MUNGU MKUU 1

 


SCENE 1: -

(Ni usiku mmoja wa giza totoro,na mvua kali inanyesha,katika mtaa mmoja wa pembeni ya  mji anapita mama mmoja anayeonekana kubeba mtoto mchanga na kwasababu ya mvua kali anaonekana kukimbia na kutafuta nyumba ya kujikinga na mvua hiyo,baada ya kuhangaika kwa muda mrefu hatimaye anafika kwenye nyumba moja ya kifahari,kwakuwa mageti yamefungwa,anaamua kutandika khanga yake kisha anaondoka huku anamuacha mtoto mahali pale,lakini kabla ya kuondoka anabonyeza kengele ya geti ya nyumba ile ya fahari,anabonyeza mara kadhaa kisha kwa mbali anasikia kama kuna mtu anafungua mlango kwa ndani anakimbia na kujibanza sehemu huku akiangalia hatima ya mtoto wake mchanga,wakati huo amejificha anatoka mwanamke mmoja pamoja na mwanaume wawili hao wanaonekana ni wanandoa na wamiliki halali wa nyumba hii)

Mwanamke :( anaonekana ana usingizi Sana) jamani nani tena amegonga geti tumetoka hatumuoni

Mwanaume: sijui nani? (Anamuita mlinzi) Edson…

Edson :( anatoka) naam boss…

Mwanaume: unaweza ukawa unajua mtu aliyekuwa anatugongea?

Edson: hapana boss, sijamuona …

Mwanamke: ah…sawa, Kennedy umeshajua kuwa hakuna mtu embu turudi ndani bwana mi nina usingizi…

Kennedy :( anacheka) Kedness, kwa usingizi jamani unataka kuzidi haya twende

(Kabla hawajapiga hatua kwenda popote wanasikia mtoto kwa pembeni Analia na wakati huo wote mama mzazi wa mtoto huyo yupo sehemu pembeni amejibanza akiangalia hatima ya mtoto wake)

Mama :( anaonesha masikitiko) nisamehe mwanangu, unadhani nitafanyaje? sina uwezo wa kukulea…baba yako amenikataa na kunitukana matusi mengi na mabaya unadhani hata mimi napenda kukuacha hapa? baba yako kakukataa, bibi na babu yako hawakutaki, waliniambia hata kabla sijakuzaa kwamba inanipasa nikutoe mwanangu lakini mimi kiubishi nimekuzaa ila sina uwezo wa kukulea mwanangu, namuomba Mungu hawa watu wakuchukue tu uwe mtoto wao…

(Wakati huo Keneddy na mkewe Kedness wanashangazwa na mazingira aliyopo kichanga hicho)

Kedness: maskini, na baridi lote hili…mwanamke gani mwenye roho ngumu kamuacha mtoto hata kumfunika?

(Mama wa mtoto Analia kwa uchungu)

Kennedy: yaani dah

Kedness :( anamnyanyua yule mtoto) halafu kazuri kweli…

Keneddy:ni wa jinsia gani?

Kedness :( anamfunua kidogo) ni wa kike…

Kennedy: kwanzia leo atakuwa mtoto wetu

Kedness: wewe ni bora tukatoe taarifa polisi ili kusije kukawa na kesi, anaweza kuja mama yake na mtoto na kusema kuwa tumemuiba na tukapata kesi kubwa mume wangu

Kennedy: sawa haina shida ila polisi wakikosa mama yake Ariana wetu atapata mdogo wake

Kedness: ama hakika Ariana atafurahi sana maana alitaka sana kuwa na mdogo

Kennedy: mvua naona inazidi unaonaje tukaingia ndani?

Kedness: kwanza tumpe mtoto wetu mpya jina...

Kennedy: wewe umesema kuwa mpaka tukatoe taarifa polisi

Kedness: sawa ila polisi wanaweza wakatupa tumlee kwahiyo tunachotakiwa kufanya ni kumpa jina tu sio kwa ubaya…

Keneddy: sawa Keddy…tukisoma kutoka tunaona Mussa alizaliwa na kuwekwa katika mazingira haya haya tuliyomkuta huyu mtoto

Keddy: Ken, unamaanisha tumuite mtoto Mussa?

(Kwa pamoja wanacheka)

Ken: hapana mama Ariana, Mussa alikuwa ana dada yake tumuite mtoto Miriam...

Keddy: Safi…Miriam linafaa

(Mama wa mtoto anaonekana kuridhiana na jina la mtoto)

Mama: Miriam…jina zuri sana…hata mimi nimelipenda...

