I KILLED MY LOVER 60 (MWISHO)

 


SCENE 60: -

FINALE: -

BAADA YA MIEZI 10: -

 (Ni asubuhi nyingine njema Kama ilivyokusudiwa na Mungu muumbaji, Liliana akiwa katika hali ya ujauzito tena uliofikia hatua ya kujifungua, anaingia katika moja ya supermarkets za mumewe kufanya manunuzi ya nyumbani, wakati anaingia simu yake ya mkononi inaita)

Liliana: (anaipokea) baby

Raphael: nimekuja nyumbani mara moja kukuona haupo umeenda wapi na hii hali baby?

Liliana: nipo Ra-Li supermarket baby

Raphael: okay nakuja hapo usiondoke

Liliana: (anacheka kidogo) baby bwana iam okay nanyoosha viungo tu jamani

Raphael: no baby unatakiwa upumzike bwana nakuja hapo (anakata simu)

Liliana: (anatikisa kichwa kisha anatabasamu) ila huyu kaka (anacheka)

(Anakaribishwa Kwa heshima zote)

Liliana: asanteni jamani hamjambo? (Anaanza mahemezi ya hapa na pale)

(Sauti ya kiume kutoka nyuma yake inamuita)

Liliana: (anageuka kuangalia ni nani) nani?

King: Mimi hapa shemeji

Liliana: oh, Shem za siku?

King: nzuri Sana (anatabasamu) hongera Kwa harusi lakini pia naona mambo sio mabaya

Liliana: (anaangalia tumbo lake) eeh shemeji

King: hongereni Sana na samahani kwa yote

Liliana: oh, shemeji hayo ni ya kale tuachane nayo sio lazima kukaa kukumbushiana

King: kwakweli ila lile jambo limeharibu urafiki wangu na Rapha

Liliana: hana kinyongo tena namjua mume wangu habebi vinyongo

King: eti eeh basi Kama ni hivyo safi sana

Liliana: kuwa na Amani

King: basi sawa acha niendelee na mahemezi ya hapa na pale

Liliana: karibu Sana shemeji

King: nipo na wife nay eye yupo kama wewe

(Wanacheka)

Mrs.King: (anaugulia) baby

King: (anakuja anakimbia) vipi baby

Mrs.King: tumbo

Liliana: (anakuja kuwasaidia ile anapiga hatua nae anasikia uchungu ghafla)

Wafanyakazi: (wanakimbia kuwasaidia)

Raphael: (anafika) nini kinaendelea hapa

Mmoja wa wafanyakazi: queen anaumwa

Raphael: oh My God (anakimbia kumuona anakutana na King) aisee na wewe, mkeo amepata uchungu

King: yes

Raphael: (anambeba mkewe) lets go twendeni hospitali

(Haraka wanapanda gari kuelekea hospitali baada ya mwendo kidogo wanafika hospitali na kama kawaida manesi wanawapokea vizuri, wanawake wale wawili wanapelekwa leba wakati wanaume wanabaki nje kusubiria habari njema)

King: (Kwa Raphael) hatujaonana mwaka sasa ndugu yangu

Raphael: ni kweli

King: nisamehe Sana Kwa lile tukio halafu sio hilo tu hata la kumchukulia mkeo Malaya kutembea na baba na mwana

Raphael: oh, King Hilo limepita ndugu yangu tugange yajayo rafiki yangu…nimekusamehe ondoa shaka

King: (anampa mkono)

Raphael: (anamvuta) come here (anamkumbatia)

(Wakati wamekumbatiana ndugu zake Liliana pamoja na Raphael wanafika mahali pale)

Bella: shemeji?

Rphael: naam Shem

Anna: huyu vipi?

Raphael: ah bado tu ndugu yangu

Gabriel: don’t worry she will be fine

Michael: Na King Anafanya nini hapa?

King: kaka

Raphael: it is okay (Kwa Michael) yupo hapa maana na yeye mke wake kaingia leba na mke wangu

Lydia: (anafika hospitali hapo)

Wote: (wanamsalimia)

Lydia: marahaba

Raphael: Bianca yupo wapi?

Lydia: shule

Gabriel: mbona umekuja umetoa macho hivyo?

Lydia: (anacheka) nimeambiwa bibie kapata uchungu vipi anaendeleaje?

Raphael: ndo tunasubiri hapa

Lydia: she will be fine

Raphael: I know mama but iam very nervous

Michael: tunaelewa bwana ndo mara ya kwanza kuwa baba ni lazima uwe na mhaho wa adabu

(Wanacheka)

Raphael: yaani nyie mnanichanganya tu bwana

Gabriel: wewe nae tusicheke

Lydia: unajua mwenzenu yupo serious amechanganyikiwa

Michael: mama take it easy jamani mbona hivyo?

Gabriel: mama is going to be a very sexy granny

(Wote wanacheka)

Raphael: let’s get serious guys

Michael: hey chill nini mbaya jamani?

Raphael: akili yangu haipo

Gabriel: then….

(Sauti ya kichanga inasikika kutoka katika chumba walichopo mke wa King na liliana)

Raphael: (anafurahi Sana) Oh My God mwanangu

King: (anafurahi pia)

(Vilio vya watoto vinasikika, vilio vile vinaleta furaha Kwa watu wote waliokuwepo hapo)

Raphael: wow…iam a father

Gabriel: (huku anatabasamu) yes, my little brother

Raphael: Asante Mungu

Lydia: (anafurahi Sana mpaka anajikuta anatoka machozi)

Anna: aunt vipi mbona machozi?

