I KILLED MY LOVER 24

 


SCENE 24: -

BAADA YA MWEZI MMOJA: -

(Anna, Bella na Liliana wanashuka kwenye gari wakitokea shuleni, wanaonekana wanafuraha sana na shauku yao ni kumuona Bianca maana hawajamuona tangu asubuhi)

Liliana:(huku anaingia ndani akiwaongoza binamu zake) mama

Bianca:(amekaa sebuleni akiwa na mjomba wake Liliana) abeee

Liliana:(anamuona mjomba wake) mjomba…

Mjomba: naam mwanangu

(Anna na Bella wanamkimbilia baba yao)

Mjomba: hamjambo jamani habari za shule?

(Watoto wote wanaitikia)

Anna: habari za huko baba…umepona?

Mjomba: ndio mwanangu nimepona…

Bella: huko India pazuri baba

Mjomba: pazuri eeh

Liliana:(anatabasamu huku anamuangalia Bianca)

Bianca: nendeni mkabadilishe nguo mle mfanye kama mna homework

Anna na Bella: sawa aunt

Liliana: sawa mama

(Wanaenda chumbani kwa Liliana)

Mjomba:(anacheka kidogo) wanaonekana kufurahi sana…

Bianca: acha wafurahi ni watoto…mimi napenda sana watoto Mung utu hakunijalia mtoto…

Mjomba: ipo siku moja atakupa

Bianca:(anatabasamu) emeshanipa na sio mmoja watatu kabisa

Mjomba: safi sana na yote ni kwasababu ya upendo wako na roho yako Mungu atakubariki Zaidi na Zaidi

Bianca: usijali kaka yangu… (anabadilisha mada) embu niambie habari za huko?

Mjomba: ah salama tu dada yangu matibabau yameenda vizuri na ninamshukuru Mungu nimerudi salama

Bianca: asante sana…sasa upumzike kidogo uanze tena kuchapa kazi uikoe familia yako si unajua kuwa wewe ndo kichwa...mkeo hana hata akili vizuri

Mjomba:(anacheka huku anaangalia dirishani) hatajwi huyo hapo

Bianca: yaani una mke mtata(anaguna)

Shangazi:(anagonga mlango)

Msichana wa kazi:(anafungua mlango)

Bianca: karibu

Shangazi:(anaingia kwa shari)

Bianca:(anaguna) kumekucha

Mjomba:(kwa mke wake) vipi mwenzetu mbona umeingia kama kuna ugomvi

Shangazi: hapa ndo kwa mke wako? maana umetoka huko sijui India mbio mwanaume usivyokuwa huna adabu…mpaka kwa mwanamke mwingine ndo mke wako?

(Bianca na mjomba wamekaa kimya huku wanamuangalia tu)

Shangazi:(anacheka kidogo) au mna mahusiano?

Bianca:(anabaki mdomo wazi)

Shangazi: niambie nimjue mke mwenzangu na nilijua tu sio bure tu…mara kakupeleka India mara sijui nini mara kasomesha watoto wako mara kamlea huyo mtoto wa dada yako yote hayo anayafanya kama nani? kama sio hawara ni nini? mnadhani mimi ni mtoto mdogo sina akili au?

Mjomba: wewe mwanamke wewe (anasikitika sana)

Shangazi: wewe mwanamke nini? we huoni aibu sasa hivi una watoto ni wakubwa unakuwa na mahawara nje utakufa mshenzi wewe

Mjomba: kuwa na adabu mimi ni mumeo

Shangazi:(anafyonza) nenda zako huko

Mjomba:(kwa Bianca) dada nashukuru kwa misaada yako yote dada yangu

Shangazi: eti dada hamuoni hata haya watizame nyuso zao…(anafyonza)

Mjomba: ila mimi siwezi kukaa na huyu mwanamke tena...Namuachia ile nyumba akae peke yake naomba tu unisaidie nipate hata chumba na sebule niishi na wanangu kwa Amani utakuwa unanikata kwenye mshahara

Bianca: usijali kaka yangu utapata tu nyumba nzuri hao wanao ni wanangu pia ni jukumu letu kuwalea

Shangazi :( anapiga makofi kishari) kwanini msiambiane ahamie kabisa humu?

Bianca: sikiliza mama Anna…mumeo sio hawara yangu narudia tena kuwa misaada ninayotoa ninatoa tu kibinadamu maana mimi sina watoto na Liliana aliniomba niwasaidie kwa vyovyote vile umemtesa sana Liliana lakini hajawasahau wala kulipa kisasi sasa badala ushukuru wewe unabwabwaja tu kama mwendawazimu

Shangazi: sikuwaomba na wala sikumuomba huyo Liliana anifanyie chochote ni kiherehere chake tu mjinga sana huyo

Bianca:(anafyonza) natamani nikutandike kibao kimoja acha kumuita mwanangu mjinga unasikia wewe usidhani ni enzi hizo hana wa kumtetea sasa hivi nipo mimi

Shangazi:(anabenjua midomo)

Mjomba:(kwa mkewe) embu ondoka nenda zako

Shangazi: naenda na wanangu

Mjomba: wanangu hawaondoki hapa eti kwenda wakaishi na wewe mwendawazimu

Shangazi: kwahiyo kwa mantiki hiyo unataka kusemaje?

Mjomba: tunakuhama...baki na nyumba yako

Shangazi:(anaonyesha kuchanganyikiwa) eti nini? Hivi unasema kweli?

Mjomba: umesikia vyema mama…siwezi kuishi na mwanamke mkorofi kama wewe nimetoka safari hata unipokee vizuri kwa adabu umpe asante huyu dada katusaidia unamwambia maneno mabaya

Shangazi:(anaanza kushuka) lakini mume wangu jamani nisamehe unajua ni wivu tu na nimesikia kuwa unatembea na huyu mwanamke ndo maana nimekasirika hata ingekuwa wewe umesikia hivyo ungejisikiaje?

(Mjomba na Bianca wamenyamaza kimya)

Shangazi: mume wangu sasa ukiondoka mimi nitakaa na nani?

Mjomba:na huyo atakayeweza kukaa na wewe mimi hapana…

Shangazi:(anawaita watoto) Anna, Bella

Mjomba: embu acha kelele embu heshimu miji ya watu wewe mwanamke jamani

(Anna na Bella wanakuja sebuleni)

Anna: shikamoo mama

Shangazi:(anawashika mkono) twendeni nyumbani wanangu

Bella: tunafanya homework…

Shangazi: mtafanyia nyumbani wanangu jamani

Mjomba: hawa watoto naenda kuishi nao

Shangazi: eti wanangu kati ya baba yenu na mimi mnataka kuishi na nani?

Watoto:(bila kusita) na baba

Shangazi: jamani wanangu

Mjomba: ondoka uende zako (kwa Bianca) tunaomba tulale hapa leo

Bianca: haina shida kaka

Shangazi:(anashikwa hasira sana, anaondoka zake)

(Watoto, mjomba pamoja na Bianca wanabaki wanasikitika)

Bianca: yaani asipoangalia akaendelea na hii tabia basi ana hali mbaya sana…atajikuta anachanganyikiwa…

Post a Comment

0 Comments