(kwa Kennedy na mkewe)

Ken: bwana akamfanye kuwa mtumishi wake (anamshika na kumuinua juu) Miriam ukawe faraja katika familia yetu, nakutamkia mema katika maisha yako, Mungu aliyewakumbuka waisraeli jangwani akakukumbuke hata wewe na maisha yako, bwana akakutendee yaliyo mema na hila zote za shetani zikakupite mbali mwanangu, nakukaribisha nyumbani kwangu na hata kama si mwanangu, nitakulea na kukupa kila kitu, elimu nzuri na kila kitu utakachohitaji katika maisha yako

Keddy: amina mume wangu sasa tumepata binti mwingine

Mama wa mtoto :(akiwa bado amejificha) amina (anajikuta anatokwa na machozi)

Ken: twende ndani mke wangu bwana ametupa mtoto wa pili katika njia zake alizopanga mwenyewe

Keddy: Amina mume wangu

Mama :( anaondoka zake na kwenda pasipojulikana)

(Ken na mkewe wanaingia ndani na kumuamsha binti yao mwenye mkubwa mwenye kati ya miaka kumi au kumi na mbili)

Ken: Ariana…unamuona mdogo wako anaitwa Miriam

Ariana :( anafikicha macho na anaonekana ana usingizi sana) mmetoa wapi?

Keddy: Mungu katuletea

Ariana :( anaguna) amewaleteaje?

Ken: tumemkuta hapo nje mwanangu yaani ni miujiza tu ya mungu mwenyewe

Ariana :(anamuangalia mtoto) sawa ni mzuri…

Ken :( tabasamu linapotea usoni mwake) mbona unaonekana huna furaha?

Ariana: nataka mdogo wangu wa kiume?

Keddy: mwanangu ni jambo la kumshukuru Mungu kuwa ametuletea mtoto na sisi familia yetu iwe kubwa tafadhali usiwe hivyo.

Ariana: samahani mama

Ken: usijali mama, we lala kesho shule tutazungumza kesho asubuhi

Ariana: sawa (anajifunika blanketi)

(Ken na mkewe wanatoka chumbani humo wanazima taa kisha wanaenda chumbani kwao, wanapofika wanamvalisha baadhi ya nguo za Ariana za utotoni maana walizitunza na kumfunika mtoto vizuri kisha wanamlaza pembeni yao)

Keddy: kile kitanda cha Ariana tulikigawa, itabidi tumnunulie kitanda chake mwenyewe

Ken :( anacheka) naona jinsi unavyopanga utasema mtoto keshakuwa wa kwako, itakuwa kesho kama mama yake atatokea?

Keddy: Mungu ametupa mtoto baada ya kumtafuta mtoto Zaidi ya miaka kumi kila mara tulijaribu kupata mtoto mwingine Zaidi ya Ariana ilishindikana leo hii kwa namna ya pekee mtoto ameachwa nje ya geti letu Mungu alikuwa anajua kuwa tunahitaji mtoto ndo akatupa huyu mtoto kwa njia ya ajabu kweli mungu ni mkuu na njia zake hazichunguziki…

Ken: amina mke wangu kesho asubuhi tutaenda polisi na kutoa taarifa juu ya huyu mtoto

Keddy: sawa, ila kuna kitu kingine kinanitatiza, Ariana mbona hajafurahi huku alikuwa anahitaji mdogo wake?

Ken:mpe muda si unajua kuwa imekuwa ghafla sana, tusubiri kesho tuone itakuwaje?

Keddy: tusubiri…tu (anamuangalia mtoto aliyekuwa kalala fofofo) yaani sijui akikojoa usiku tutamvalisha nepi gani hatuna pampers wala nepi…

Ken:(anacheka) mpaka unatamani Mungu angekuotesha kuwa utapata mtoto usiku kwahiyo jiandae

Keddy:(anacheka) yaani nimempenda Miriam ana sura nzuri kweli (anamuegemea mumewe kifuani)

Ken: naomba mtu yeyote asijue kuwa Miriam sio mtoto wetu, tutamlea kama vile mtoto tuliyemzaa wenyewe…

Keddy: sawa mume wangu sitamwambia yeyote, ila watu hawakuniona na mimba(anacheka)

Ken:(anacheka) Mungu atatutetea

Keddy:(anatabasamu) haya mume wangu…usiku mwema baba

Ken:na kwako pia

(Kila mtu anageukia upande wake na kulala, wakati huo na mtoto nae kalala fofofo)

 

 

Post a Comment

2 Comments