Lydia: sikuwahi kufikiri Kama hata siku moja nitawahi kufurahia furaha ya Liliana nilimuona Liliana Kama ni shetani aliyekuja kuharibu furaha ya familia yangu (anasikitika) Liliana ni shujaa ameteseka sana katika maisha yake nimesikia hadithi ya maisha yake na nimeelewa ule usemi unaosema hata kama usiku ukiwa mrefu vipi lazima papambazuke naona kwa Liliana pameshapambazuka (kwa Raphael) hongera mwanangu kwa kuwa baba

Raphael: Asante mama (anamkumbatia)

(Wote waliopo pale wanakumbatiana huku kila mmoja anaonekana kuwa na furaha isiyo na kifani)

Dokta: (anatoka anawakuta wamekumbatiana) naona mmeshapata jibu

Lydia: yes tumepata

Dokta: Mrs.Liliana amejifungua mtoto WA kiume na Mrs. King amejifungua mtoto wa kiume pia hongereni sana

(King Na Raphael wanakumbatiana)

Lydia: Asante Mungu finally everyone is happy

Anna: tunaweza kumuona I mean kuwaona?

Dokta: yes, sure please go ahead

(Wanaingia Kwa pamoja kumuona Liliana pamoja na mke wa King)

Raphael: oh, my wife

Liliana: it’s a boy

Raphael: (huku anatabasamu) I know baby I know…hongera Sana my love

Liliana: hongera kwetu sote mpenzi

Anna: hongera Sana cousin

Liliana: thank you cousin

(Watu wote waliopo hapo wanawapongeza wazazi Kwa kuleta furaha kwenye familia hizo mbili)

Lydia: hongera Sana

Liliana: Asante Sana mama

Liliana: (anaongea mwenyewe moyoni) all is well…it ended well and iam so proud…yes nilipitia magumu sana tangu wazazi wangu walipofariki nilitukanwa nilifanyishwa kazi kwenye nyumba yangu mwenyewe, nilibakwa nilinyimwa chakula lakini pamoja na yote Mungu hakunitupa nikampata mama yangu Bianca (anatabasamu kidogo) mama yangu Bianca akanilea akanisomesha niliishi maisha mazuri ghafla nikaona usemi uliosema baada ya dhiki faraja nikafarijika sana nikamtukuza Mungu sana lakini siku moja tu nikaamua kupenda hapo ikawa mwanzo wa mateso yangu bwana yule aliniharibia maisha yangu kwa kunipa gonjwa ambalo ni tishio lakini pamoja na hayo Mungu hakuniacha nikaendelea kufurahi sana kwasababu mama yangu alikuwepo kunipa moyo lakini furaha yangu haikudumu hawara yangu akamuua mama yangu sikukubali na mimi nikawa na kisasi moyoni mwangu kilichopelekea kumuua hawara yangu sitasahau mateso niliyoishi nayo nikafungwa miaka ila ndani ya miaka minne nikatoka silalamiki nilipotoka ndo furaha ikanizidia maana nilipata tulizo la moyo…(huku anamuangalia mumewe) mume wangu Raphael mtoto wa hawara yangu pamoja na kwamba watu walimwambia asinioe hakuwa sikiliza hata mimi mwanzoni niliona kuwa haitakuwa vizuri mimi kuwa nae yeye alitumia nguvu nyingi sana kunishawishi kuwa kila kitu kitakuwa sawa na leo kweli kila kitu kipo sawa nimezaa na baba na mtoto and all is well ndo Mungu alivyopanga asante sana jehova kwa upendo wako sina cha kukurudishia ila nitaziimba sifa zako siku zote za maisha yangu

Bella: (anamshtua) wewe binamu unawaza nini?

Liliana: hapana siwazi kitu just nafurahi ukuu wa Mungu

Gabriel: Mungu wetu ni mzuri sana

Michael: kabisa

Raphael: hakika

King: hakika

Anna: kabisa

Lydia: kila kitu kipo sawa (anambeba mtoto mchanga) anaitwa nani mtoto?

Raphael: bado hatujamuita jina lolote hatukupanga

Gabriel: au hamkupanga mtoto wa kiume

Liliana: (anacheka kidogo) hapana shemeji sisi tulijiandaa kwa ajili ya mtoto yeyote

Raphael: yes

Lydia: ataitwa Robert

(Wanashangaa)

Raphael: mama

Lydia: au?

Anna: Mimi naona sawa tu

Liliana: (anacheka)

Lydia: msamhee Robert Liliana mwanangu

Liliana: (anatabasamu) sawa nimemsamehee na mwanangu ataitwa Robert

(Wanafurahi Sana)

Bianca: (anakuja akitokea shuleni) mama

Raphael: (anambeba) umepata mdogo wako mwanangu

Bianca: (anafurahi Sana)

(Wote walipo hapo wanafurahi Sana na kila mmoja anaonekana kuridhika na hali ile ya wakati ule)

Raphael: all is well

Gabriel: tungekuwa na shampeni sasa

(Wanacheka na kufurahia maisha kwa ujumla)

THE END

Post a Comment

0 Comments