SCENE 48: -
MTAANI KWA KINA ROBERT: -
(Majira ya saa saba mchana hali
ya hewa ni ya mawingu kiasi, Liliana anafika katika nyumba kubwa tena
inaonekana ina wapangaji wengi sana)
Mama
mwenye nyumba: oh, binti ndo umekuja?
Liliana:
ndio nimekuja...natumaini chumba changu kipo tayari
Mama:
kabisa mimi sina ahadi za kijinga au za uongo nimekuwekea chumba kizuri kama
ulivyotaka
Liliana:
asante (anacheka kidogo) nilitaka
chumba chenye utulivu si unaona hali yangu hii?
Mama:
naiona
(Wanacheka)
Mama:
usijali (anamfungulia chumba) sasa
mbona hujaja na kitu chochote utakuwa unalala wapi?
Liliana:
nitavileta tu
Mama:
oh sawa
Liliana:
asante (anaangalia mazingira ya chumba
kile) nimekipenda ni kizuri (anafungua
dirisha anaona nyumba ya Robert) na ni kizuri sana naiona nyumba ile kwa
uzuri kabisa
Mama:
yule ni Robert tajiri mkubwa sana hapa mtaani kwetu ni mtu mzuri anapenda watu
ila ubaya wake anapenda sana wanawake
Liliana:
oh, anapenda sana wanawake ee
(Wanacheka pamoja)
Mama:
sana
Liliana:
atakufa
Mama:
na UKIMWI au?
Liliana:
(anajichekesha)
Mama:
hapo alipo nasikia anao (anacheka) mimi nami mmbea
Liliana:
wala hata sio mmbea unasema tu
Mama:
(anacheka)
Liliana:
kwani hana familia?
Mama:
nasikia anayo watoto watatu na mke
Liliana:
wanaishi wapi?
Mama:
Canada
Liliana:
sasa yeye anafanya nini huku?
Mama:
ana miradi baba ana miradi baba tajiri huyu mpaka sio poa haki ya nani
Liliana:
eti ee ndo anawadanganyia wanawake pesa zake
Mama:
wanawake nao wanataka wenyewe…mimi mwenyewe ningekuwa siogopi UKIMWI ningemuendea
nikajipendekeza
(Wanacheka)
Liliana:
unaogopa UKIMWI siku hizi mbona Malaria tu hiyo?
Mama:
pamoja na kwamba ni hivyo bado ni tishio
Liliana:
hamna wewe tulia mbona watu wanaishi nao miaka 20,30 inategemea tu unajilinda
vipi na unatumiaje dawa
Mama:
(anaguna) haya bwana nitajipendekeza
(Wanacheka)
Mama:
mama chumba chako ndo hiki
Liliana:
asante
Mama:
haya acha nikuache ila ndo huna hata pa kukaa
Liliana:
usijali kuhusu mimi
Mama:
(anatoka)
Liliana:
(anachungulia dirishani kwa mbali
anamuona Robert) muone alivyo hana hata haya huyu mwanaume ambae sijui
alitapikwa au alifanywaje? Ona anavyowaua watoto wa watu kwa maradhi kwa
kuwalaghai kwa pesa na zawadi ndogondogo baada ya hapo akutane na mama zao
awatamani pia wale mama wamkatae awaue kama alivyofanya Kwa mama yangu sasa
kabla hajafanya huu ujinga lazima nimuue hawa watu hawatakiwi katika hii dunia
Robert:
(anamshika kiuno mrembo aliyekuja nae
mahali hapo) mrembo tamba mama tamba leo zamu yako
Mrembo:
(anajichekesha) Robert pedeshee
Robert:
ewaaaaaaa
Liliana:
(akiwa chumbani kwake) tamba tu wewe
tamba tu mwisho wako unakuja sijui utanijibu nini
Robert:
(anaonekana kufurahia maisha na mrembo)
Mrembo:
daddy una nyumba nzuri
Robert:
mimi ndo Rob mapesa mama sema utakacho mimi nitakupa
Liliana:
