I KILLED MY LOVER 47

 


SCENE 47: -

BAADA YA MSIBA: -

(Liliana na binamu zake wamekaa katika nyumba nyingine ya Bianca na kila mmoja anaonekana kuwa na huzuni sana)

Anna: tumebaki yatima sasa…

Bella: (Analia) baba na aunt Bianca walikuwa wanategemea kufunga ndoa walikuwa na furaha sana

Liliana: nitamuua Robert

Anna: (anafuta machozi) no mdogo wangu usifanye hivyo

Liliana: nilikuwa yatima Mungu akanipa nafasi ya pili niishi kwa kunipa Bianca kama mama yangu Robert kwasababu ya ujinga wake amekuja kumuua (kwa hasira) I swear I will kill him

Anna: acha sheria ifate mkondo wake

Liliana: sheria? Sheria gani unayoongelea wewe Robert ameniambia simuwezi kiserikali kwahiyo anaweza kuhonga halafu kesi ikazimwa

Anna: lakini Liliana embu mfikirie mtoto wako tumboni

Liliana: namfikiria sana sitaki mwanangu aje akutane na baba yake ambae alimuulia bibi yake

Bella: Liliana achana na Robert msamehe na uache sheria ichukue hatua zake

Liliana: katika maisha yangu nimeshasamehe sana mara ya kwanza niliwasamehe wazazi wenu kwa kuniulia wazazi wangu nikaja nikamsamehe mjomba wangu kwa kunibaka mfululizo nikaja nikakusamehe wewe Bella na nikaja nikamsamehe Robert kwa kunibaka utotoni huyohuyo Robert nimemsamehe kwa kuniambukiza HIV kwa hili la kumuua mama yangu simsamehi lazima nimuadhibu…lazima afe (anaonekana kuwa na hasira sana)

Anna: (anashusha pumzi) unapanga kufanya nini?

Liliana: ni siri yangu

Anna: be careful vipi polisi waikijua

Liliana: nipo tayari kutumikia kifungo au hata kunyongwa ila tu niacheni nimuue Robert

Bella: binamu hatukubaliani na wewe

Liliana: sijali

Anna: Liliana

Liliana: ndo nakwambia sasa sijali kesho nahama naenda kuishi jirani kabisa na Robert naenda kupanga

Anna: Liliana mdogo wangu

Liliana: nimeshaamua sina mjadala kwa hili…nahama hapa maana nikikaa hapa nitakuwa namkumbuka mam yangu sana sitaishi kwa Amani

Bella: (anashusha pumzi) basi sawa

(Mlango unagongwa)

Anna: nani tena? (ananyaanyuka ili kwenda kuufungua mlango) oh karibuni sana

Liliana: nani?

Anna: wafanyakazi wa ofisini kwa marehemu Bianca

Liliana: (machozi yanamtoka) mama yangu anaitwa marehemu sasa kisa Robert (analia sana)

(Wafanyakazi wanaingia)

Mfanyakazi 1: oh, Liliana acha kulia umeshalia sana…kazi ya Mungu haina makosa yeye alipanga iwe hivyo angeamua aunt apone angepona ila ndo kaamua iwe hivyo usijali nyamaza kulia

Liliana: (Analia kwa uchungu uliochanganyika na hasira) aliyefanya haya atalipa haki ya Mungu naapa

Mfanyakazi 2: (anampigapiga) basi tulia mama tulia usije kuingia matatizoni

Liliana: I don’t care ni lazima nifanye kama alivyo fanya kwa mama yangu I swear

Anna: binamu yangu tulia naomba ukapumzike

Lilian: nitapumzikia jela

Mfanykazi 3: hali yako hairuhusu uwe na hasira au mawazo, relax Liliana

Liliana: ndo nasema mwanangu atanisamehe ila ni lazima nimuue huyo baba

Mfanyakazi 1: usiseme hivyo unaongea kwa hasira hujui unachoongea Liliana nakusihi utulie

Liliana: sitatulia kwa lolote mpaka pale nitakapoona Robert amekufa tena kama alivyokufa mama yangu (Analia) ni lazima nimuue

Anna: mdogo wangu

Liliana: sitaki kusikia kitu

(Wanabaki wanamuangalia kwa hasira alizo nazo)

Bella: (anashusha pumzi) najua una hasira sana binamu naomba upumzike

Liliana: naona hatusikilizani naomba mniache kila mtu aende kwao nina maandalizi mengi sana ya kufanya

(Kila mmoja ananyanyuka na kuanza kuondoka)

Anna: ukiwa na shida nipigie

Liliana: (anakaza macho) sawa

(Wanaondoka)

Liliana: (anabaki peke yake hali ya huzuni na uchungu inamuandama pale anapomkumbuka mama yake kipenzi) mama nakukumbuka sana…natamani mjukuu wako azaliwe umuone ila yule mshenzi amekatisha maisha yako kisa tamaa zake za kimwili nitamuonyesha kuwa mimi ni Liliana and no body messes with me…nitamuua haki ya Mungu naapa majira kama haya Robert atakufa I swear lazima afeeee (anakaza macho huku machozi yanatiririka mfano wa maji kwenye mfereji) nitamuua sitamuacha (anaukumbatia mto huku Analia sana)

Post a Comment

0 Comments