IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 59

 


SCENE 59: -

SHEREHE YA HARUSI YA ANGELINA NA RAYMOND UKUMBINI: -

(jioni tulivu,kuna manyunyu Fulani ya mvua,watu wengi sana jamaa,ndugu,marafiki hata majirani wa Angelina na Raymond wamekusanyika katika ukumbi mkubwa tena wa kifahari kuliko kumbi zote jijini hapo,watu wanakunywa,wanafurahi kabla ya sherehe yenyewe kuanza,miongoni mwa matukio ni tukio la red carpet kabla ya mambo yote,watu wanapita wakiwa wamependeza katika zuria jekundu lililowekwa kwa ajili ya wageni wote.Nyuma ya jukwaa la mahojiano kumebandikwa picha kubwa sana yenye sura za Angelina na mumewe na kuna maneno yameandikwa “welcome to wedding reception of Raymond and Angelina)

Mtangazaji: wow… (anaangalia camera) karibuni mabibi na mabwana katika sherehe ya harusi ya Angelina na Raymond, kwa kuanza kabisa naomba nipige stori mbili tatu na wageni waalikwa kabla hawajaingia ukumbini kushuhudia yaliyo humo (anamgeukia mgeni wa kwanza ambae ni Christina) wow…dada mambo

Christina: poa…

Mtangazaji: umependeza Sana

Christina: Asante Sana…

Mtangazaji: kwanza kabisa tuanze na kichwani nywele tamu hiyo toka wapi?

Christina: hii nywele tamu toka nywele classic wapo Kariakoo msimbazi mkabala na big born sheli

Mtangazaji: wow…na nani kakuvalisha?

Christina: nimevalishwa na gauni pambe pia wapo Kariakoo…

Mtangazaji: barabara kabisa…na pochi nzuri toka wapi?

Christina: pochi nzuri hii toka jumba la pochi nao wapo Kariakoo

Mtangazaji: Safi na kucha nani kakutengeneza?

Christina: mwenyewe (anacheka)

Mtangazaji: na viatu…

Christina: shoes online

Mtangazaji: Safi na (anamuangalia Peter aliyekuwa amesimama pembeni ya mkewe) na kaka hapo umependeza sana

Peter: Asante Sana…

Mtangazaji: unajisikiaje kuwa mmoja wa wageni waalikwa leo kwenye harusi kubwa inayotikisa Dar?

Peter: najisikia vizuri na furaha pia…kuwa miongoni mwa wageni waalikwa kwenye hafla ya kuwapongeza ndugu zetu kwa kufunga ndoa

Mtangazaji: Asante Sana...Karibuni mburudike (anaenda Kwa wazazi wa Raymond) shikamooni

Wazazi: marahaba...

Mtangazaji: mmependeza

Wazazi: Asante Sana

Mtangazaji: mnajisikiaje kuwa katika sherehe hii?

Mr. Bembele: Nina furaha tu toka asubuhi mchana na mpaka sasa hivi mwanangu kaoa nina furaha sana

Mtangazaji: oh, kumbe wewe ni baba wa bwana harusi?

Mr. Bembele: ndio…we huoni chata hii

Mtangazaji: nawaona…kweli mmefanana Sana

Mr. Bembele: ndo hivyo

Mtangazaji :( anacheka kidogo) basi sawa haina shida karibuni ukumbini

Wazazi: Asante Sana (wanaingia ukumbini)

(Mtangazaji anaendelea kuhoji watu mbalimbali ikiwemo ndugu zake Angelina na marafiki waliokuja kuungana pamoja katika hafla ya kuwapongeza maharusi wa siku hiyo, mahojiano yanaendelea kwa muda na hatimaye wanaisha na kila mtu akiwemo cameraman na mtangazaji wanahamia ukumbini. Ukumbi umependeza sio mchezo na unang’aa kweli kweli na watu wanaonekana kwa uzuri kabisa. Kila mtu anaonekana kufurahi sana)

Mc: jamani mnafuraha nyie

(Watu wanacheka)

Mc: kwanini sasa?

Watu: Raymond kaoa…

Mc: kumbe???Sikujua naona tu shamrashamra watu hawatulii makamera mpaka juu ya vichwa vyetu kumbe Ray ameoa? Basi sawa bila kupoteza wakati mtakuwa nami mc wenu, mc mjanja kuliko hao wote Mc Rugemalira…yaani Mc Ruge…pigeni basi makofi

Watu :( wanapiga makofi)

Mc: basi sawa naomba niuruhusu msafara wa maharusi wetu…waingie ukumbini…Dj fanya yako baba

(unapigwa muziki mzuri na msafara wa maharusi yaani mabrighter wakike na wa kiume wanaingia wakiwa wanacheza vizuri sana, miongoni mwa mabrighter wa kike ni wadogo zake Angelina na wa kiume yupo mdogo wa Angelina pia, wanacheza vizuri sana na watu wanawashangilia sana, wanacheza na mwisho wanafika mbele)

Mc: Dj tulia kidogo… (Kwa watu) jamani wamependeza hawajapendeza?

