I KILLED MY LOVER 3

 


SCENE 3: -

BAADA YA MIEZI SITA:

(Familia ya bw. Robert yaani mke na watoto wake wapo kituo cha polisi wakifuatilia kesi ya mauaji ya mpendwa wao)

Gabriel :( mmoja wa watoto wa bw. Robert) mkuu huu ni mwezi wa sita tangu baba yetu auawe kikatili lakini bado hakuna vitu vya maana ambavyo mmetupa Zaidi ya kusema kuwa mnaifanyia kazi, mnafanyia kazi mpaka lini mkuu? Embu tupeni jibu la kueleweka bwana tumesubiri Sana

Polisi: naomba tuendelee kuwa wapole tu, tutampata aliyefanya mauaji Yale na kuchoma nyumba yenu, kuweni wapole tu…tutampata tu, kesi ngumu sana maana hakuacha ushahidi mwingi

Raphael: kila mara huwa mnatuambia hivyo…tumechoka Kama hamuwezi naomba tuite wapelelezi toka nchi za wenzetu waje wafanye uchunguzi

Lydia :( Analia) yaani mume wangu aliuawa kikatili Sana na hakuna mtu anaehangaika na kifo chake nyinyi polisi hamfanyi chochote kila tukija hadithi ni ile ile kuwa mtaifanyia kazi lakini kimya, jamani tusaidieni tunataka kupata muafaka wa hili suala (anaanza kulia) au mnataka kesi ya mume wangu iishie njiani?

Michael: (mtoto wa pili wa bw Robert) mama acha kulia hapa cha msingi ni kutafuta wapelelezi kutoka nje naona hawa polisi wameshindwa kufanya kazi yao

Polisi :( anapata jazba) kijana chunga mdomo wako, watu hatulali

Michael: mbona hakuna jipya kila siku point ni ile ile? Bora tuite wapelelezi kutoka nje

Gabriel: ndo maana yake dogo hapo maana huu ni mwezi wa sita na hakuna kilichofanyika Zaidi ya hadithi…hii inamaanisha kuwa hamjui kufanya kazi zenu…

(Wakati huu anakuja mwanamke Fulani haonekani kirahisi na amebeba mtoto mchanga anafika anaingia walipo familia ya bw. Robert na polisi mwenye dhamana ya kusimamia kesi ya bwana Robert)

Polisi :( Kwa jazba) wewe mama unataka nini?

Mwanamke :( anaonekana kikamilifu na si mwingine bali ni Liliana yuleyule mmoja wa majirani waliokuwa wanaishi karibu na nyumba ya bw. Robert) nimekuja kujitoa mwenyewe maana nimeona mlishindwa kunikamata

Polisi: unamaanisha nini?

Liliana: (Kwa upole Sana) nilimuua bw. Robert

(Wote waliopo hapo wanapigwa butwaa)

Lydia: wewe mtoto…kwanini ulifanya vile? Kwanini (Analia Sana) ulimuua mume wangu alikufanya nini kibaya wewe mtoto…

Gabriel: wewe dada…nini kilikufanya ufanye vile? Nini kilikupelekea kufanya yote hayo…?

Raphael: sikutegemea na wala sikuwaza kuwa mmoja wa majirani zake wangemfanyia hivyo?

Polisi :( anasikitika Sana) kwanini ulifanya vile

Michael :( anamsogelea) kwanini ulimuua baba yangu na kuchoma nyumba yetu?

Liliana:(kwa utaratibu)hasira…huyu mtoto ni mtoto wa bw.Robert…na pia alinidanganya hana mke wala watoto,aliniambia kuwa mke na watoto wake wote walikufa kwenye ajali hivyo kabaki hana mtu na kwamba ananipenda sana,kwa akili zangu za kitoto nilimuamini sana na nikajua nimepata mwanaume wa maisha yangu alinidanganya aliponichoka akaniambia   kuwa ana mke na watoto…na anawapenda sana,alinitukana sana na kuniambia maneno ya kashfa…kitendo kilichonipa hasira…sana na kikanipa hasira na kunifanya nifanye kitendo kile haikuwa kwa nia mbaya ilikuwa ni hasira tu…alinisukuma kwa mambo mengi mengine ni hadithi ndefu sana

Polisi: pamoja na hayo usingemuua…

Liliana: ningefanyaje? Aliniharibia maisha yangu na furaha yangu kwa asilimia mia…namchukiaa sana

Polisi :( kimya kidogo)

Liliana: ningefanyaje? Ningekuja kwenu je mngenisaidia?

