I KILLED MY LOVER 44

 


SCENE 44:

CHUONI KWA KINA LILIANA: -

(Majira ya saa sita adhuhuri, Liliana pamoja na binamu zake wamekaa katika moja ya migahawa ya chuoni kwao wakipata chakula huku wanaongea mambo mbalimbali yahusuyo maisha. Wanaonekana wana furaha sana na maongezi yao yanaonekana ni ya Amani)

Anna: nani angejua kuwa Bianca na baba wangependana na kuoana

Bella: wanatarajia

Anna: ni kile kile bwana

Liliana: (anacheka kidogo) na shangazi alikuwa anawahisi kuwa wanatoka kimapenzi

Anna: kwa kipindi kile hawakuwa wanatoka

Liliana: ni vile tu mama yangu anajua kuheshimu watu

Bella: kabisa

Anna: halafu naona ile kuwahisi na kukaa kuwaambia ambia kuwa wana mahusiano ndo kiliwaleta pamoja

(Wanacheka)

Liliana: ndio

(Robert anakuja kwa mbali)

Anna: eeh yule si shemeji?

Liliana: Robert?

Anna: ndio

Robert: (anawafikia)

(Wanamsalimia)

Robert: (haitikii)

(Wanashangaa)

Robert: (kwa Liliana) wewe mwanamke…

Liliana: (anamshangaa)

Robert: ukiachwa achika

Liliana: bado sijakuelewa kwani mimi nimekufata tena baada yaw ewe kuniambia maneno makali kama yale?

Robert: nimempenda Bianca na nipo radhi kumuacha mke wangu na kumuoa Bianca

Anna: shemeji

Robert: (kwa hasira) mimi sio shemeji yako unikome

Liliana: umeongea nimekusikia sasa mimi nimekuzuia nini?

Robert: kila nikiongea nae anakutaja wewe inamaana wewe ndo unamzuia…kwanini lakini?

Bella: Liliana hazuii chochote yeye wala haongei na mama yake kuhusu wewe…topic yako kwenye nyumba ya kina Liliana haipo baba…Bianca hakutaki maana anatarajia kufunga ndoa na baba yangu

Robert: wewe mtoto wewe...shika adabu yako

Bella: wewe ndo ushike adabu yako wewe baba mtu mzima usiye na haya kazi kuharibu maisha ya watu lione lizomeeni

Anna: Bella acha

Liliana: (anasikitika) Robert nilikupenda sana ila umeniumiza sana pamoja na hayo mimi sikutaka kitu chochote kutoka kwako ila wewe bado unaendelea kutaka kitu maishani mwangu

Robert: kitu gani maishani mwako huku hata huyo mwanaharamu uliyembeba tumboni kwako simtambui na wala simjui

Liliana: (anasikitika) bado unanifata fata kisa mama yangu...Robert kwanini usituache tu tukae kwa Amani jamani

Robert: siwezi kukuacha kwa Amani maana nampenda sana Bianca

Liliana: sawa haina shida mwambie tu

Robert: hawezi kukubali maana anahofia wewe utamuonaje sijui

Liliana: nitamuonaje

Robert: sijui

Liliana: Robert listen nilikuwa nipo hapa na binamu zangu tunapanga harusi ya mama yangu naomba uondoke ili tuendelee na mipango yetu

Anna: umekuja kutuharibia wakati wetu mzuri

Bella: kwanza amejuaje tupo hapa?

Liliana: alihisi tu maana huwa napenda kukaa sana hapa

Robert: naomba nikutume wewe Liliana ya kwamba mwambie mama yako kuwa nampenda sana na asiolewe na kama hatakuwa wangu basi hatakuwa wa mtu yeyote

Anna: aisee

Bella: mtu mzima hovyoooo (anafyonza) hana hata aibu lione

Liliana: (kwa Robert) ujumbe wako nitaufikisha usijali

Robert: good (anaondoka zake)

Anna: huyu baba zinamtosha kweli?

Liliana: yaani sijui ni mkosi gani nilionao mwenzenu (machozi yanamlenga) sijawahi kufurahia maisha yangu

Anna: no usikumbuke ya zamani mdogo wangu huna mkosi wowote wewe ni Baraka Liliana kwanza una roho nzuri embu kumbuka mambo yote tuliyokufanyia mwanzoni lakini bado ulitusamehe hata Mungu alipokupa nafasi ya kuishi vizuri ulituita na tukaishi maisha mazuri Liliana baba alikufanyia unyama lakini umemsamehe na leo hii tunatarajia kuishi pamoja kama familia…wewe ni Baraka huna mkosi Liliana

Liliana: (anashusha pumzi) najua ila ikija suala la mahusiano sijawahi kufurahia maisha mwenzenu

Bella: come down cousin jamani

Liliana: (anashusha pumzi) yaani sijui

Anna: cheer up na tuendelee kuongea kuhusu harusi yaani kwanza mmeona gauni la Bianca?

Bella: nimeliona…yaani yule mwanamke ameenda age lakini bwana ana mvuto loh lile tako vipi?

Liliana: (anacheka) jamani

Bella: mimi nawaambia

Liliana: ndo maana Robert amedata

Anna: naomba usimuwaze yule mwanaharamu

Liliana: mwanaharamu amemuita mwanangu… I swear nitailea hii mimba na vyovyote

Anna: tupo sisi na mama yako atakuwa tu

Liliana: nimeathirika pia mwenzenu

Anna: it doesn’t matter kwani kuathirika ni nini mwenzangu? Utaishi tu

Liliana: sawa (anashusha pumzi) asanteni kwa kunipa moyo nawapenda sana

Anna: nasi tunakupenda sana

Liliana: (anatabasamu)

Anna: you are so beautiful Liliana

Liliana: (anatabasamu) asante sana

Bella: (anatabasamu pia)

Anna: twendeni nyumbani?

Bella: ofcourse hapa ni nyumbani tu

Liliana: okay twendeni kwa bibi harusi

(Wanacheka kisha wananyanyuka na kuondoka zao)

Anna: twendeni kwanza kwenye icecream

Bella: na wewe utasema una mimba

(Wanacheka huku wanaondoka mahali hapo)

 

Post a Comment

0 Comments