I KILLED MY LOVER 25

 


SCENE 25: -

BAADA YA MIAKA KUMI NA SITA: -

(Asubuhi nyingine njema, hali ya hewa ni njema na ya kupendeza, jua ndo linaanza kuchomoza, binti mrembo anafungua mapazia kuruhusu mwanga kuingia chumbani kwake, anatabasamu mara baada ya kuona mwanga unaompa tumaini la siku mpya)

Binti :( anakaa kitandani) oh napenda Sana maisha yangu…

(Kuna mama ameenda umri anakuja chumbani Kwa binti)

Mama: Liliana…mwanangu

Binti: abee mama yangu mpenzi…Madam Bianca

(Wanacheka)

Bianca: umebadilika Sana mwanangu…yaani mtu akikuona hawezi kukukumbuka…

Liliana :( anacheka)

Bianca: happy 23rd birthday my love

Liliana: thank you…mama (anamkumbatia)

Bianca :( anamkumbatia pia) nakupenda binti yangu umekuwa ukinipa Amani na furaha kubwa tangu siku ya kwanza nimekuona mwanangu

Liliana: Asante mama kwa kunilea vyema umenisomesha umenipenda nakupenda sana mama

Bianca :( anacheka Sana) tumepatana

Liliana: Sana…

Bianca :( anashangaa) Liliana

Liliana :( anaogopa) nini mama?

Bianca: hujaoga, hujavaa na leo ni birthday yako una mambo mengi sana ya kufanya moja ni kwenda chuo

Liliana: NO…mama…No Leo siendi chuo I want to enjoy with you mama…

Bianca: of course, ila mwenzio nimezeeka hata sijui kuenjoi

Liliana: nani kakwambia umezeeka bado ni binti mrembo na wa kuvutia kama ulivyokuwa miaka 16 iliyopita

Bianca: unanipamba tu muone…kitoto kiongo hiki

Liliana :( anacheka kidogo) acha nikaoge...Toka nibadilishe nguo

Bianca: hivi umesahau nilikuwa nakuogesha na mara zote ulipokuwa ukiugua nakuogesha naukubwa wako

Liliana: nakumbuka mama ila sasa mwenzio nimeshakuwa limama

Bianca: hiloooo…umekuwa limama wapi hata boyfriend huna…toka hapa

Liliana: mama sitaki boyfriend kwa sasa na unajua…unajua nilijaribu kuwa nae akanidanganya kwahiyo sitaki tena...Nataka kuwa single kwanza kwa muda

Bianca: wewe mimi nishazeeka nataka wajukuu…

Liliana: mama mi bado mdogo bwana nitakuwa nae

Bianca: okay…take your time usije ukasema mama alinishawishi…ila kumbuka wewe sio teenager tena umeshavuka ule umri wa kuruka kutoka kwa huyu kwenda kwa huyu sasa wewe umefikia umri wa kuchagua na kuwa serious

Liliana:(anatabasamu) nakuelewa mama kwamba unataka mjukuu utampata

Bianca: lini sasa?

Liliana: soon…haya nenda nioge nije ninywe chai niwachukue Anna na Bella tukazurure

Bianca: haya bwana…ngoja nitoke…(anatoka)

Liliana:(anaingia bafuni na kuanza kuoga, na baada ya dakika kadhaa anamaliza kuoga anavaa kisha anapaka vipodozi kidogo kisha anatoka kuelekea jikoni) yaani nina njaa...Mungu wangu

(Binamu zake na baadhi ya marafiki zake wanapiga kelele)

Watu: surprise…

Liliana :( anageuka walipo watu wale) Oh My God…nyie mmefanya hii kitu saa ngapi

Bianca: wakati katoto kanakoroma sisi tulikuwa tunapamba kupika keki na kuandaa zawadi

Liliana: jamani… (Anataka kulia) asanteni Sana

Anna :( amekuwa binti mkubwa na umri wake ni miaka 28) happy birthday cousin (anampa zawadi)

Liliana :( anapokea zawadi) thank you cousin jamani... (Anamkumbatia)

Bella :( amekuwa binti mkubwa umri miaka 25) happy birthday binamu mjanja kuliko woteeeee (anampa zawadi)

Liliana (anacheka huku anapokea zawadi) Asante binamu mtata (anamkumbatia)

(Rafiki zake wanampa zawadi huku wafanyakazi wa Bianca wakionekana kuwa na furaha juu ya siku hiyo yenye kawaida ya kusherekewa kila mwaka)

Mpishi: yaani madam anampenda Sana mwanae…

Mtunza bustani: yaani Sana

Bianca :( Kwa Liliana) my baby… (Anampa ufunguo wa gari) zawadi yako ya birthday

Liliana: wow…mama gari?

Bianca: yeah mama gari

(Rafiki zake wanashangilia)

Bianca: umefurahi?

Liliana: saaaana mama…Asante Sana mama...Naomba nilione

Bianca: sure…lipo nje…twendeni tukalione

(Liliana na rafiki pamoja na binamu zake wanatoka nje kuliangalia gari hilo)

Liliana: wow mama gari zuri Sana

Bianca: umelipenda?

Liliana: ndio mama

Bianca: changamoto ni kwamba hujui kuendesha

(Wanacheka)

Liliana:(anaingia ndani ya gari)

(Rafiki zake wanampiga picha)

Bianca: nakwambia mtoto wa Bianca anavyopenda kuonekana (anaguna kisha anacheka)

Liliana:(anaanza kudeka) jamani mama

Bianca: sasa kwani uongo?

Anna:(kwa Bianca) aunt tunaweza kwenda kwenye pati leo?

Bianca: ya nani tena? leo kuna pati ya Liliana hapa jioni

Bella:(anamnong’oneza Bianca) tumemuandalia pati aunt

Bianca: hata mimi nimemuandalia pati jamani

Anna: basi tukimaliza ya hapa

Bianca: kwanini msifanye kesho bwana si huwa mnajua kuwa sipendi kuwaona mnadhurura usiku

Anna: basi sawa tutafanya kesho ila leo ndo ingenoga aunt maana ndo siku yake…

Bianca: hata kesho itanoga sana tu bwana…baba yenu yuko wapi?

Anna: yupo nyumbani yaani tangu mama amefariki hataki kutoka nje kujichanganya

Bianca: maskini…mke ni mke tu pamoja na kwamba mama yenu alikuwa mkorofi ila baba yenu alimpenda hivyohivyo

Bella: Sana...

Bianca: anyways tusiongelee masuala ya misiba Leo ni siku ya Liliana tuenjoi nataka mkaangalie magauni yenu nimeweka chumbani kwa Liliana ndo mtavaa usiku au mlitaka mvae vimini kama mnavyovaaga…halafu mbona hao wakwe hamniletei

(Anna na Bella wanacheka kisha wanaingia ndani)

Bianca: hawajibu…watoto wa siku hizi (anamuangalia Liliana ambae anaonekana kufurahia zawadi yake ya gari) mwanangu kafurahi mwenyewe na hivi anapenda zawadi (anatabasamu)

(Liliana na rafiki zake bado wanaendelea kufurahia maisha kabla ya sherehe ya usiku)

Post a Comment

0 Comments