Lydia :( Analia) lakini pamoja na hayo usingemuua mume wangu…

Liliana: ningefanyaje? na pia nilimuua kujikinga mimi na mwanangu maana sio mara moja bali mara nyingi sana alituma watu waje waniue

Polisi: sijui kwakweli kikubwa tu upo chini ya ulinzi…tukutane mahakamani binti

Liliana :( kimya hasemi kitu)

Polisi :( anatoka)

(Wote waliopo hapo hawana la kusema Zaidi ya kukaa kimya na kuangalia chini huku kila mtu anawaza la kwake)

Gabriel:(anajikuta anasikitika sana) sijui ni nini ila kwa niaba ya wadogo zangu na baba yangu napenda kukuomba msamaha kwa maumivu yote ambayo baba yetu alikusababishia…msamehe sana na umuombee Mungu amsamehe kwa yote aliyokufanyia…

Liliana :( Analia sana)

Raphael: hatujakifahamu kisa chote kilichokusababisha ufanye hivyo ilia naomba kwa hayo machache uliyotuambia mi naomba nimuunge mkono kaka yangu na kuwaomba msamaha wewe na mwanao kwa yote ambayo yamejitokeza

Michael: msamehe baba yetu na umuombee apumzike kwa Amani

Lydia :( Analia)

Polisi :( anarudi yeye pamoja na askari mwenzake huku wamebeba pingu)

Lydia: si mngemuacha amlee mtoto wake hata mpaka akue kidogo, wewe ni wa kunyongwa tu (kwa polisi) anyongwe huyu…muuaji mkubwa huyu

Polisi: mahakama itaamua na sio sio… (Kwa polisi mwenzie) afande Marco mfunge pingu umpeleke rumande, (kwa Liliana) mlete mtoto

Liliana :( anamshusha mtoto na kumpa polisi)

Polisi :( anamkabidhi mtoto kwa Lydia)

Lydia :( anampokea)

Afande marko: sawa afande… (Anamfunga pingu kisha anamchukua na kumpeleka rumande)

Polisi :( anashusha pumzi) kitu mlichokitaka kimetimia

Lydia: ni kweli lakini…sijui kwanini pamoja na jazba yote mara baada ya kumuona muuaji wa mume wangu na pamoja na kwamba ninamkumbuka sana mume wangu…ila baada ya huyu binti kusema kwanini alimuua mume wangu sina hasira nae nimejikuta tu namuonea huruma sana…

Polisi :( anacheka kidogo) si umesema anyongwe?

Lydia :( anacheka kidogo) ni hasira tu

Gabriel: kuna kitu kuhusu huyu dada ambacho watu wengi hawawezi kukijua kirahisi mpaka akiseme yeye…

Lydia: sijui ni nini

Gabriel:ni hasira tu

Raphael: kweli…hiyo hasira ilisababishwa na kitu Fulani…sijui ni nini lakini hiyo hasira ilisababishwa na kitu kama depression…

Polisi: yote kwa yote…aliua, na hatuwezi kulikalia kimya…

Michael: hakuwa katika akili yake timamu…alisukumwa na kitu

Polisi: aliua, iwe kwa makusudi au kwa kusukumwa…atahukumiwa…Lulu alipomuua Kanumba si ilikuwa kwa bahati mbaya ila si alihukumiwa?

Raphael: kwa kweli

Lydia: sawa…tutamsikiliza Zaidi atuambie…kisa kizima kwa sasa turudi nyumbani

Polisi: nyie nendeni tukutane mahakamani

Raphael: mtoto bado mchanga Sana, unaonaje akachwa hapa akae na mama yake?

Gabriel: yes, aachwe tu na mama yake maana atahitaji kunyonya na kadhalika

Polisi: sawa (anaita mmoja wa maafande)

Afande :( anakuja)

Polisi: kuna mama amekamatwa sasa hivi hapa mpelekee mtoto wake

Raphael:(anaonekana kumhurumia sana Liliana) maskini mwanae bado mdogo

Afande :( anamchukua mtoto kisha anatoka nae kuelekea rumande alipo Liliana)

Polisi: ndo hivyo…yote maisha na hakuna ajuae kesho

Wote: kabisa

Lydia: sawa sisi…tunaenda

Polisi: karibuni Sana

(Lydia na wanae wanaondoka huku wamepoa tofauti na jinsi walivyokuja, wanapanda gari kisha wanaondoka zao)

Post a Comment

0 Comments