I KILLED MY LOVER 2

 


SCENE 2:

(Dada Fulani amekaa kwenye chumba Fulani kinaonekana kina Giza kiasi na haonekani vizuri kwa mantiki ya sura ila inajulikana kwamba ni mwanamke)

Mwanamke: Robert alinikosea ndo maana nikaona nimuue…asingefanya alichokifanya basi nisingemuua na wala nisingepata wazo za kumuua kinyama hivyo… natumaini kuwa huko alipo atakuwa ameona sababu ya mimi kumuua alinichezea na kuniacha solemba na kunifanyia vitu vingi sana vibaya kwa jeuri ya pesa hiyo ndo adhabu yake, ilinilazimu nilipize kisasi jamani sio kwa mambo ya ajabu aliyoamua kunifanyia huyu mzee asiyekuwa na haya…nenda Robert…nenda hawara yangu…pole kwa wote walioguswa na msiba huu.

(Mara inasikika kelele nje, hatoki anaendelea kukaa kwenye chumba kile chenye Giza)

Polisi :( wamesimama nje ya nyumba ile iliyoungua na moto jana yake) jamani habari zenu

Majirani: salama

Polisi: naombeni wote mtoke nje kuna kitu hapa kimejitokeza juu ya mwili wa marehemu

(Majirani wote wanatoka nje kuja kusikiliza wito)

Polisi: mmetoka wote?

Liliana:(anakuwa wa mwisho kutoka) nilikuwa nimebaki mimi tu(anatabasamu)

Polisi: ulikuwa wapi?

Liliana: nilikuwa naoga

Polisi: sawa

Mama Neema: hapa sasa tumetoka wote sasa

Polisi: sawa… (anawaangalia majirani wote) basi sawa…kwa mujibu wa taarifa ya hospitali marehemu bwana Robert hakufa kwa ajali ya moto bali alichomwa kwanza visu ndipo akaungua

(Minong’ong’ono baina ya majirani)

Polisi: nani kati yenu alisikia au alishuhudia tukio hili

Mama neema: mimi nikiwa mmoja wao…

Polisi: uliona nini?

Mama neema: moto tu

Polisi: hukuona mtu…anaingia na kutoka?

Mama neema: hapana hatukuona kabisa

Polisi: jaribu kukumbuka

Mama neema: hapana sikuona kabisa

Liliana: jaribu kuvuta kumbukumbu unaweza ukakumbuka

Mama neema :(kwa polisi) yaani sikumuona kabisa labda kama wenzangu walimuona

Polisi :( anawageukia wale wawili) hamkuona kitu…

Majirani: hapana

Polisi :( anajikuna kichwa) dah!!Muuaji alitumia akili Sana hakuingilia mlango wa mbele wala kutokea huko na pia ameharibu ushahidi wote uliokuwa unatakiwa…amecheza karata vizuri sana

Mama neema: yaani…ila hawezi kuwa ametokea mtaa wetu, Bw. Robert alikuwa ni mtu mzuri sana alikuwa ni tajiri lakini aliishi na watu vizuri alitupenda sana na kipindi cha sikukuu wote hapa majirani zake tulikuwa tunanufaika, hakika alikuwa ni mtu wa watu sana hasahasa hapa kwetu wote hapa tulikuwa tunampenda

Liliana: lakini usiusemee moyo ndugu yangu

Kijana:ni kweli dada yangu unachosema ila kwa bw. Robert ambae amemuua (kimya kidogo) hawezi kuwa ametokea hapa mtaani, wewe si umekuja juzi juzi tu…humjui vizuri bw. robert alikuwa ni mtu wa watu sana

Polisi: sawa…ila wanasema kikulacho ki nguoni mwako na rafiki yako wa karibu ndo adui yako naungana na huyu binti mjamzito kwa kusema msiusemee moyo…hivyo basi…majirani wote ndo mtakuwa ni watu wa kwanza kabisa kuondoka na mimi mpaka kituoni kwa ajili ya kuangaliwa alama za vidole yaani finger prints maana kilikutwa kisu eneo la tukio hivyo tutapima alama ya vidole kisha tutajua na jinsi mlivyo pandeni kwenye gari hakuna mtu kutoroka hapa

