I KILLED MY LOVER 58

 


SCENE 58: -

HOSPITALINI: -

(Raphael anafika hospitali akiwa amembeba mpenzi wake mikononi mwake na anaonekana akiwa amechanganyikiwa kwa hali ile)

Raphael: nesi naomba msaada wako

Nesi: (anamjia) amefanyaje?

Raphael: sijui nesi nimemkuta amelala sakafuni

Nesi: (anaenda kuchukua machela na kurudi nayo)

Raphael: ameumia Sana na wala haongei wala kufumbua macho

Nesi: atakuwa sawa usijali (anamuita daktari) naaomba utusaidie huyu mgonjwa yuko very critical

Raphael: please msaidieni

Nesi: hakuna kitakachoharibika kaka punguza presha

Raphael: Ni mwanamke nimpendae Kwa dhati na ameishi maisha ya mateso sana sitaki aendelee kuishi maisha ya mateso

Nesi: atakuwa sawa…she will be fine you will see

Daktari: (anakuja kutoa msaada na haraka anaamuru mgonjwa apelekwe katika chumba cha wagonjwa mahututi) haraka mgonjwa akimbizwe ICU

(Wauguzi na wasaidizi wao wanahangaika na hali ya Liliana wakati huo raphael anaonekana kuchanganyikiwa kupita kiasi)

Raphael: dear God I hope atakuwa sawa (anachukua simu yake mfukoni kwake na kubonyeza namba ya kaka yake mkubwa)

(Simu inaita)

Gabriel: oyaaa bwana harusi

Raphael: kaka Liliana yupo hospitali

Gabriel: (anaishiwa tabasamu) kwanini? Imekuwaje? Amefanya nini?

Raphael: sijui yaani I can’t explain kaka hali yake sio nzuri

Gabriel: oh my God nambie uko wapi tunakuja

Raphael: (anamuelekeza)

Gabriel: okay tunakuja (anakata simu kasha anamgeukia Anna, Bella na Michael) Liliana yupo hospitali

Anna: what do you mean yupo hospitali? Amekuwaje?

Gabriel: Rapha ahajaniambia vizuri ila najua tu hana hali nzuri

Bella: sasa tunasubiri nini twendeni

(Haraka wanatoka nje wanapanda gari moja na kuondoka zao)

HOSPITALI: -

(Raphael amekaa amejiinamia hana raha ya maisha machozi yanamdondoka na anaonekana ana mawazo sana, wakati amejiinamia anashtuliwa na sauti ya kaka yake mkubwa)

Gabriel: Raphael?

Raphael: (ananyanyuka na kumkumbatia kaka yake kwa nguvu)

Gabriel: it is okay she will be fine my brother

Raphael: (anafuta machozi) asanteni Kwa kuja

Anna: NO, it is okay shemeji, Liliana anaendeleaje? Na mtoto yuko wapi?

Raphael: yupo na mama

Bella: how is my cousin?

Raphael: madaktari wameingia nae ICU bado hawajatoka yaani mwenzenu sielewi

Michael: kwani imetokea nini mpaka yupo hapa? Ameugua ghafla?

Raphael: nimemkuta sakafuni kazimia sasa sijui aliteleza yaani sielewi

Gabriel: My God hiyo ni mbaya

Anna: let’s hope for the best Nina Imani atakaa sawa

Raphael: namuwazia mgongo asije akawa kilema

Bella: no shemeji usiwaze kote huko ukiwaza hivyo ndo unazidi kuchanganyikiwa wewe amini tu kuwa Mungu atamtendea liliana is very good woman…moyo wake upo so pure anasamehe na anawapenda watu wote she is very good jamani kwakweli namuombea tu apone

Raphael: amina shemeji yangu

(Wanaendelea kupeana moyo na Imani ya hapa na pale)

Daktari: (anatokea chumba cha wagonjwa mahututi)

Raphael: (haraka ananyanyuka na kumfuata) daktari

Daktari: come down

Raphael: anaendeleaje?

Daktari: ah

(Wote wanamuangalia Kwa umakini na wasiwasi mkubwa)

Daktari: haikuwa mbaya Kama tulivyodhani naona wote tulipaniki wakati analetwa

Bella: kwahiyo

Daktari: anaendelea vizuri na amezinduka pia anaendelea vizuri

Raphael: naweza kumuona?

Daktari: yes, sure ila ngoja tumtoe humu tumpeleke chumba cha mapumziko

Raphael: saa ngapi sasa?

Daktari: ona ni sasa hivi tu

(Machela inapita ikiwa imembeba Liliana)

Raphael: oh, baby you gonna be fine my love

Liliana: (kimya hasemi kitu ila anatabasamu)

Raphael: yes... (Anafurahi Sana)

Gabriel: nilikuambia kuwa kila kitu kitakuwa sawa

Raphael: sawa Asante Sana my brother

Gabriel: usijali

Nesi: mnaweza kumuona sasa

(Wanaingia chumba alichopo Liliana)

Raphael: oh, Mama Bianca wangu

Liliana: (anaongea Kwa shida kidogo) ye…sss

Michael: pumzika Kama hujisikii vizuri shemeji

Gabriel: uliteleza?

Liliana: (anatikisa kichwa kuashiria kukataa)

Michael: mtu alikusukuma?

Liliana: (kimya)

Raphael: nani amekufanyia hivyo baby? Answer me please

Liliana: (Kwa shida) ki…ng

Raphael: hapohapo huyu mshenzi atajua hajui Leo ngoja

Bella: tulia shemeji it is not worthy it…akae anajua tu amekukosa wewe Kama rafiki hayo mengine achana nayo

Anna: kabisa shemeji tumshukuru Mungu tu Kwa kila jambo maana hata kupona Kwa mpendwa wetu ni jambo la kushukuru sana

Gabriel: kabisa achana na King tupange harusi

(Wanacheka)

Raphael: (anashusha pumzi Kama mtu aliyechoka Sana)

Post a Comment

0 Comments