Watu: ndio

Mr. Bembele: love is most beautiful thing…

Edmond: selfiiiiieeeee

(wote wanajipanga kupiga picha ya pamoja, wanaonekana kufurahi sana na kila mmoja anaonekana hana kinyongo, kuna pongezi na Amani mahali hapo, watu wanatabasamu, wanacheka kila kitu kipo safi.)

WRITTEN BY: MARYGLORY SEVERINE KIWANGO (VIDYA)

THE END

 

Post a Comment

0 Comments