I KILLED MY LOVER 28

 


SCENE 28: -

(Majira ya saa tatu usiku Liliana yupo chumbani kwake anatazama tamthiliya huku anachati kwenye group ambalo yupo yeye na binamu zake)

Liliana:(anacheka sana) yaani haya majinga (anacheka tena)

(Bianca anaingia)

Liliana: oh mama…hujalala tu?

Bianca: unajua mama kuwa siwezi kulala bila kukuona na kukubusu na kukutakia usiku mwema mwanangu

Liliana: najua mama kuwa huwezi kulala bila kuniona

Bianca:(anatabasamu) asante Liliana kwa kuja katika maisha yangu mwanangu nimekuwa ni mtu mwenye furaha sana na zaidi nimekuwa ni mtu mwenye bahati sana

Liliana: mama, jamani wewe ndo nikushukuru mama yangu umenilea mimi na ndugu zangu kwa miaka yote hii umenipa elimu nzuri kwakweli sina cha kukulipa…

Bianca:(anatabasamu kisha anamkumbatia)

Liliana:(anamkumbatia pia) asante mama, nina bahati sana kukutana na wewe nakupenda mama

Bianca: usijali mwanangu…

Liliana:(anatabasamu)

Bianca: mbona unatabasamu sana?

Liliana:(anacheka) nothing mama

Bianca: umepata boyfriend

Liliana:(anacheka kwa nguvu) of course not mama…sijapata boyfriend

Bianca: umri unaenda mwanangu

Liliana: I know mama, ila sasa nataka kuwa sure

Bianca:is there someone?

Liliana: maybe yes, maybe no (anacheka sana)

Bianca: you little girl (anacheka) meaning?

Liliana: kuna mtu amenivutia ila yeye bado hajanionyesha dalili zozote za kutaka mahusiano na mimi

Bianca:be careful with your own heart my child usije ukasababisha majereha makubwa kwenye moyo wako

Liliana: yes mama

Bianca: okay mimi nina usingizi sana…naomba nikalale wewe endelea na kuchat na mkwe

Liliana:no mama nachati na cousins

Bianca:(anacheka sana kisha anambusu shavuni) lala salama mwanangu

Liliana: good night mama

Bianca:(anatoka chumbani humo)

Liliana:(anaendelea na kuchat)

(Wakati anaendelea na kuchati, mara simu yake inaita anaipokea)

Liliana: yes hello

Sauti ya kiume: mrembo

Liliana: nani?

Sauti: Robert…umenipa namba yako asubuhi tulipokutana mall

Liliana:(anachezea nywele zake) oh okay nambie…shikamoo

Robert: marahaba mrembo vipi umelala?

Liliana: hapana nipo tu ila ndo najiandaa nilale...

Robert: oh, okay mrembo…hata mimi najiandaa nilale… (anashusha pumzi) labda samahani naomba uniambie nina mazunguzo kidogo na wewe sijui nitakuona lini? kesho labda

Liliana:(bado anachezea nywele zake) mmmmmh mimi nasoma kwahiyo ninakuwa busy sana mchana labda jioni

Robert: perfect maana hata mimi ninapata muda jioni siku nzima ninafanya kazi nina makampuni yangu mwenyewe sasa ninajikita sana na kazi ukizingatia sina familia mimi nipo single

Liliana: unasema kweli wewe huna familia?

Robert: mke na watoto wangu walikufa wakati wanatoka safari, walipata ajali mbaya na kupoteza maisha sasa nipo kwenye mchakato wa kupata mke na watoto wengine

Liliana: maskini pole sana yaani dah…nimesikitika sana

Robert: ndo hivyo kazi ya Mungu haina makossa

Liliana: kabisa…basi sawa tutaonana kesho jioni

Robert: sawa mrembo nikutakie usiku mwema

Liliana:na kwako pia…

(Wanakata simu)

Liliana: maskini anasikitisha imagine kupoteza mke na watoto kwa mpigo (anasikitika)pole yake sana… (anaamua kupiga simu kwa Anna) dada yule baba kanipigia simu

Anna: enhe!!

Liliana: kaniambia kesho tuonane

Anna: go girl…

(wanacheka kisha wanakata simu, Liliana anajifunika shuka kisha analala)

Post a Comment

0 Comments