I KILLED MY LOVER 27

 


SCENE 27: -

(Mchana wa siku kadhaa baada ya sherehe ya Liliana, Liliana na binamu zake wanashuka katika gari ambalo ni mali halali ya Liliana zawadi aliyopewa na mama yake wa kufikia siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwake)

Anna: wow...Binamu sikujua kuwa tunakuja mall…

Liliana :( anacheka) sasa unajua kuwa tumekuja …can we go?

Anna na Bella: sure

(Wanacheka)

Liliana :( anaongoza njia)

(Wakati wote wanaingia ndani, wanapishana na Robert yule mwanaume waliokutana katika mgahawa siku ya sherehe ya Liliana)

Robert :( anamuona Liliana) hey mrembo mambo

Liliana :( anasimama na kujaribu kuvuta kumbukukumbu)

Robert: tulionana kwenye mgahawa Fulani siku chache nyuma…mlikuwa na sherehe Fulani sijui ilikuwa birthday ile?

Liliana: ok nimekukumbuka…shikamoo?

Robert: marahaba mrembo uko poa?

Liliana: nipo poa za toka siku ile?

Robert: ah Safi tu…naona mnaingia kuchukua viwili vitatu

Liliana: ndio…

Robert: haina shida…ila (anatoa simu yake) ningepata namba yako ningefurahi sana

Liliana :( anawaangalia binamu zake)

Anna :( anampa ishara ya kukubali)

Liliana :( anamtajia)

Robert :( anaandika)

Liliana: haya poa

Robert: poa nitakutafuta...

Liliana: sawa

Robert :( anaondoka na kuelekea kwenye gari lake)

Liliana :( anamuangalia Sana)

Bella: oh My God, he is so handsome

Liliana: umempenda?

Bella: ah wapi na bae wangu nimuachie nani?

Anna: niachie Mimi

(Wanacheka)

Anna: ila girls jokes apart, huyu baba mzuri

Liliana: so?

Anna: aha tunasema tu…maana anaonekana amekuzimikia kweli

Liliana: oh, please ni mume wa mtu...

Bella; umejuaje?

Liliana: anaonekana tena ukute ana watoto wanaolingana na mimi n ahata kunizidi

Anna: sio rahisi

Bella: kwanini usimpe nafasi?

Liliana: jamani hata hajanitokea

Anna: atakutokea tena siku si nyingi

Liliana :( anacheka) mna mambo nyie

Bella :( anatabasamu) yaani

Liliana: I mean ni mzee jamani

Anna: age is just number my cousin

Liliana: cuzo wewe?

Bella: kabisa…akikutokea go for it girl

Liliana :( anatikisa kichwa kidogo kisha anacheka) mmenishinda tabia walahi (anacheka) embu twendeni huko mnanishawishi vitu ambavyo mnajua kabisa kuwa mama hawezi kukubali hata kidogo

Anna: unamuongelea Aunt Bianca…wewe yule mzungu utaona tu anachopenda yeye ni kukuona kuwa una raha na sio vinginevyo

Bella: go for it baby…yaani natamani picha ianze hata sasa hivi

Anna: yaani wewe hunishindi

Liliana :( anatabasamu) yes…he is so cute na hizo ndevu zake zenye mvi…amenivutia sana

(Wanacheka)

Bella: go girl… (Anacheza kidogo)

Liliana: yaani sijui ningekuwa wapi Kama nisingekuwa na nyie machizi wangu wa nguvu

(Wanacheka huku wanaingia ndani maana muda wote walikuwa wamesimama nje)

Post a Comment

0 Comments