(anachungulia dirishani) wewe
unafurahi wakati mama yangu amelala mauti tena hata maiti yake hatukuipata
ilikuwa ni majivu (anatokwa machozi)
nakuchukia sana Robert ile nguvu niliyokuwa nayo ya kukupenda imebadilika kuwa
chuki mbaya sana najuta hata kwanini nilikuwa mpenzi wako sikukujua wewe ni
mwanaume mbaya sana na Mungu akusamehe nakuchukia sana
Robert:
(anaendelea kufurahia maisha kama kawaida)
napenda wanawake wembamba tena wenye mironjo kama wewe
Mrembo:
jamani daddy mbona unanitukana tena jamani
Robert:
no baby sikutukani (anacheka)
Liliana:
(anang’ata meno) cheka Robert cheka
sana tena kazana kucheka maana umeamua kucheka furahia ila nakuhakikishia
majira kama haya na wewe utabaki majivu utalala mauti (Analia sana) mama yangu (anakumbuka
matukio muhimu aliyofanya na Bianca kuanzia alipochukuliwa kutoka mitaani mpaka
kusomeshwa na kulelewa vizuri bila shida, mapenzi yote aliyoonyeshwa na Bianca)
mama yangu... wewe Mungu uliyenipokonya wazazi kisha nikaishi kwa dhiki kubwa
kisha ukanipa mama aliyenilea vizuri kwa upendo na kwa mapenzi yako ukamchukua
naomba ujibu kwa moto this time sitasamehe nilimsamehe shangazi na mjomba wangu
kwa kunifanya kijakazi ndani ya nyumba ya wazazi wangu naomba unisamehe
sitasamehe
Robert:
(anaendelea kufurahia maisha na mrembo)
Mrembo:
daddy naomba basi uninunulie gari
Robert:
sema aina gani mrembo hapa ni kwa mapesa ni wewe tu jitahidi kunipa mapenzi ya
kweli leo hii wallahi utaondoka na gari unaweza kuchagua hapa au tukaenda show
room
Mrembo:
(kwa madeko kidogo) nataka show room
daddy
Robert:
imekuwa mrembo (anambusu mdomoni)
Liliana:
(anafyonza) lione
Robert:
(hana habari kama Liliana anamuangalia)
Mrembo:
twende ndani daddy nikakupe mambo adimu
Robert:
mmmmh hamna jipya na uzee huu unadhani sijawahi kupata mambo yote?
Mrembo:
(anabaki anashangaa)
Robert:
(anacheka kwa nguvu) nakutania ila
siku nyingine usiseme kuwa unataka kunipa mambo adimu nitakushangaa sio mimi tu
bali mtu yeyote anayepita hapa atabaki anakushangaa
Mrembo:
sawa daddy
Robert:
usiniite daddy hilo jina linanikumbusha mtu mmoja ambae tulimaliza vibaya sana
kitoto kilikuwa kinanilia pesa kidogo kinifilisi (anamkumbuka Liliana) anyways sitaki kukumbuka alinisababisha
nikamfanyia kitu kibaya sana mwanamke nimpendae kwa dhati namchukia ilikuwa
kwasababu yake yule mwanamke alinikataa kabisa (anamkubuka Bianca) alikuwa ni mwanamke mrembo sana (anakumbuka tabasamu la Bianca)
Mrembo:
daddy
Robert:
(kwa ukali) get out…toka
Mrembo:
(anashangaa huku anaondoka)
Robert:
(anamkumbuka Bianca sana) oh my God
nilifanya nini?
Liliana:
(anamuangalia anavyohangaika) mzimu
wa mama yangu hautakuacha kirahisi Robert
Robert:
nilimpenda sana Bianca nilifanya vile kwa hasira na wivu maana alikuwa anaolewa
na mwanaume mwingine
Liliana:
suffer Robert suffer (anatabasamu)
0 Comments