Watu: wamependezaaaaaaa

Mc :( Kwa Dj) niletee matron Na bestman tafadhali

(Dj anaachia muziki mzuri na Edmond pamoja na mkewe wanaingia wanacheza kwa madaha yote, kama ilivyo kawaida ya watu wanacheza na kufurahi sana, wanashangilia sana. Edmond wanasakata rhumba mpaka wanafika mbele wanapofika mbele wanasimama kusubiri maharusi waingie)

Mc:(kwa Dj) kamatia hapo (kwa Edmond na mkewe) mmependeza…

Edmond na Catherine: asante (wanatabasamu) asante sana…

Mc: basi sasa ni wakati wa kuwakaribisha bibi na bwana harusi… (Kwa Dj) embu niletee hao waliotufanya tukutane pamoja hapa leo

Dj :( anaachia wimbo mzuri Sana unaoendana nao)

(Maharusi wanaingia wakiwa wamebadili nguo tofauti na zile walizokuwa wamevaa asubuhi wakati wa kufunga ndoa, Angelina amevaa gauni aina ya nguva lililombana vyema na kumonyesha umbo vizuri na pia lina mkia mrefu kiatu alichovaa ni kirefu sana,mtoto wa Kihangaza ameng’aa ukimuangalia kweli unakubali,kwa upande wa amevaa suti aina ya taxedo ya rangi ya kijivu na kiatu cheusi amependeza.Maharusi hao wanaingia wakiwa wanacheza kwa furaha sana na kufanya kila mtu atambue kuwa wana furaha ya kuwa mume na mke.Baada ya kucheza kwa madoido kwa muda kidogo hatimaye wanafika mbele,wanapokelewa na mabrighters,wanaowasindikiza karibu kabisa na meza yao yaani High Table)

Mc:(anashusha pumzi kidogo) kwani bibi harusi wewe kabila gani?

Angelina: mhangaza...

Mc: ndo wazuri hivyo…He!!Naoa wahangaza mie…cha kufia nini?

(Watu ikiwemo Angelina mwenyewe wanacheka)

Mc: basi sawa…kabla hatujapoteza muda Zaidi kuna kamchezo fulani tunaenda kucheza hapa kabla ya utambulisho na kila kitu…huo mchezo unaitwa (anavuta viti viwili) shoe game…nyie maharusi njooni make hapa…vueni viatu, wewe bibi harusi shika kiatu kimoja cha mumeo na chako na wewe bwana harusi shika chako na cha mkeo

Maharusi :( wanafanya Kama walivyoambiwa)

Mc: nyinyi mabrighter kaeni jamani muenjoi…hii ni harusi ya masteringi…

(Watu wanacheka)

Mc :( kwa maharusi) mko tayari kwa mchezo huu? (kwa watu) mko tayari?

Watu: tuko tayariiiii

Mc: Safi…naanza, iko hivi nikiuliza swali Kama jibu ni bibi harusi mnanyoosha kiatu cha bibi harusi na jibu kama ni bwana harusi basi kiatu cha bwana harusi kinanyooshwa…haya tunaanza

Maharusi: tuanze

Mc: swali la kwanza, nani alikuwa wa kwanza kumpenda mwenzie?

Angelina:(ananyoosha kiatu chake)

Raymond :( ananyoosha kiatu chake)

Mc: hakuna kuangalia nyuma (anashangaa) kwahiyo jibu ni bibi na bwana harusi… (Anaguna) kwahiyo wote mlianza kupendana

Raymond: Mimi ndo nilianza

(Watu wanacheka)

Mc: nani alianza kumwambia mwenzie hisia zake?

Maharusi :( wananyanyua kiatu cha Raymond Kwa pamoja)

Mc: wow…swali lingine…nani kati yenu ni mbishi jamani yaani akibisha hata dagaa haoni ndani

Maharusi :( wananyanyua kiatu cha Angelina Kwa pamoja)

Watu :( wanacheka Sana)

Mc: nani…mgomvi…

Maharusi :( wananyanyua kiatu cha Raymond Kwa pamoja)

Mc: nani ndo anapenda kushika rimoti?

Maharusi :( wananyanyua kiatu cha Angelina)

Raymond: halafu sasa anaweka ma muvi ya kihindi halafu analala…ukitoa, akishtuka utakubali muziki…

Angelina :( anacheka Sana)

Watu :( wanacheka pia)

Mc :( anacheka kidogo) nani anapenda kudeka?

