MUNGU MKUU 17

 


SCENE 17: -

(Mchana mtulivu, jua linawaka kwa mbali, upepo unavuma vyema ndege wanapita mawinguni na kila kitu kinaonekana katika hali nzuri, Miriam amekaa peke yake chini ya mti mmoja uliopo chuoni kwao akiwa anajisomea mwenyewe. Wakati anajisomea anakuwa ana mawazo Fulani)

Miriam: yaani mimi sijui nani aliniambia nikubali huu ujinga ona sasa nampenda Jeremy na sipo tayari kuachana nae…

Vanessa:(anakuja anakaa pembeni yake)

Miriam:(kwa kuwa anakuwa na mawazo hasikii)

Vanessa:(anamgusa) Miriam?

Miriam:(anashtuka) abee

Vanessa: unawaza nini?

Miriam:(anashusha pumzi)

Vanessa: nini?

Miriam: nampenda Jeremy

Vanessa: (anacheka kwa nguvu) eh bwana dah!!! Mambo sio ndo hayo… (anacheka kidogo tena) sasa kuna shida gani ukimpenda?

Miriam: Vanessa wewe unajua kabisa tangu mwanzo inshu ilikuwa ni kujifanya kuwa nae ili asijidhuru lakini sasa kila siku zinavyozidi kwenda ndo nataka kuendelea kuwa nae…nampenda nipo serious nae, yaani hivi unadhani wazazi wa pande zote mbili watanionaje mimi?

Vanessa: wataelewa kuwa penzi kikohozi jamani kinampata mtu yeyeote wewe tulia na uchukulie poa tu...kwani wewe ulipenda si imejitokeza tu?

Miriam:na wala sikupanga kuwa nitampenda imetokea tu

Vanessa: sasa je…wewe tulia tu na uendelee kula good time…zikiisha unaongeza… (anapiga vigelegele)

Miriam: hivyo vigelegele vipi?

Vanessa: nachukulia picha siku mnaoana na baby Jeremy…

Miriam: yaani hiyo itasubiri sana maana (anaguna)mpaka nimalize shule

Vanessa: wewe si ulisema Jeremy anataka kuoa ndo maana aliwaambia wazazi wake kuwa wamtafutie mchumba

Miriam:(anacheka kidogo) mimi aliniambia kuwa yupo tayari kusubiri…nikimaliza kusoma na nikawa tayari kwa ndoa basi tutafunga ndoa

Vanessa: mmeshapanga mpaka ndoa

Miriam: yeye ndo huwa anazungumzia sana

Vanessa:(anacheka) by the way yaani mnapendezeana sio yeye na Ariana sema siku Ariana akijua wewe ndo unamchukulia bwana na hivi hakupendi sijui itakuwaje

Miriam: yaani mimi mwenzenu sijui itakuwaje…

Vanessa:na Ariana ana gubu yule sijui tu…hivi siku hizi ameacha kwenda club

Miriam: hajaacha yaani mama na baba wanaona kuwa akiolewa atatulia maana sio kwa sifa mbaya anazoiletea familia

Vanessa:na ni mhuni juzi tu nilimuona anaingia gesti na baba Fulani hivi

Miriam:(anashangaa) wewe, enhe ikawaje?

Vanessa: sasa iweje? mi nikapita zangu nikaondoa nilikuwa napita tu

Miriam:(anasikitika kidogo) yaani sijui ndo stress zenyewe za kuachwa na Jeremy

Vanessa: wala…wewe unamjua Ariana na usivunge humjui dada yako…na sio kwamba anataka kuolewa bado anataka kula ujana, ndo maana mimi naona wewe na Jeremy mnaendana maana wote mnajiheshimu

Miriam:(anatabasamu) yaani nampenda Jeremy na ile rangi yake

Vanessa:(anacheka sana) angalia usije ukawa chizi…

Miriam: usimwambie mtu lakini…yaani iwe siri yetu rafiki yangu

Vanessa: usijali mami

(Kwa mbali anakuja kijana mmoja)

Vanessa: Fredrick huyo hapo

Miriam: yuko wapi

Vanessa: anakuja utamuona tu…enhe!!unajua kuna kipindi ulianzaga kumpenda Fredrick sema nay eye sasa akawa anakuletea pozi

Miriam: hilo ndo kosa lake yaani kunitongoza anitongoze yeye halafu aanze kuniletea pozi utasema sijui ni mwanamke Fulani

(Wanacheka)

Vanessa:(kwa kunong’ona) amefika

Fredrick:(anawafikia) we Miriam…mbona hata simu zangu hupokei una shida gani?

Miriam:(anacheka) sasa hapo nikujibuje? okay sijisikii kuzijibu

Fredrick: wewe mtoto siku hizi umeota mapembe ee

Miriam: sikiliza nikwambie wewe sijui Fredrick sijui Fred huna mamlaka ya kuniongelesha jinsi unavyoniongelesha sasa hivi…yaani ni kwanini unaniongelesha kama umenizaa au una mamlaka na mimi?

Vanessa:(kimya)

Miriam: wewe ni nani kwani?

Fredrick: mimi ni nani kivipi inamaana hujui mimi ni nani?

Miriam: wewe ni Fredrick

Fredrick: mimi ni mpenzi wako

Miriam: hakukuwahi kuwa na mahusiano kati yetu na wala hayatawahi kuwepo

Fredrick:(anamfyonza) unajifanya mtoto wa mchungaji huku unabadilisha wanaume kama nguo

Miriam: una uhakika na unachokisema?

Fredrick: sasa kama umeniruka si inamaana una mwanaume mpya tena katika maisha yako

Miriam:(ananyanyuka) Vanessa twende (anataka kuondoka)

Fredrick:(anamvuta) unaenda wapi

Miriam:(anamsukuma) niache

Fredrick:(anamvuta kwa nguvu)

(Sauti ya Jeremy inatokea nyuma yao)

Jeremy: kuna nini kinaendelea hapo?

Vanessa:(anageuka) eh bwana ee kama staa kwenye muvi…(anacheka)

Jeremy:(anawaendea walipo) kuna nini?

Fredrick: hayakuhusu…

Jeremy: sikuulizi wewe...namuuliza Miriam (kwa Miriam) honey kuna nini?

Miriam:(macho yamekuwa mekundu sababu ya hasira)

Jeremy: Miriam!!???

Miriam:(kwasababu ya hasira machozi yanamtoka)

Fredrick: oh, kumbe haka ndo kamwanaume ambako kamekufanya unikatae mimi na kusahau tulipotoka

Vanessa: muongo hawakuwahi kuwa na mahusiano

Jeremy:(kwa Miriam na Vanessa) twendeni

(Wanaondoka)

Fredrick: unadhani mtafika mbali basi tunawahesabia siku tu…shenzi nyie mtaachana tu (anaondoka)

Jeremy: (anamgeukia Fredrick anamsikitikia)

Miriam: (amejaa kifua kwa hasira)

Jeremy: baby take it easy (anafika alipoegesha gari lake na kutoa chupa moja ya maji) kunywa maji kidogo, tulia baby (anamuangalia Vanessa) si mmemaliza vipindi…twendeni mkale kisha nitawapeleka nyumbani

Vanessa: okay shemeji

(Wanapanda kwenya gari kisha wanaondoka mahali pale)

Jeremy: (kwa Miriam) relax baby

Post a Comment

0 Comments