(Bila wasiwasi majirani wote wanapanda kwenye gari la polisi na kuelekea kituo cha polisi, wanapofika huko haraka bila kupoteza muda wote wanapimwa alama za vidole vyao na kuamuliwa wasubiri nje)

Polisi: sawa naomba mnisubiri hapo nje nakuja baada ya muda

(Majirani wanatoka nje na kusubiri kwenye viti, na baada ya sekunde kadhaa polisi anakuja)

Polisi: kweli mlisema kweli kwamba Robert alikuwa ni watu wa mtu na hata siku moja hawezi kuwa ameuawa na mmoja wa majirani zake…hiki kisu hakiendani na alama ya vidole ya yoyote hapa…sasa ni jukumu letu sisi polisi kumtafuta muuaji na wala hataenda bure

Mama neema:si nilikuambia yaani muuaji ametoka mbali sana sijui wapi

Polisi:ni kweli mama tumeamini maneno yako

(Wakati huo mke na watoto wa bw. Robert wanafika kituoni hapo)

Lydia :( mke wa Robert) jamani habari zenu

Wote: salama…

Polisi: na wewe ni…

Mama neema:ni mke wa marehemu huyu anaishi Canada watoto wake wanafanya kazi huko ndo wamemchukua

Liliana: maskini pole dada yote ni kazi ya Mungu, mume wako anaonekana alikuwa ana upendo sana na watu…watu wengi wanamlilia (anasikitika)

Lydia :( anaanza kulia kwa uchungu sana) Mume wangu tulitoka kuongea nae jana akaniambia kuwa amenikumbuka anataka aje akae Canada amechoka kukaa peke yake huku…jana hiyohiyo nikapigiwa simu kuwa mume wangu amekufa jamani (Analia sana)

Polisi: pole sana mama, (anamsogezea kiti kisha anamsaidia kukaa) jikaze mama

Lydia: naomba polisi mfanye kazi yenu kuhakikisha kuwa muuaji wa mume wangu anapatikana mapema Zaidi…nataka apatikane ili (anaongea kwa hasira) nimshuhudie kwa macho anavyonyongwa

Raphael :( mmoja wa watoto wa marehemu) habari zenu jamani...

Wote: salama

Polisi: wewe ndo mtoto au?

Raphael: (kinyonge sana) ndio, naitwa Raphael…kaka zangu watakuja baadae kidogo (anasikitika sana) jamani baba yangu dah…alipanga kuja kukaa na sisi Canada leo hayupo tena (Analia)

Majirani: pole sana

Raphael: (anafuta machozi) nashukuru sana na Mungu ndo mpangaji wa yote…ila (anamuangalia polisi) naomba haki itendeke nakutegemea sana…sisi tumeshakuwa watu wazima ndio tuna wake zetu lakini tulikuwa tunamhitaji baba yetu

Polisi: usijali tutafanya kila kitu mpaka haki itatendeka lazima tumpate muuaji

Liliana: aisee…na alifanya kitu cha kinyama sana

Polisi: sio kidogo

Liliana: na alikuwa mwanamke au mwanaume?

Polisi: haijajulikana…

Mama Neema: yaani hakuna anayejua chchote

Polisi: katumia akili nyingi Sana

Mama Neema: sana

Polisi: ila itakuwa ni mwanaume tu maana kama ni mwanamke asingeweza kupambana nae hivyo

Mama Neema: na Robert alikuwa yuko vizuri sana kimazoezi

Polisi: nilikuwa namfahamu maana mara nyingi sana alikuwa anakuja kuwaona wafungwa

Mama Neema: hakika tumepoteza jembe…

Kijana: hakika

Liliana: Mimi nilikuwa simjui…hata kidogo

Mama Neema: sasa wewe unashinda unalala ungemjulia wapi?

Liliana: ndo hivyo vitu vizuri huwa havidumu

Mama Neema: kabisa

Polisi: sasa nyie nendeni mkafanye mipango ya mazishi mwili wa Robert umeharibika sana cha msingi tu n kwenda kumzika tu halafu sisi bado tunafanya uchunguzi tutakuwa tunawapa taarifa ni wapi tumefikia sawa

Majirani pamoja na familia ya marehemu: sawa

(Wanaondoka)

Post a Comment

0 Comments