I KILLED MY LOVER 45

 


SCENE 45: -

BAADA YA MWEZI MMOJA: -

NYUMBANI KWA BIANCA: -

(Majira ya saa mbili usiku, Bianca pamoja na mchumba wake wamekaa sebuleni huku wanaonekana kuwa na mazungumzo ya kawaida, mkao wao ni wa kimahaba, Bianca amemlalia mjomba kifuani)

Bianca: baby mbona huwa unaogopa kuja akiwepo Liliana? na ukija unakuwa ni muoga…(anacheka)

Mjomba: (anacheka kidogo) nitazoea tu bwana wala usijali

Bianca: haya wewe ogopa tu ona sasa hivi umekuja maana nimekuambia yupo kwenye sherehe ya rafiki yake ukisikia tu gari linaingia mbio unakaa kama mimi ni dada yako

Mjomba: (anacheka)

(Kuna sauti ya gari linaingia ndani ya geti)

Mbise: (anachungulia dirishani)

Mjomba: (kwa Mbise) Mbise Liliana huyo?

Mbise: hapana sio Liliana ni yule shemeji

Bianca: Robert?

Mbise: ndio

Bianca: (ananyanyuka) anataka nini usiku huu?

Mbise: sijui

Robert: (anashuka kwenye gari na moja kwa moja anauendea mlango)

Bianca: huyu mwanaume vipi jamani

Robert: hodi… (anagonga)

Mjomba: (anafungua)

Robert: (anaingia)

Bianca: unafanya nini? Unataka nini Robert…

Robert: Bianca usiolewe mpenzi

Mbise: (anaweka mikono mdomoni ishara ya kushangaa)

Rober: nakupenda sana Bianca nipe nafasi

Bianca: (anamsukuma) embu nenda zako

Robert: kama hautakuwa wangu basi hautakuwa wa mtu yeyote (anatoka nje anaenda moja kwa moja mpaka kwenye gari yake anachukua dumu la mafuta ya taa na kiberiti na kurudi nayo ndani)

Bianca: (anamuona) Robert unafanya nini?

Robert: nakuua Bianca

Mjomba: (anashangaa) embu acha ujinga ndugu yangu huu ni utahira

Robert: sitanii

Bianca: Robert,

Robert: nikubalie Bianca I swear sitakuua yaani siwezi tu kukuona unaolewa na mwanaume mwingine huku mimi nakupenda nikubali mpenzi hii ndoa itakuwa yetu mpenzi...

Bianca: Robert umelewa embu tulia

Robert: (anamwaga mafuta) nikubalie mpenzi

Bianca: wewe ni kichaa

Robert: (anamaliza kumwaga mafuta) nikubalie mpenzi ili nisikuue

Bianca: siwezi Robert… siwezi kukukubalia (kwa Mbise) kimbia kaombe msaada huyu mjinga atatuulia humu ndani

Mbise: (anataka kukimbilia nje)

Robert: (anamrudisha) embu rudi hapa

Bianca: get out Robert

Robert: inaonyesha hunitaki kabisa sasa kama ni hivyo nakuua (anawasha kiberiti na kukitupia kwenye mafuta kisha anaondoka anachukua ufunguo na kufunga kwa nje)

Bianca: (anapiga kelele) tusaidieni

Lupemba: (anashtuka na kujaribu kuokoa jahazi)

(moto umezidi nguvu)

Bianca: (anateketea kwa moto)

Mjomba: (anateketea kwa moto)

Mbise: (anateketea)

Lupemba: (anakimbilia nje kuomba msaada)

(Nyumba inateketea kwa moto)

(Majirani wanajaa)

Lupemba: (anapiga simu kwa gari zima moto)

(Baada ya muda kidogo zima moto linafika)

Lupemba: (anapiga simu kwa Liliana) njoo nyumbani sasa hivi kuna tatizo (anakata simu) eh Mungu watu wote wamekufa… Husna, Siwema Mbise wote wamekufa (anasiktika sana) ni Robert huyo ndo kawaua

 

Post a Comment

0 Comments