Maharusi :( wananyanyua kiatu cha Angelina)

Mc: nani ana upendo Kwa ndugu?

Maharusi :( kila mmoja wao ananyanyua kiatu cha mwenzie)

Watu: wow...

Mc: basi naona bibi harusi kashinda kwenye mchezo huu mfupi… (Kwa watu) mmefurahia?

Watu: saaaana endelea

Mc: ah inatosha…sasa rudini (kwa maharusi) mkakae na ratiba nyingine ziendelee

(Maharusi wanaenda kukaa)

Mc: utambulisho sasa…

(Maharusi wanatambulisha ndugu zao, jamaa na marafiki zao kwa nyakati mbalimbali, wakitambulishwa kwa nyakati tofauti wananyanyuka na kuwapungia watu mikono, utambulisho unaendelea na baada ya muda utambulisho unaisha)

Mc: sasa naomba wasukuma mje mtuchangamshe kidogo maana nimeambiwa bwana harusi ni msukuma wa Mwanza naombeni mje mtupe mambo

(Wasukuma na watu mbalimbali wanapita mbele kucheza ngoma za kwao)

Mc: Asante Dj…sasa jamani zawadi…

(Watu mbalimbali wanajiandaa Kwa zawadi)

Mc: vikundi ni vingi jamani hawa watu wanaonekana wanaishi na watu vizuri sana…nitatoa utaratibu wa zawadi msijali wote mtapata nafasi ya kutoa zawadi

(Watu wanajiandaa)

Mc: tunaanza na wazazi…wa pande zote mbili…

(Wazazi wa pande mbili wanapita mbele yaani Mr and Mrs Bembele pamoja na mama mzazi wa Angelina)

Mc :( anampa kipaza sauti baba mzazi wa Raymond)

Mr. Bembele :( anapokea kipaza sauti hicho) harusi Safi?

Watu: safiiiii

Mr. Bembele: asanteni sana mabibi na mabwana, nafuraha sana…nakumbuka mwaka kama mmoja uliopita nilisimama mbele ya watu kama hivi nikampa zawadi nyingi sana kijana wangu aliyekuwa amehitimu shahada yake ya udaktari sasa leo tena nimepewa nafasi kuwazawadia watoto wangu wawili wa kike na kiume…

Watu :( wanashangilia Sana)

Mr. Bembele: asante kijana wangu kwa kunipa binti…nilikuwa nina mtoto mmoja tu ila kwa ajili ya mwanangu nimepata binti… (kwa Angelina) karibu sana binti yangu

Angelina :( anapiga magoti) Asante baba

Mr. Bembele: Asante mwanangu

Raymond :( analengwa machozi na anajikuta Analia kwa furaha)

Mr. Bembele: nawapenda wanangu…sisi wazazi wenu tunawapa zawadi ya nyumba moja na mapumziko ya nchi za ulaya kwa muda wa mwezi mmoja, kuzungukia nchi mbalimbali za ulaya ndani ya mwezi mzima (anawapa pasipoti zao)

Watu: wanashangilia Sana

Mr. Bembele :( anawakabidhi pia hati za nyumba)

(Baada ya zawadi hiyo wazazi wa pande mbili wanarudi kukaa, zawadi zinaendelea kuletwa kwa maharusi hao wanaopendwa sana na watu,watu wanacheza,wanakula,wanapiga picha wanafurahia sherehe hiyo,wazazi wana furahi,wafanyakazi wa Raymond wa ofisini na nyumbani wanaonekana wana furaha kubwa,marafiki wa Raymond na Angelina nao wanafurahi sana,Christina ambae alikuwa ndo kizingiti kikubwa katika penzi la Angelina na Raymond nae anaonekana kuwa na furaha kubwa sana yeye pamoja na hawara yake wa zamani na mume kwa sasa,mambo ni burudani,wadogo zake Angelina nao wanaonekana kufurahi sana,picha zinapigwa za ukumbusho kwa ndugu jamaa na marafiki,kila kitu kinaonekana kupendeza na siku hiyo inakuwa ni siku nzuri kwa Angelina,Raymond pamoja na familia zao.Angelina ni mke halali wa aliyekuwa bosi wake Bw.Raymond Bembele kijana tajiri na mtoto wa pekee wa mfanyabiashara tajiri jijini hapo.harusi imefana kwelikweli na ni ya kifahari kwelikweli,watu wamekula,wamekunywa,wamepata zawadi mbalimbali,kuna burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali hasa waimbaji wa nyimbo za injili,ni harusi ya kukumbukwa.)

Post a Comment

0 Comments